NJOMBE

NJOMBE

Wednesday, May 9, 2012

MAHUSIANO na UTANDAWAZI kwa VIJANA


Habari za leo tena natumai sote tu wazima ,si lengo langu kuwa beza wale walio vitandani na ma hosptalini wakijiuguza au kuugulia hapana, amani na uponyaji uwe juu yao. Nifuraha yangu kukutana tena leo katika UKURASA huu, lengo na dhumuni  langu ni kuzungumzia  mambo machache kuhusu maisha ya  vijana na mahusiano ya kimapenzi.
Kwangu mimi, ni kitu ambacho nakiamini  kwa mtazamo wangu na ningeomba sote tukichukulie kama angalizo tu kwa kile ambacho nita kiongelea hapa.
Kumekuwa na matukio mengi katika mahusiano ya vijana na hata watu wazima ,lakini ningependa kutumia nafasi hii kuzungumzia sana vijana wa rika kama langu(miaka 18-35). Katika kipindi cha karibu kumekuwa na wimbi kubwa la vijana wadogo kujikita katika dibwi la mahusiano katka umri ambao ni mdogo na hiii imepelakea dunia ya maraha kuwa na vita baridi kwa vijana, ambavyo wengi wetu tumekuwa hatumjui adui yetu hasa katika vita hii, nikinukuu kauli ya kiongozi mmoja wa zamani wa jamhuri ya china  alisema  “....hakuna wakati mzuri katika kipindi cha vita kama mwisho wa vita hiyo....““
Katika asiimia 100 ya vijana walio katika mahusiano ya kimapenzi ni kwa asilimia 25 tu ndio kwa hakika wanafuraha ya kweli katika mahusiano yao, kwa mtazamo wangu.
Zifuatavyo ni sababu ya zinatuweka vijana katika wakati mgumu kimahusiano.
1.      1. Utandawazi
2.     2.  Kutosoma nyakati
3.      3. Uelewa mdogo wa nini na nani chaguo lako
utandawazi
kutokana na ukuaji wa teknologia na sayansi, hali hii imeathiri kwa kiasi kikubwa mahusiano ya vijana katika jamii yetu kwa sasa, vijana wengi tumekuwa ni watu wa kuishi katika jamiii nyingine au tamaduni nyingine katika nyanja ya kimahusiano.,tumekuwa ni watu wa kuiga na kuishi kitamthilia zaidi, na shawishika kusema tunaishi kivenezuela na kifilipino zaidi.
Anyway ni vizuri kujua na kufahamu nini tamaduni na mila za watu wengine , lakini limeibuka tatizo la vijana wengi kutaka kuishi maisha tofauti na tamaduni zetu hilo limepelekea vijana wengi kushindwa kuelewa nini na kwa muda gani vitu hivi vifanyike na kushindwa kuvichukulia vitu kwa ukubwa wake.
Ushauri wangu ni vema vijana tuishi kati yetu wenyewe (yaani katika tamaduni na mazingira yetu)hii itapunguza kwa kiasi kikubwa maumivu na misukosuko miongoni mwetu. Watafsiri wa mambo wanasema ni vema kuishi kama wewe kwani ukishi kama mwingine, hakuna wa kutimiza majukumu yako katika nafasi yako kama wewe ..hivyo ilo litakuwa ni tatizo ambalo mtatuzi ni wewe. So be yourself no matter how is hard to be...
Nyakati
Ni kweli mambo yanakwenda yakibadilika na mabadilio kwa binadamu ni kitu ambacho ni vigumu kikizuia, lakini pia sio kila kitu kina badalika au kinaendana na mabadilko hayo, vingine vilikuwepo vipo na vitaendelea kuwepo tu bila kujali kigezo cha muda au Nyakati. Ni vema tukaliangalia upya swala ili la mabadilko na mahausiano. Kama nilivyosema mwanzo sasa kumekuwa na lundo la vijana wadogo kujiingiza katika mausiano katika umri mdogo, pasipo kuwa na utayari na ukomavu wa akili na kiuchambuzi pia.
Ushauri wangu  ni vema jamii kwa ujumla kukaa na kulizungumzia jambo hili kwa upana na ukubwa wake pasipo kujali rika ili kuweza kukinusuru kizazi hiki cha sasa.  Its better to be open for the best direction
Uelewa mdogo
Hili nitatizo pia kwa upande wake , si tu kujua nini mwenzi wako anapenda na nini hapendi lakini nadhani ni zaidi ya kujamiana,(ngono) mapenzi ni uwanja mpana sana ambao wausika wanahitaji kuwa na uelewa mpana wa kutambua mipaka ya upana huo ili kuweza kuwa na ufanisi mkubwa katika kulitumia jukwaa hilola wapendana nao…
Kwa leo naomba niishie hapa…..
Lakini kuna mengi ya kuyazungumzia na kuchangia pia,nijukumu letu sote kusaidiana na kushauriana pale inapowezekana pia….. kwani kujua bila kufanya siyo kujua(to know without doing is not knowing)

Saturday, May 5, 2012

JK afanya ajizi baraza la Mawaziri wapo walio ula na wapo waliopigwa chini

JK AWATUPA MKULO,NGELEJA,MAIGE,NUNDU NA DK MPONDA,ATEUA WATATU WAPYA,PROFESA MAGHEMBE,MKUCHIKA WAPONA MAKAMBA SIMBACHAWENE SASA MANAIBU.
                                   Rais Jakaya Kikwete akitangaza Baraza jipya la Mawaziri, Ikulu jana.
RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko makubwa katika Baraza la Mawaziri kwa kuteua wapya watatu na manaibu 10 huku akiwaacha wanane.

