NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, June 26, 2012

Mohammed Mursi kuunda serikali mpya


Mohammed Musri akifanya sala

Rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia nchini Misri Mohammed Mursi, anaanza kuunda serikali mpya baada ya kuahidi kuwa kiongozi wa raia wote wa Misri.
Viongozi wa dunia wamempongeza Kiongozi huyo aliyeungwa mkono na mrengo wa Muslim Brotherhood baada ya kumshinda Waziri Mkuu wa zamani Ahmed Shafiq.
Bw Musri anatarajiwa kuapishwa rasmi hapo Juni 30, japo kuna hoja kuhusiana na madaraka gani anapata.
Watawala wa kijeshi wamedhibiti madaraka mengi anayopata Rais pamoja na kufuta bunge.
Kwenye hotuba yake ya ushindi, Mursi aliwahakikishia raia kuwahudumia wote bila kubagua.
Mohammed Mursi anaanza kuunda serikali ya kiraia lakini macho yote yanatazaman chaguo lake la Waziri Mkuu.
Mwandishi wa BBC Jon Leyne mjini Cairo amesema kuwepo na mazungumo na mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel Mohamed ElBaradei, ambaye atatuliza wasi wasi wa mrengo usiopendelea sheria za dini na vijana.
Mursi ameahudi kuwateuwa manaibu wake na mawaziri kutoka pande zote.

No comments:

Post a Comment