NJOMBE

NJOMBE

Thursday, January 17, 2013

HIVI NI LINI WATOTO WA KIBONGO MTAACHA KUWANUNULIA BOXER WAPENZI WENU??



Haya jamani wadada wa kitanzania, wadada wa Dar es Salaam, wakaka wanaulizaa lini mtaacha kuwapa zawadi za boxer na vest na kuanza kutoa zawadi za maana kama wadada wenzenu wa nje..??


Wakionesha kuchoshwa kabisa na zawadi hizo wakaka hao walienda mbali zaidi na kutolea mifano ya zawadi ambazo wasichana wa nje wamekuwa wakitoa kwa wapenzi wao ambapo walianza na Mariah Carey ambaye alimnunulia pete mpenzi wake ambaye sasa ni mume wake Nick Cannon yenye thamani ya dola milioni mbili..



Awakuishia kwa Mariah Carey, waliendelea mbeleee, wakamzungumzia na Kim Kardashian aliyemnunulia baby dady wake Kanye West gari ya kifahari ya LAMBORGHINI yenye thamani ya dolla laki 7.5 kwenye birthday ya baby wake..




Wakamalizia kwa mama Blu Ivy Beyonce!! Alimpa mume wake Jay Z private jet yenye thamani ya dola millioni 40 kwenye Father's Day.



Lakini wao wanaambulia boxer na vest kwahiyo wanawaomba mbadilike muendane na mfumo wa digitali, hayo mambo ya vest na boxer ni analogia yashapitwa na wakati..



Hako ni kajiutani tu msichukulie kama vipi japo kunakaujumbe

WAMECHOKA!!

No comments:

Post a Comment