Katika mabadiliko hayo, Rais Kikwete amewapandisha manaibu mawaziri wanne kuwa mawaziri kamili na kuwahamisha wizara mawaziri wanane na manaibu waziri sita, huku mawaziri na manaibu waziri 22 wakibaki katika wizara zao za awali.

Kutokana na mabadiliko hayo, idadi ya mawaziri na manaibu wao sasa imeongezeka kutoka 50 katika baraza la awali hadi 55. Mawaziri kamili wameongezeka kutoka 29 hadi 30 huku manaibu waziri wakiongezeka kutoka 21 hadi 25.

Mawaziri ambao wameng’olewa na wizara walizokuwa wakiziongoza kwenye mabano ni Mustafa Mkulo (Fedha), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii) William Ngeleja (Nishati na Madini), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), Omar Nundu (Uchukuzi) na Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii).

Panga hilo la mabadiliko limewakumba pia Manaibu Waziri wawili, Dk Lucy Nkya (Afya na Ustawi wa Jamii) na Dk Athumani Mfutakamba (Uchukuzi).

Akitangaza baraza hilo Ikulu jana, Rais Kikwete alisema mabadiliko hayo yametokana na mjadala mkali ulioanzia bungeni baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na kwamba ametumia fursa hiyo kufanya marekebisho kadhaa ili kuimarisha utendaji wa Serikali.

“Baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ile kulikuwa na mjadala mkali bungeni, lakini pia kwenye kikao cha wabunge wa chama na Waziri Mkuu (Mizengo Pinda), alinipa taarifa hiyo na wanasema mawaziri wote waliotajwa waondolewe,” alisema Kikwete na kuongeza:

“Tumekaa kwa pamoja na kumwangalia kila mmoja na tuhuma zake, kwa Kiingereza tunasema ‘case by case’ na tukaona kwamba wawili kati yao tuwahamishie katika wizara nyingine lakini tukatumia fursa hiyo kufanya mabadiliko mengine kwa lengo la kuimarisha utendaji wa Serikali.”

Mawaziri wengine ambao walikuwa wakikabiliwa na shinikizo la kuondolewa madarakani ni aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), George Mkuchika na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe.

Mkuchika sasa amehamishiwa Ofisi ya Rais – Utawala Bora wakati Maghembe amehamishiwa Wizara ya Maji akichukua nafasi ya Profesa Mark Mwandosya ambaye ameteuliwa kuwa Waziri katika Ofisi ya Rais, asiyekuwa na Wizara Maalumu.

Rais Kikwete alisema ameteua manaibu waziri wawili katika Wizara ya Nishati na Madini; mmoja atakayeshughulikia masuala ya nishati na mwingine madini.

“Kulikuwa na mjadala mkali kuhusu kutenganishwa kwa wizara hii ya nishati na madini, lakini tumeangalia kwamba kuunda wizara mpya katikati hivi halafu kuna masuala ya kibajeti, tukaona itatusumbua, hivyo tumeamua kuwe na manaibu waziri wawili halafu hayo mapendekezo mengine tukasema tuangalie mbele ya safari,” alisema.

Alisema uamuzi huo umezingatia ukubwa wa wizara hiyo na changamoto zake akisema nishati ni sekta inayokua hasa kutokana na kugundulika kwa kiasi kikubwa cha gesi pia kuwapo kwa dalili za kupatikana kwa mafuta.

Alisema kwa upande wa madini, pia sekta hiyo imekuwa ikikuwa kwa kiasi kikubwa na kwamba kwa miaka mitano mfululizo imekuwa ikishika nafasi ya pili katika kuliingizia taifa mapato, baada ya utalii.

Mbali na kuongezwa kwa naibu waziri katika wizara hiyo, Rais Kikwete pia ameteua manaibu waziri katika wizara ambazo awali hazikuwa na nafasi hizo.

Wizara hizo ni pamoja na Ofisi ya Makamu wa Rais, Katiba na Sheria na Maliasili na Utalii.

Mawaziri wapya
Mawaziri wapya walioteuliwa na Wizara zao kwenye mabano ni Mbunge wa Handeni,  Dk Abdallah Kigoda (Viwanda na Biashara), Mbunge wa Kalenga, Dk William Mgimwa (Fedha) na Mbunge wa Kuteuliwa Profesa  Sospeter Muhongo (Nishati na Madini).

Walioteuliwa kuwa Manaibu Waziri ni Mbunge wa Rufiji Dk Seif Suleiman Rashid (Afya na Ustawi wa Jamii), Mbunge wa Kibakwe, George Simbachawene (Nishati na Madini), Mbunge wa Bumbuli, January Makamba (Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia), Mbunge wa Buchosa, Dk Charles Tizeba (Uchukuzi) na Mbunge wa Mvomero, Amos Makala (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo).

