NJOMBE

NJOMBE

Monday, February 4, 2013

KARUECHE TRAN KWENYE ROLLING OUT NA RIHANNA KWENYE ROLLINGSTONE COVERS

Baada ya Karrueche Tran kwa mara ya kwanza kutokea kwenye magazine cover Rolling Out na kuingia mtaani, Rihanna ametokea kwenye cover ya Rolling Stone Magazine akiongelea mahusiano yake na Chriss Brown. Rihanna ameliambia gazeti hilo anasema “ Niliamua ilikuwa muhimu zaidi kwangu kuwa na furaha, Nisingeacha maoni ya mtu yeyote yaje kiivyo, hata kama ni kosa , kosa ni langu, baada ya kuchafuliwa sana kwa miaka mingi, kunifanya niwe nahasira na kuniweka gizani, bora niishi maisha yangu ya ukweli na kujibu mashambulizi. Naweza sana” Alisema Rihanna Na kuendelea kusema “ Ukiongeza kipande kutoka nje, sio tatizo sana duniani. Unatuona tukitembea kuelekea sehemu Fulani, kuendesha gari kuelekea sehemu Fulani, studio, club na unadhani unajua. Lakini ni tofauti sasa hivi, hatuna yale malumbano ya aina ile tena. Tunaongea kuhusu upuuzi, Tunaheshimiana. Tunajua kabisa nini tunacho sasa, na hatutaki kupoteza. Siwezi kusema hakuna kitu tena kitaenda kinyume lakini na uhakika itamshtua, Alisema Rihanna kupitia Rolling Stone Magazine.

No comments:

Post a Comment