NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, May 22, 2012

mahusiano, tamaduni, maumivu, hisia na ashiki

Naam katika mahusiano tamaduni na miiko mbali mbali huingilia kati. Vijana hukutana na vizingiti zaidi katika hili. Dini za kigeni zinamaoni yake katika hili wakati tamaduni na dini za kiasili nazo huwa na mitizamo yake.
Tamaduni nyingi za kiafrika zilipinga sana upatikanaji wa Mimba kwa binti kabla ya kuoelewa. Katika jamii za wahaya kwa mfano, binti aliyepata mimba katika kipindi hicho alikabiliwa na hadhabu kali ya kifo cha kikatili. Mchumba alitafutwa na kukubaliana kati ya wazazi husika na wanandoa kukutanishwa baadae
Dini nyingi za kigeni kama vile ukristo na uisilamu nazo zina tamadmuni zake kwa wachumba na wanandoa. Wale waliobahatika kupata mimba kabla ya kufungishwa ndoa na kiongozi wa dini, hupewa adhabu Fulani Fulani za kiimani kama kutoshiriki kiitwacho chakula cha bwana au hata kutengwa mbali kabisa na nyumba za ibada
Katika mahusiano ya kisasa vijana nao huja na mambo yao. Huu utumika kama wakati wa kujifunza mapenzi yenye ashiki na hisia kali. Hapa wengi hawaambiliki na hujiona wamefika na wanajua kila kitu katika massuala ya mahusiano. Kumbuka tunapokua na kujijua na kutoka nje ya nyumba za wazazi/walezi wetu, jambo kubwa huwa ni mahusiano ya kimapenzi a watu wa jinsia tofauti na za kwetu.
Huwa ni kipindi kigumu cha kujifunza masmuala haya magumu bila kufata utaratibu wowote namwisho huwa ni maumivu ya kuachana na Yule ambaye mtu aliamini ni wa milele. Hata hivyo maumivu haya huwa sio halisi kwani huko mbeleni huja kukutana na wapenzi wengine ambao hupendani sana kuliko wale wa zamani. Kuna wanaozunguka na kurudiana na wale wa zamani
Wazazi wengi hawawasaidii vijana wao katika masuala ya mahusiano isipokuwa wengi huwaingilia na kutaka kuwa tafutia wenza au hata kuwapiga mkwara juu ya mambo haya.
Ndoa hunukia kwa mbali

No comments:

Post a Comment