Wengine ni Mbunge wa Makete, Dk Binilith Mahenge (Maji), Mbunge wa Shinyanga Mjini, Stephen Maselle (Nishati na Madini – Madini), Mbunge wa Viti Maalumu, Angela Kairuki (Katiba na Sheria) na Wabunge wa Kuteuliwa Janet Mbene na Saada Mkuya Salum  wote Fedha.

Naibu Mawaziri waliopandishwa na kuwa mawaziri kamili wamo, Christopher Chiza (Kilimo, Chakula na Ushirika), Dk Harrison Mwakyembe (Uchukuzi), Dk Fenella Mukangala (Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo) na Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii).

Kabla ya kuwa mawaziri kamili, Chiza na Dk Mukangara walikuwa Naibu mawaziri katika wizara walizopangiwa wakati Dk Mwakyembe alikuwa Naibu Waziri wa Ujenzi na Kaghasheki alikuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Mawaziri wengine waliohamishwa kutoka wizara zao za awali ni, Celina Kombani kutoka Katiba na Sheria kwenda Ofisi ya Rais (Manejimenti ya Utumishi wa Umma) ambako amechukua nafasi ya  Hawa Ghasia ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi).

Shamsi Vuai Nahodha amehamishiwa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, ambako amechukua nafasi ya Dk Hussein Mwinyi ambaye amehamishiwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

Dk Emmanuel Nchimbi amehamishiwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, kuchukua nafasi ya Nahodha akitokea Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo wakati Waziri wa Katiba na Sheria ni Mathias Chikawe ambaye alikuwa Ofisi ya Rais Utawala Bora.
Manaibu waziri waliohamishwa ni Charles Kitwanga ambaye amepelekwa Ofisi ya Makamu wa Rais akitokea Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Adam Malima ambaye amehamishiwa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika akitokea Nishati na Madini na Pereira Ame Silima ambaye alikuwa Naibu Waziri wa Fedha sasa anakuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Gregory Teu ambaye pia alikuwa Wizara ya Fedha amehamishiwa Wizara ya Viwanda na Biashara ambako anachukua nafasi ya Lazaro Nyalandu ambaye amehamishiwa Wizara ya Maliasili na Utalii, wakati aliyekuwa Naibu Waziri wa Maji, Gerson Lwenge, amehamishiwa Wizara ya Ujenzi, kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk Mwakyembe.

Waliobaki kwenye nafasi zao
Mawaziri waliobaki kwenye nafasi zao ni pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk Terezya Huvisa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri  Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Dk Mary Nagu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.

Wengine ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk David Mathayo.

Pia wamo Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka; Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.

Kwa upande wa Manaibu Waziri wamo Kassim Majaliwa (Ofisi  ya Waziri Mkuu, Tamisemi - Elimu), Aggrey Mwanry (Ofisi  ya Waziri Mkuu, Tamisemi), Dk Makongoro (Kazi na Ajira) na Benedict Ole-Nangoro (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi).

Wengine ni Mahadhi Juma Maalim ( Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa),  Goodluck J. Ole-Medeye (Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi), Ummy Mwalimu (Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto), Philipo Mulugo (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Dk Abdulla Juma Abdulla (Ushirikiano wa Afrika Mashariki).

Uwajibikaji
Kuhusu uwajibikaji Rais Kikwete alisema baada mawaziri kuwajibika kisiasa, wanaofuta ni watendaji katika wizara na taasisi nyingine za umma ambao ndiyo chanzo cha mawaziri hao kuwajibika.

Alisema mawaziri wamekuwa wakijiuzulu hata kwa makosa ambayo si yao na kwamba hivi sasa Serikali itaanza kuchukua hatua kwa watendaji wakiwamo makatibu wakuu, wakurugenzi wa wizara, watendaji wakuu wa mashirika na taasisi za umma pamoja na bodi za mashirika husika.

“Pamoja na kuwa na utaratibu huu mzuri wa kuwajibika kwa wanasiasa, sasa lazima tuwawajibishe hata hao wanaosababisha mawaziri hawa kujiuzulu, maana wakati mwingine wanawajibika kwa makosa ambayo si yao,” alisema Kikwete na kuongeza:

“Kuna watu ambao kazi yao ni kupiga fitina tu … wao wana kazi ya kusema kaja hapa ataondoka kwani yeye ni nani bwana …… sasa watu wa aina hii hatuwezi kuendelea kuwavumilia hata kidogo, lazima hatua zichukuliwe kwa watendaji wakuu awe ni katibu mkuu wa wizara, ofisa mtendaji mkuu wa shrika la umma, mkurugenzi wizarani au hata bodi ambazo zinasimamia taasisi hizi.”

Mawaziri wapya na waliohamishwa wataapishwa keshokutwa Jumatatu kuanzia saa 5:00 asubuhi katika Viwanja vya Ikulu.


Madaktari wafurahia Dk Mponda, Nkya kuondolewa


Aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda
CHAMA cha Madaktari  Tanzania (Mat) kimeeleza kufurahishwa na hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuwaondoa aliyekuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Hadji Mponda na Naibu wake, Dk Lucy Nkya, kuwa ametekeleza madai yao.

