NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, June 19, 2012

Maumivu Wakati wa Tendo la Ndoa


Maumivu wakati wa tendo la ndoa au kuumia wakati mnafanya tendo la ndoa kwa mwanamke hujulikana kama Dyspareunia.
Neno Dyspareunia tamka (dis-pa-roon-ia) linatokana na neno la kigiriki lenye maana ya shida katika kuingiliana wakati wa kufanya tendo la ndoa (difficulty mating au badly mated).

Utafiti unaonesha kwamba kati ya wanawake watatu, wawili wamewahi au hupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.
Imefika kwamba baadhi ya ndoa, mwanamke anapata maumivu kiasi cha kutokuwa na hamu tena ya tendo la ndoa na matokeo yake wamekuwa na wakati mgumu linapokuja suala la kufanya mapenzi na pia kila wakirudia kufanya tendo la ndoa, mambo ni yamekuwa ni yaleyale kwa mwanamke kuumia zaidi kuliko mara ya kwanza.

Kawaida huwa haifurahishi kabisa na haina hata ladha kufanya tendo la ndoa huku mmoja kati yenu akiwa anapata maumivu makali au shida hiyo husababisha kutojishughulisha katika kuleta raha ya kweli na hatimaye kuridhishana kimapenzi wakati wa tendo la ndoa.
Tendo la ndoa halikuwekwa ili kukupa shida au maumivu bali kukupa raha, furaha na kuridhishwa.
Moja ya kanuni muhimu sana katika tendo la ndoa ni
K
ama unapata maumivu usifanye
Badala yake tafuta nini kimesababisha na tafuta jibu sahihi la kuondoa hiyo hali au muone daktari akusaidie.
Na baada ya kupata tiba na kupona ndiyo unaruhusiwa kuendelea kufanya tendo la ndoa kwa kufurahia na kukupa raha zaidi, vinginevyo itakuwa ni kuleta maangamizi.

Ni kweli kwamba kama moja wapo ya mahitaji ya msingi ya kihisia (emotions) kama hili la tendo la ndoa halipatikani katika ndoa linaweza kusababisha mmoja ya wanandoa kutokuwa mwaminifu kwa mwenzake na kutoka nje kwenda kutafuta mtu wa kumridhisha zaidi, hata hivyo kwa mwanamke kufanya tendo la ndoa huku anapata maumivu au kuumia kwa kuogopa kwamba asipompa Mume wake haki yake basi anaweza kutoka nje na kutokuwa mwaminifu hilo si sahihi kwani ni kutojiamini na kutojali si afya yako tu bali haki yako ya msingi ya kufanya tyendo la ndoa kwa kupata raha.
Mnahitaji kujulishana na kuelezana ukweli ili muweze kupata dawa na hatimaye kurudi kwenye raha upya badala ya kuumizana.

Kuna mambo mengi yanayosababisha mwanamke au hata mwanaume kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa na inaweza kuwa ni wakati mwanaume anapoingia (penetrate) au wakati wa kitendo chenyewe au baada ya kitendo chenyewe.
Inaweza kuwa ni maumivu makali sana au inaweza kuwa ni kuwashwa au inaweza kuwa ni maumivu wakati wa kukojoa mkojo wa kawaida au inaweza kuwa ni maumivu ambayo unasikia
kama moto unawaka vile ndani yako wakati wa tendo la ndoa.

 Sasa pata sababu zinazosababisha Maumivu wakati wa tendo la ndoa kwa mwanamke
1. Fibroids; uvimbe katika kizazi unaowatesa wanawake Tanzania
KATIKA siku za hivi karibuni, wanawake nchini wamekuwa wakilalamika kuwa kila wanapokwenda kujifungua basi hukutwa na uvimbe katika nyumba ya uzazi.

 Uvimbe huo, ambao si saratani, umekuwa ni tishio kwa maelfu ya wanawake nchini jambo linalosababisha wengi wao kuondolewa vizazi vyao.

