NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, April 3, 2012

AIRTEL YALA RAHA NA WATOTO WA WATEJA WAO JIJINI DAR ES SALAAM

 Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania wakijumuika kwa pamoja
na  watoto  wa wafanyakazi wa Airtel kukakata keki iliyoandaliwa na
kampuni ya Airtel Tanzania katika shamra shamra za tamasha maalum
kuelekea sikukuu ya pasaka ambapo watoto hao walipata nafasi ya
kucheza  michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika
kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la
Qualty center Jijini Dar-es-salaam.

 Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania wakijumuika kwa pamoja
na  watoto  wa wafanyakazi wa Airtel katika shamra shamra tamasha
maalum la watoto kuelekea kusheherekea sikukuu ya pasaka kwa michezo
mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha michezo ya
watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini
Dar-es-salaam kwa hisani ya Airtel.

 Meneja mauzo wa kampuni ya Airtel Tanzania Bi.Hilda Nakajumo akikata
keki kwa  pamoja na Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania na
watoto  wa wafanyakazi wa Airtel katika shamra shamra za  kuelekea
sikukuu ya pasaka ambapo watoto hao walipata nafasi ya  kucheza
michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha
michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center
Jijini Dar-es-salaam.

 Mkurugenzi wa Biashara  wa kampuni ya Airtel Tanzania Bw.Irene  Madeje
akizungumza na waandishi wa habari katika sherehe ya michezo kwa
Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania na  watoto  wa
wafanyakazi wa kampuni hiyo katika shamra shamra za  kusheherekea
sikukuu ya pasaka na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo kati ya wateja
wa Airtel na wafanyakazi wa Airtel ambapo watoto hao walipata nafasi
ya  kucheza  michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika
kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la
Qualty center Jijini Dar-es-salaam.

Watoto wakicheza mchezo wa kuendesha magari wakati wa tamasha maalum
la michezo kwa watoto lilioandaliwa na Airtel ili  kutoa nafasi kwa
watoto  wafanyakazi wa Airtel pamoja na watoto wa wateja wa Airtel
jijini Dar esa salaam kukutana na kucheza  michezo mbali mbali kwa
pamoja , tamasha hilo  lililofanyika katika kituo cha michezo ya
watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini
Dar-es-salaam kwa udhamini wa  Airtel 

Airtel yaanza shamra shamra za sikukuu kwa kushereheka na watoto
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel yaanza shamrashamra za sikukuu
kwa kujumuika na watoto wa wateja wao jijini Dar es saalam ambapo
watoto zaidi ya 150 walipata nafasi ya kukutana pamoja jumamosi
mwishoni mwa wiki hii  katika ukumbi wa Quality Center - Fun sports na
kufurahi kwa pamoja.
.
Huu ni mkakati ambao Airtel imejiwekea  kusherehekea pamoja na watoto
wa wateja wao wa makapuni ( corporate customer)  wiki moja kabla ya
sikukuu za pasaka huku lengo likiwa ni kuwa karibu na wateja wao na
kusambaza upendo wa kampuni hiyo kwa wateja wake na familia zao.

Akiongea kwa niaba ya Airtel Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Bi Irene Madege

alisema" leo tunajisikia furaha kuwa na watoto wa wateja wetu na
kujumuika nao pamoja, Tumekuwa tukifanya shughuli mbalimbali ikiwa ni
katika kuwazawadia wateja wetu, lakini leo tunatumia muda huu kuwapa
burudani watoto ambao ndio wateja wetu wa kesho".

Kwa muda wa takribani masaa 4 watoto zaidi ya 150 walipata burudani

mbalimbali ikiwa pamoja na michezo mbalimbali ya watoto kama  face
painting, mashindano ya kucheza music, na pia kupata nafasi ya
kukutana na wafanyakazi wa Airtel,  kumzungumza pamoja na kuwasisitiza
watoto kuwa wasikivu shuleni ili  kufanya vizuri kwenye masomo yao,
tunaamini watoto hawa wamekuwa na wakati mzuri pamoja nasi. Aliongeza
Bi Irene
.

No comments:

Post a Comment