Pia, chama hicho kimesema kimefurahishwa na uteuzi wa Dk Hussein Mwinyi kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwa sababu, ni mtendaji anayeaminika.

Katibu Mkuu wa Mat, Dk Rodrick Kabangila, alisema madaktari wamefurahi kuondolewa kwa mawaziri waliokuwapo kwa sababu walikuwa kikwazo kwenye utekelezaji wa madai yao.

“Kwa sasa tuna imani na Serikali, madai yetu na hata yale tunayojadili baina yetu na Serikali yatatekelezwa, tunasema hivyo kwa sababu kama wangeendelea kubaki mawaziri wa awali utekelezaji wake ungekuwa na mashaka,” alisema Dk Kabangila.

Kabangila alisema mawaziri hao walikuwa wagumu wa kutekeleza madai yao na wakati mwingine, walioonekana kuwadharau hali iliyosababisha waingie kwenye mgomo.

“Dk Mwinyi tunamfahamu, wakati madaktari tulipogoma mwaka 2004/05 alikuwa Naibu waziri alikuja kutusikiliza, yapo mambo alichukua hatua kwa wakati,” alisema Dk Kabangila na kuongeza:

“Akiwa Naibu waziri wakati huo alionyesha tofauti kubwa na Naibu waziri aliyeondolewa Dk Nkya, kwani amekuwa na kiburi hata madaktari walipogoma aliendelea na msimamo wake.”

Kuhusu uteuzi wa mawaziri wapya kwa jumla, Dk Kibangila alisema unaleta matumaini kwa sababu una sura nyingi mpya na zenye majina yanayoonyesha uadilifu.Chanzo ni Mwananchi
  

Thursday, May 3, 2012

Unajua kipaji chako?

Utambuzi wa vipaji hula fikra.
Vijana wengi tumeshapitia au tunapitia kwenye kipindi kigumu sana maishani. Nina uhakika wengi wetu tumeshawahi kukosa usingizi wakati tupo kitandani na kubaki tu kuangalia dari na kujiuliza maswali mengi sana; nitafanya nini maishani? Mustakabali wa maisha yangu ni upi? Nitakuwa wapi baada ya miaka miwili, mitano au hata kumi?
Bahati mbaya Watanzania hatuna hulka ya kujadili mambo kama haya kwa uwazi tukiwa na ndugu, jamaa na marafiki zetu. Na matokeo yake (tunaonekana kama) hatujifunzi kutoka kwa wenzetu — hili suala ndilo linalonipa misongo kwenye mijadala mbalimbali. Kwahiyo, ni matumaini yangu kuwa nasaha zilizopo kwenye makala hii zitabadilisha fikra za angalau kijana mmoja na kutambua kuwa maisha yake ya baadae yako kwenye viganja vyake! Kwa maneno mengine, wewe msomaji ndio mwenye uwezo mkubwa wa kuamua maisha yako huko mbeleni yaweje.
Je, unajua una kipawa, kipaji au talanta ipi? Baada ya kumaliza elimu ya sekondari au chuo kikuu, ulikuwa au unajua unataka ufanye nini; uwe mtu wa aina gani kwenye jamii?
Kama unashindwa kujibu hayo maswali haraka na kwa ufasaha, usiogope na wala usitetereke. Hauko mwenyewe, kijana. Wengi tumeshapitia na tunaendelea kupitia kwenye kipindi ambacho fikra zetu zinakuwa zimejawa na mawazo ya utata. Lakini utakubaliana nami kuwa wenzetu ambao tayari wanajua wana vipaji fulani na kuvifanyia kazi, maisha yao huonekana marahisi machoni mwa wengi.
Amini usiamini, majibu ya maswali mengi hupatikana hapa — kwenye tovuti ya Bongo Celebrity. Jeff na timu yake wamekuwa wanajitahidi kutuletea mahojiano murua ya watu maarufu wanaofanya vizuri Bongo kwenye nyanja mbalimbali, ili mimi na wewe tujifunze mawili matatu kutoka kwao na kutumia ‘maujanja’ kwenye maisha yetu; kukuza vipaji vyetu na kuviendeleza.
Jifunze kutoka kwa waliofanikiwa
Kwa mfano, Profesa Jay akihojiwa huwa anatoa nasaha nyingi sana ambazo binafsi naamini zinatakiwa kuhamasisha kila kijana anayezisikia kwa namna moja au nyingine. Cha kusikitisha wengi wetu tutakumbuka tu ni lini Mzee wa Mitulinga atatoa album mpya. Basi.
Mmoja wa waliofanikiwa.
Sielewi kwanini tunafumbia macho ukweli kuwa Jay huwa anatembea na karatasi na kalamu karibia muda wote, na akiona kitu ambacho anadhani kitakaa vizuri kwenye mashairi yake huwa anakiandika papo kwa papo. Muda mwingine hata akiwa na marafiki zake. Kama bado hujanielewa, Jay ni mwandishi mzuri sana na huwa anaandika mashairi muda wote! Na suala la kipaji chake kukua, kupevuka na kukomaa linajidhihirisha kila kukicha. Kasikikilize wimbo unaoitwa Chuzi limekubali wa Hard Blasters Crew, halafu linganisha na mashairi yaliyojaa busara kwenye wimbo Machozi, Jasho na Damu aliouimba takribani miaka miwili baadae.
Ninachojaribu kukuasa kijana mwenzangu ni kama ifuatavyo: Fungua macho ukiwa kwenye pita-pita na mihangaiko yako; ukiona kichuguu kizuri angalia kwa makini na jifunze jinsi kinavyojengwa na siafu, badala ya kukisifia tu na kuendelea na safari.
Tambua una vipaji

