NJOMBE

NJOMBE

Sunday, June 17, 2012

Wachunguzi wa UN wasimamisha kazi Syria

Mkuu wa ujumbe wa wachunguzi wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Jenerali Robert Mood, ametangaza kuwa wanasimamisha kazi yao kwa sababu ghasia zinazidi.
Kofi Annan akimpa mkono Jenerali Mood

Meja Jenerali Robert Mood alisema wachunguzi hawatapiga doria, na watabaki kwenye vituo vyao hadi kutolewe tangazo jengine.
Hapo Ijumaa Jenerali Mood alisema pande zote mbili katika mzozo zinalenga mafanikio ya kijeshi, na hakuna hamu ya kutafuta kipindi cha mpito cha amani.
Alizisihi pande zote kutekeleza mpango wa amani uliopendekezwa na Umoja wa Mataifa, ambao alisema bado unaweza kusaidia kuleta suluhu ya amani.

No comments:

Post a Comment