NJOMBE

NJOMBE

Sunday, November 11, 2012

Je unajuwa kinachoweka nyumba nadhifu:Upangaji wa nyumba


arrange
Upangaji wa nyumba hasa sebule, jikoni na vyumbani ni jambo ambalo kila mwanamke anapenda alifanye kwa ukamilifu. Tatizo linakuja muda wa kufanya hivyo unakuwa hafifu sababu ya shughuli nyingi za ujenzi wa taifa na kazi ya Mungu pia.
Kuna njia nzuri ya kukuwezesha kufanya hivyo kwa muda huo kidogo ulio nao. Kwanza angalia zile sehemu ambazo zinahitaji muda mrefu ili ziwe nadhifu, kwa mfano jikoni, kabati languo, chumba cha watoto, shelfu la vitabu n.k.
Panga muda wa dakika 15 kila siku ambao utautumia kufanya shughuli hii. Anza na eneo moja kwanza hadi umalize ndio uende sehemu nyingine, ikiwezekana weka alarm ili usitumie zaidi ya dakika 15.
Mwanzo kazi itakuwa ngumu hasa kama hukuwa na utaratibu wa kupanga mara kwa mara ila baadaye utaona ilivyo rahisi kuweka nyumba yako nadhifu bila kutumia nguvu nyingi.
Inatosha kwa leo.

Mungu akubariki sana.
Happy Sunday

No comments:

Post a Comment