Safari ya kutambua una kipaji au vipaji gani, kuvikuza na kuvifanyia kazi inaweza ikawa ngumu au rahisi kutegemeana na mazingira na mazingara uliyokulia na uliyomo. Huo ni mjadala mrefu sana ila sitaki kuzama huko, kwasababu naamini vitu ambavyo vinampa mtu motisha vina nguvu zaidi.
Kama nilivyosema hapo awali, usikubali mtu mwingine akuamulie maisha yako ya baadae yaweje kwasababu tu amekuzidi umri au ana mamlaka fulani. Aghalabu kauli zenye mamlaka zinaweza kukufunga mawazo yako na kukusukuma kufanya jambo ambalo labda sio ile kitu roho inapenda. Pia, usifuate mkumbo; jaribu kufikiria mustakabali wako binafsi kwanza.
Kwa mantiki hiyo, ni jukumu lako kugundua una vipawa gani. Sidhani kama kuna njia rahisi ya kukwambia, “Aisee, bwa’ mdogo una kipaji (fulani)! Kifanyie kazi.” Njia pekee itakayokuwezesha kufaulu huo mtihani ni kujaribu kufanya na kufuatilia mambo mbalimbali — iwe kwa kusoma vitabu vya taaluma au magazeti, kuongea na kubadilisha mawazo na watu n.k. Huwezi kung’amua kuwa wewe ni mchezaji mzuri wa mpira kwa kukaa kijiweni, wakati u mvivu wa hata kupiga danadana tu.
Wewe imba, mimi nitadonoa nyuzi za gitaa.
Jiulize, ingekuwa vipi kama Man Dojo na Domo Kaya wangekaa tu vijiweni Arusha na kutothubutu kujaribu kupiga gitaa na kuimba?
Usiogope kukosolewa
Changamoto kubwa mwanzoni ni kuondokana na hofu ya kufanya makosa au kuogopa kukosolewa. Ni kawaida kila  binadamu kuogopa, ila kinachotufautisha ni jinsi tunavyokivuka hiki kihunzi. Unadhani sikujawa na hofu hata chembe nilipopewa fursa ya kuandika hii makala na kuanika mawazo yangu hadharani? Kilichonipoza ni ile motisha ya kutumia kasoro zozote zitakazojitokeza na kuhakikisha naandika makala nzuri zaidi nitakapopewa fursa nyingine.
Lengo langu kubwa ni kuanzisha mjadala mzuri, kwasababu ninaamini kuna Watanzania wengine wengi wenye uzoefu na mawazo mazuri zaidi yangu, na nina kiu na njaa ya kujifunza kutoka kwao!
Ukiacha kipaji, huyu ana 'kismati' cha kupendwa kutokana na tabia yake.
Hadithi nzuri kuhusu kujua jinsi ya kutumia vema ukosolewaji inatoka kwa Sir Juma Nature. Sir Nature alitoka kwa njia ya kushirikishwa kwenye nyimbo kama Mtani Jirani, Mtulize na Maskini Jeuri. Mimi ni mmojawapo wa mashabiki wake wakubwa na nilivutiwa sana na kisa alichokiimba kwenye wimbo Mtani Jirani. Ila Juma wa kipindi kile ni tofauti na yule Juma aliyetikisa na Hili Gemu, Kighetto-ghetto (remix), Jinsi Kijana na nyimbo nyingine lukuki.
Juma alikuwa anatumia lugha ‘ngumu’ iliyokuwa inaeleweka kwa vijana wa Kurasini, Keko, Temeke, Tandika, Mtoni na Mbagala. Nakumbuka P-Funk, Bonny Luv, Sebastian Maganga na wengine wengi walimkosoa na kumshauri ‘alainishe’ mashairi yake. Kijana hakuzira wala kunywea, akaufanyia kazi ushauri.
Jiamini na amini unachofanya
Rock City sasa inaitwa Rap City.
Labda hii ndio nguzo kubwa kuliko zote. Sijui kama inajengwa kwa mambo niliyoyajadili kwa kifupi hapo juu, au ndio msingi unaohimili niliyoyataja. Kama wewe hujiamini na wala huamini kuwa unachofanya ni kizuri na kina manufaa kwa jamii, unategemea wanaokuzunguka wakuamini?
Hakika kauli za kutia moyo kutoka kwa wazazi, ndugu, marafiki na watu ulio nao karibu zinaweza kukusaidia. Ila huwa napenda kusisitiza zaidi ile motisha mtu binafsi aliyonayo.
Huyu Fid Q kipenzi cha wengi, safari yake haikuanzia na wimbo Mwanza au FidQ.com. Kijana ilibidi atoke Mwanza kwa hela ndogo aliyokuwa nayo hadi Dar ili aje kufanya alichoamini ni kipaji chake. Unaweza ukadhani  alikuwa anacheza karata tatu au kamari, kwasababu lolote lile lingeweza kutokea kwenye safari yake na labda tusingepata kumsikia hata mara moja.
Bahati mbaya (kwa wapinzani wake) na nzuri (kwa mashabiki wake), alipewa nafasi ya kughani kwenye wimbo mmoja unaoitwa Ukweli na Uwazi uliopo kwenye album ya Wachuja Nafaka. Fid Q akatoka rasmi. Ukisikiliza nyimbo zake mbili za kwanza, utaafiki kuwa alikuwa anajiamini na anaamini alichokuwa anafanya.
Sio kazi na dawa, bali ni kazi na kazi
Ingawa sipendi kurusha mawe ya lawama, nitajiona mwenye hatia kama nisiposema haya yafuatayo kwa wale ma-DJ na waandishi wa habari wanaopata fursa ya kuwahoji watu waliofanikiwa kwenye fani mbalimbali.
Waandishi hamna budi kuuliza maswali yatakayozaa majibu yenye manufaa.
Wachache wenu mmesahau kuwa kazi mliyokuwa nayo ni dhamana. Mna zana zote za kubadilisha fikra za watu wanaosikiliza vipindi vyenu. Mimi siridhiki mnapotaja tu wimbo au kitabu fulani cha mhusika kitatoka lini na mambo mengine kama hayo kwa dakika thelathini!
Mnasahau kuwa kazi mnazoletewa ni matunda yanayotokana na juhudi, jasho na uwajibikaji wa wahusika. Kwanini mnashindwa kusisitiza kazi nzuri hutokana na watu kujituma? Vipi, mbona mnashindwa kutuambia zile shows nzuri za Waunaume Halisi au TMK zinatokana na vijana kufanya mazoezi kila siku?
Ukiongea na watu waliofanikiwa utagundua kuwa, ukiacha vipaji walivyonavyo, ni wavumilivu na wanajituma. Kwahiyo, kijana mwenzangu, ukishagundua kipaji chako, huna budi kukilea, kukitunza na kukilinda kama mboni za macho yako. Na muhimu zaidi ni kukifanyia kazi kila siku; hakika hiyo ndio njia pekee itakayokuletea matunda.
Ukiangalia kulia, kushoto, mbele na nyuma utaona ‘vita baridi’ kati ya kizazi cha vijana wa sasa na wa zamani. Bahati mbaya vijana wa sasa (wanaonekana) wamepoteza matumaini na wamebakia kulaumu, ilihali wanaweza kuamka, kugundua vipaji vipaji vyao, kujenga moyo wa kujiamini na kufanya kazi ili kuleta mabadiliko.
Kila mkoa unatakiwa kuwa na vijana kama hawa!
Kila mkoa unatakiwa kuwa na vijana kama hawa!
Nchi inahitaji kina Modesta, Zitto na January kwenye kila mkoa; viongozi wapya wanahitajika. Magazeti yanahitaji waandishi wanaoweza kuakisi mawazo yetu. Jenerali Ulimwengu akistahafu, hatuna budi kuliziba pengo lake kwa kuwa tutaendelea kuhitaji makala zitakazotufanya tufikirie. Wahandisi na wanasheria wanahitajika na wataendelea kuhitajika.
Kijana, huu ni waraka kwako: Tambua na tumia kipaji chako ipasavyo — usijidharau.