Daktari Bingwa  wa magonjwa ya uzazi wa kitengo cha Patholojia wa Chuo Kikuu Sayansi ya Tiba Muhimbili, Henry Mwakyoma, anaulezea ugonjwa huu na kusema kuwa  fibroids kwa kitaalamu ‘leimyoma’ ni uvimbe unaowapata asilimia 25 ya wanawake wa Kiafrika na asilimia 50 ya Wazungu.

“Nasisitiza kuwa, uvimbe huu  si saratani, unajitokeza ama katika ukuta wa kati, wa nje au ndani  kabisa ya nyumba ya uzazi,” anasema.

 Anasema; “uvimbe huu huwa katika umbile la misuli myembamba na laini  na hukua siku hadi siku,”  anabainisha Dk Mwakyoma  na kuongeza kuwa, sababu kuu ya ugonjwa huu,  bado haijajulikana.

 Anafafanua kuwa, pamoja na kuwa sababu kuu haijajulikana, lakini zipo sababu ambazo zimehakikiwa kusababisha  mwanamke kupata uvimbe wa fibroids.

“Sababu inayopewa kipaumbele zaidi ni wingi wa vichocheo vya ‘estrogen’ ambavyo vipo katika miili ya wanawake,” Anasema.

Dk Mwakyoma anafafanua kuwa, vichocheo hivi ndivyo hufanya kazi katika mwili wa mwanamke na kumsababishia kupata siku zake za hedhi.

“Ndiyo maana wengi wanaopata uvimbe huu, huwa ni wanawake walio katika balehe au ambao tayari wamevunja ungo, kwani ndiyo ambao huzalisha vichocheo vya estrogen,” anabainisha mtaalam huyo.

Lakini, pia anasema kuwa endapo inatokea mwanamke akapata matibabu ambayo yatamtaka kuongezewe vichocheo hivi, huwa katika hatari ya kupata uvimbe huu.

 Aidha, daktari huyu anabainisha kuwa, ndiyo maana wanawake walio katika kikomo cha hedhi(menopause) na  watoto hawawezi kupata uvimbe huu.

Anazitaja sifa kuu za ugonjwa huu na kusema, huwa ni nyingi kwa sababu ni uvimbe ambao asili yake ni mishipa midogo midogo na inapokuwa huweza kufikia urefu wa sentimeta tano na zaidi na uzito wa kilogram 10.

Anaongeza kuwa, uvimbe huu unaweza kutokea katika kuta zote za kizazi cha mwanamke na kusababisha mwanamke ang’olewe kizazi chake.

“Hata hivyo, wanawake wengi hupata uvimbe huu katika ukuta wa ndani kabisa wa kizazi,” anasema.
 Anataja sifa nyingine za uvimbe huu ni kuwa na tabia yake ya kubadilikabadilika sana.

 Kwa mfano, fibroids huweza kubadilika rangi na kuwa ya njano, ikabadilika na kuwa katika hali ya kimiminika, baadaye kuwa ngumu au kuwa laini yenye kutomasika.

Dalili za Fibroids
Dk Mwakyoma anazitaja sababu za ugonjwa huu na kusema kuwa, ni vigumu mwanamke kubaini au kuhisi dalili zake.

“Dalili hutegemeana na eneo ulipokaa uvimbe na ukubwa, wengi hugundulika wakati wa kujifungua, na ujauzito au endapo mwanamke atapata uvimbe katikati ya kizazi, basi huweza kutokwa damu kwa wingi,” Anasema.

 Anasema: “Hata hivyo, asilimia 35 hadi 50 ya wanawake wanaougua maradhi haya huonyesha dalili wakati wa kujifungua,”
Dalili nyingine ni mwanamke kutokwa damu zake za hedhi kwa wingi na kwa siku nyingi.
Damu za hedhi huweza kuwa nyingi au kidogo  sana zikiambatana na maumivu makali.

 “Asilimia 30 ya wanawake wanaopata maumivu na damu nyingi  wakati wa hedhi huwa na uvimbe wa aina hii” anasema
Anasema wakati mwingine mwanamke huweza kuhisi ana ujauzito kwani uvimbe huu huwa mkubwa na huchezacheza kana kwamba ni kiumbe.

