NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, January 29, 2013

NI MFANO WAKUIGWA:UMOJA WA BAJAJI MBEYA WATEMBELEA WATOTO YATIMA SIMIKE NA KUTOA MSAADA

Umoja wa Vijana  waendesha Pikipiki za magurudumu matatu Mkoani Mbeya umeamua kuzindua mpango wa  kutembelea  watoto yatima  na kutoa misaada  kutokana na faida wanayoipata baada ya kusaijili umoja  wao na kuchana  na kutumisha  kwenye maandamano ya kisiasa  na kusababisha vurugu Jijini . Hapa umoja huo ukitoa msaada wa sukari mchele chumvi na madaftari kwa watoto yatima wa simike mbeya
Hapa wanaumoja huo wa bajaji mkoani mbeya wakimkabidhi kijana Frank Musa ada ya awamu ya kwanza kwani kijana huyo amefauru kwenda shule ya sekondari itigi lakini alikosa ada ya kwenda shule hivyo umoja huo umetoa kiasi cha shilingi 40,000/ za kuanzia ili aanze masomo
kulia nia mama janeth Njenga yeye amejitole kumsaidia mtoto Franki kwa ada na matumizi yote ya shule mpaka atakapomalisha elimu hiyo ya sekondari 
Wanaumoja hao wa bajaji wametoa msaada kwa watoto hao yatima wenye dhamani ya shilingi 250,000/
Hapa watoto hao wakiushukuru umoja wa babaji mkoa wa Mbeya kwa kuwakumbuka na kuwajali katika chakula
Mama Anna Kasile yeye ndiyo anaewalea watoto hao akiwashukuru wanaumoja hao kuja kuwaona na kutoa msaada kwa watoto hao


“sisi ni vijana ambao tumeamua kuwa wajasiliamali  ambapo tumejipanga kwa ajili ya kuinuana kiuchumi  lakini kutokana na faida tunayoipata  tumeamua kuwa tutakuwa tunaitumia kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima  katika vituo vilivyopo Mbeya  na tutazindua mpango huu mwishoni mwa mwezi.”walisema wanaumoja hao wa Bajaji mkoani Mbeya.
Picha na Mbeya yetu

No comments:

Post a Comment