Vijana Nguvu ya Mabadiliko

Wimbi kubwa la vijana kuamua kujihusisha na “siasa” limekuwa gumzo kwenye miaka ya hivi karibuni. Lakini gumzo na maswali yanazidi hususan katika zama hizi za siasa za vyama vingi.
Ikumbukwe katika siasa za chama kimoja, TANU na baadaye CCM ilihakikisha kila rika linashiriki kikamilifu. Hata watoto wadogo na hapo ndipo tunaona uwepo wa “chipukizi”.
Lakini pindi mabadiliko na kuimarika kwa siasa za vyama vingi, wingi wa vijana (hasa vijana makini) kukimbilia na kujiunga na vyama vya upinzani na kuendesha mabadiliko kama nchi ilivyopitia katika uchaguzi wa mwaka jana, 2010, unachochea uchambuzi wa kina.
Uungwaji mkono wa siasa unaweza kuchambuliwa kuwa unaambatana na mambo makuu mawili; mosi ni msukumo binafsi wa kijana wa Kitanzania wa uhitaji wa mabadiliko.
Pili ni mhemko wa majira (seasonal emotions/exctitement). Mhemko huu ni kama kilevi ama pombe na vijana ndio wanjwaji ama walevi wakuu wa pombe hii kali, nitachambua kwa kina katika makala ijayo.
Wimbi hili kwa ujumla wake linatokana na “maisha magumu” yatokanayo madhara hasi ya utawala, uongozi, dira ya chama tawala CCM uliodumu kwa zaidi ya miaka 50.
Katika makala haya tatawamulika vijana kupitia mtazamo wa falsafa ya vijana nguvu ya mabadiliko na kuchambua kwa kina juu ya msukumo binafsi wa kijana wa Kitanzania juu ya uhitaji wake wa mabadiliko na nafasi yake katika kuleta na kuendeleza hayo mabadiliko kwa kuzingatia misingi ile ile ya falsafa ya vijana nguvu ya mabadiliko.
Hapa ieleweke kwamba katika makala haya kuwa falsafa ya vijana nguvu ya mabadiliko sio mali ya chama kimoja cha siasa hapa nchini. Pia falsafa hii katika makala haya haihusiani na ushawishi wa aina fulani ya itikadi ya kisiasa, dini, rangi ama kabila. Misingi ya falsafa hii unatokana na uhalisia wa dhana kuwa vijana katika karne hii ya 21 ni nguvu ya mabadiliko kutokana na hoja kadha wa kadha.
Lakini pia daima sifa kuu ya “ujana” kama rika ni kuwa na mapenzi katika mabadiliko. Kufanya mambo au kuwa na vitu tofauti na mazoea. Huo ndio ujana daima!
Ulimwengu unakadiriwa kuwa na idadi ya watu zaidi ya bilioni 6, kati ya hao asilimia 80 ikiwa ni vijana. Kwa kigezo cha wingi pekee hatuwezi kupuuza kuwa vijana hawawezi kuwa nguvu ya mabadiliko. Mathalani Afrika Mashariki tu ina jumla ya watu wapatao 126 milioni, kati ya hao asilimia 70 ni vijana.
Tanzania inakadiriwa kuwa na watu wapatao milioni 46, kati ya hao zaidi ya 35 asilimia ni vijana. Takwimu hizi ni kutokana na sensa ya mwaka 2002, panapo majaliwa baada ya sensa ya mwaka 2012 kufanyika huenda idadi hiyo ya vijana ikaongezeka na kuwa kubwa zaidi ya tunavyotazamia.
Hoja ya pili, pamoja na ongezeko la idadi ya watu hapa nchini na kusemekana kuwa vijana ni zaidi ya asilimia 50 ya watu wote hapa nchini, pia wanatambulika kuwa asilimia 65 ya nguvu kazi ya Taifa ni vijana. Nguvu kazi hii haiondoi ukweli kuwa wengi wao vijana hufariki kabla ya kutimiza miaka 30/40. Kama vijana wote wangepata ajira au wasipate ajira, wafanye kazi ama wasifanye kazi, muda wao wa uhai kazini unakadiriwa kuwa jumla ya miaka 8 tu.
Hoja ya tatu ni tafasiri ya neno ‘kijana’. Mwanazuoni nguli Prof. Issa Shivji aliwahi kusema katika moja ya mijadala ya vijana kuwa yeye ni kijana kutokana na kuwa upeo wake wa kufikiri bado una nguvu na hutenda kazi zaidi ya ambavyo vijana kwa mujibu wa umri wao wangeweza kufanya.
Kwa muktadha huo tafsiri ya ujana inaweza pia kuwa kwa mujibu wa fikra na sio umri pekee.