 “Nina mifano hai, wapo wanawake waliowahi kuhisi wana ujauzito, wakakosa kabisa siku zao za hedhi, wakapata dalili zote za ujauzito na kumbe walikuwa na uvimbe wa fibroids,” anasema.

Anasema, mara nyingi uvimbe unaojitokeza katika ukuta wa nje wa kizazi na kuning’nia, ndiyo hucheza na kuleta dalili za ujauzito.

Mwanamke huweza kuvimba miguu kwa sababu uvimbe huu husababisha damu isitembee.
Anataja dalili nyingine kuwa ni mwanamke kupata maumivu wakati wa tendo la ndoa.

 Wakati mwingine, fibroids hukua na kuzuia mfumo wa mmeng’enyo wa chakula na kusababisha mwanamke avimbiwe.

Vile vile, uvimbe huo huweza kuzuia kibofu cha mkojo, na kumfanya mwanamke apate haja ndogo kwa taabu , au akatokwa na uchafu ukeni.

“Hatari kuu ya uvimbe huu ni ugumba, asilimia 27 hadi 40 ya wanawake wanaopata uvimbe katika kuta zote za kizazi, hushindwa kupata watoto,” anafafanua Dk Mwakyoma

 Hatari nyingine ni kwa wanawake wajawazito wenye uvimbe huu ambao wengi hufanyiwa upasuaji kwani fibroids huweza kuzuia mlango wa kizazi na mwnamke kushindwa kujifungua.

 Imebainishwa kuwa, asilimia 30 ya wanawake hutolewa vizazi mara baada ya kujifungua kutokana na uvimbe huu.

Mtaalam huyo anatahadharisha kuwa, wanawake walio katika umri wa kuzaa lakini hawazai wapo katika hatari ya kupata maradhi haya.

“Hii ni kwa sababu vichocheo vya estrogen hukua kwa wingi na kusababisha misuli ya fibroids kukua, lakini vichocheo hivyo huacha kukua wakati wa ujauzito,” anasema.

 Anataja walio katika hatari hii ni watawa ambao hawatakiwi kuzaa au wale wanaopitiliza umri wa kuzaa.
 Matibabu ya maradhi haya mara nyingi ni kufanyiwa upasuaji na kuondoa uvimbe huu au kutolewa kabisa kizazi.

“Hii inategemeana na umri wa mgonjwa, idadi ya watoto na maamuzi yake binafsi,” anasema
Katika mahojiano na Mwananchi na wanawake wenye umri tofauti waliowahi kufanyiwa upasuaji wa kuondoa uvimbe wa fibroids, wengi wanauzungumzia kuwa ugonjwa unaosumbua.

 Mmoja wapo ni Janeth Ngaiza (23) ambaye anasema, alikuwa akitokwa damu wakati yu mjamzito, ndipo daktari alipomfanyia vipimo na kugundua uvimbe huo.

“Kwa kuwa uvimbe wangu ulikuwa bado mdogo, alinishauri kufanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua, nilifanyiwa upasuaji na uvimbe ulitolewa,” anasema Janeth ambaye hiyo ilikuwa ndiyo mimba yake ya kwanza.

 Mwanamke mwingine, Juliana Kasembe anaeleza kuwa, alipata ujauzito kwa mara ya kwanza akiwa na umri wa miaka 28, baada ya kujifungua tu, ndipo alipoanza kupata maumivu makali wakati wa hedhi.

“Damu zilikuwa zikinitoka kwa wingi, maumivu makali mno, nilipofanyiwa uchunguzi daktari aligundua uvimbe huo uliokuwa na kilo tano,” anasema.

 Kwa kuwa uvimbe wa Kasembe ulikuwa mkubwa mno, daktari alishauri atolewe kabisa kizazi chake, kwa usalama wa maisha yake.

Watalaamu mbalimbali wa afya ya uzazi wanashauri wanawake kwenda kufanyiwa uchunguzi mara kwa mara ili kubaini maradhi ambayo mengine yanaweza kutibika au kuzuilika.
Huu sio mwisho kunanyingine pia zinafuata

No comments:

Post a Comment