Bado wapo vijana japo ni wachache ambao hutumia fikra zao vyema na kufanya vizuri zaidi ya vijana wenzao kwa mujibu wa umri na pia zaidi wa watu wazima kuwapita umri.
Sera ya maendeleo ya Taifa ya vijana imetoa dira ya kitaifa katika kutafsiri neno kijana kwa kusema kuwa vijana ni wale wenye umri kati ya miaka 18 na 35. Pamoja na kuwa ulimwengu haukubaliani juu ya nani hasa awe kijana kwa mujibu wa umri, Umoja wa Mataifa wao husema kijana ni yule aliye kati ya umri wa miaka 18 na 24. Wakati programu ya Jumuiya ya madola ambayo Tanzania ni mwanachama inasema ni kati ya miaka 16 na 29. Nchi nyingine kama Malaysia inasema vijana ni kati ya miaka 15 na 40. Umoja wa Afrika kupitia makubaliano ya vijana “Youth Charter” wao husema vijana ni kati ya miaka 15 na 35. Hakika huu ni mkanganyo.
Ujana kwa mujibu wa umri sio kitu cha kukitazamia na kukitegemea sana kwa kuwa umri huwa unaongezeka na hatimaye mtu hustaafu ujana kwa mujibu wa umri. Katika Taifa changa kama Tanzania kuendelea kuutafsiri ujana kwa mujibu wa umri hakutaleta tumaini jipya la mabadiliko ya kweli. Hatupaswi kuutafsiri ujana kwa mujibu wa umri kwa kuwa wenye umri wa ujana unaweza usiwe na manufaa sana kwa Taifa kutokana na kufungiwa ndani ya umri. Mfano rahisi ni serikali iliyopo madarakani na Taifa kwa ujumla kushindwa kutumia kile inachokiita asilimia 65 ya nguvu kazi ya Taifa — vijana — katika uzalishaji ili kuongeza ajira, kukuza teknolojia na kufanya mapinduzi ya kimaendeleo.
Vijana, ujana sio umri, ujana ama kijana ni upeo wa fikra pevu. Hii ndio tafsiri ya neno kijana ambayo taifa inapaswa kuichukua na kuifanyia kazi. Upeo wa fikra pevu ndio unaotofautisha maendeleo katika nchi zilizoendelea na nchi za dunia ya tatu, mahali ambapo Tanzania ipo.
Upeo wa fikra pevu ndio utakao wafanya vijana kuwa “nguvu ya mabadiliko”. Bongo za vijana ndio chachu ya mabadiliko, na ndio chemchem ya fikra mpya na mbadala zinazotarajiwa kulitoa Taifa katika usingizi mzito wa kifikra kwa kuwa umri wao wa ujana kwa mujibu wa sera yao, ukipita hautabadilisha chochote endapo hawatatumia vema uwezo wao wa kufikiri na kutenda mambo katika shughuli zao za kila siku.
Tukiisha kufahamu kuwa ujana wetu hautokani na umri wetu bali ujana wetu unatokana na nini tunafikiria na nini tunatenda sawasawa, itatusaidia kudhihirisha kuwa kweli vijana ni nguvu ya mabadiliko.
Ufahamu wetu wa ujana sharti utokane na upeo wa fikra zetu pevu. Fikra zetu zinaweza kuwa na nguvu zaidi ya umri wetu zaidi ya ukomo wa miaka 35. Ili tuone umri wetu hautusaidii ni vema kujiuliza swali moja, je, kwa nini nchi kama Malaysia wao husema ujana unaisha pale mtu anapotimiza miaka 40? Na je, kwa nini ulimwengu haukuwahi kuwa na tafsiri moja ya neno ujana? Matokeo yake sasa nchi zilizoendelea kama Ujerumani, Uingereza na nyinginezo zimeendelea, sio kwa kigezo cha umri wa watu wao, bali kwa mapinduzi ya kifikra tangu kuwekwa kwa misingi ya mataifa yao.
Tafsiri hii mpya ya ujana itatusaidia kuweka dira sahihi ya kujitambua na kuichambua dhana ya “vijana nguvu ya mabadiliko”. Itatusaidia kuondokana na mhemko wa majira ambao nitauelezea vema huko mbele. Itatusaidia kujua tuwe na msukumo binafsi ama wa pamoja katika kudai na kuleta mabadiliko. Mwisho itatusaidia kuweka mustakabari mpya wa Taifa letu Tanzania kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.
Frederick Fussi ni Katibu Mtendaji katika shirika lisilo la kiserikali la TYVA. Barua pepe: frdmbimbi (at) yahoo (dot) ca. Blog: www.frederick-fussi.blogspot.com.

Thursday, April 12, 2012

Safari ya Simba Es Setif,Licha ya mambo yote Simba hawakukata tamaa


Kwikwi husababishwa na nini?

Baada ya kusoma makala inayohusu kijana mmoja aliyesumbuliwa na kwikwi kwa zaidi ya miaka miwili na nusu, na baadaye kutibiwa tatizo hilo kwa kufanyiwa upasuaji wa ubongo na kutolewa tezi, nimeamua leo nizungumzie kwikwi.
Kwiki ni kitendo kisichozuilika ambacho hutokana na kusinyaa kwa kuta za kiwambo cha moyo au diaphragm. Kwa kawaida kwikwi ni kitendo kinachojirudia rudia mara nyingi. Sauti ya 'hic' inayotokea wakati unapokuwa na kwikwi husababishwa na kidaka tonge (epiglottis) ambacho hufunga haraka wakati hewa inapoingia kwenye koo. Kupiga kwikwi kwa kawaida hakuna maumivu lakini mara nyingine husumbua hasa inapoendelea kwa muda mrefu. Kwikwi ya kawaida huweza kutulizwa kwa kunywa maji, lakini wakati mwingine kufanya hivyo hakusaidii.
Zifutazo ni sababu zinazoweza kukuletea kwikwi
1. Kula kwa haraka.
2. Kula chakula cha moto na kunywa maji baridi baada yake.
3. Kulia au kukasirika.
4. Kula chakula chenye viungo vingi au pilipili.
5. Kula chakula cha moto sana.
6. Kunywa pombe au soda kwa wingi.
7. Kukohoa sana.
8. Kucheka kupita kiasi.
9. Kufurahi sana, kusisimka au kupatwa na msituko.
Kwa ujumla tunaweza kusema kuwa, vitu ambavyo vinakiletea karaha kiwambo cha moyo au diaphragm husababisha kwikwi. Kuna sababu nyingi ambazo husababisha jambo hilo na hizo tulizotaja hapo juu ni miongoni mwazo,ambapo matokeo yake ni humfanya mtu apige kwikwi. Kwikwi kwa kawaida huisha baada ya dakika chache au hata sekunde. Lakini iwapo kwikwi itaendelea kwa masaa au kwa siku, huweza kuwa ni tatizo muhimu la kitiba na pengine hali kama hiyo inaweza ikawa inasababiswa na ugonjwa.
Kuna baadhi ya watu hupata kwikwi sana wakati wa ujauzito, baada ya kufanyiwa operesheni na hata watoto wachanga pia hupatwa na kwikwi mara kwa mara. Wajawazito hupata kwikwi sana mwishoni mwa miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito na mwanzoni mwa miezi mitatu ya pili. Kwikwi hutokea wakati wa ujauzito ni kwa sababu wakati huo uwezo wa kuvuta hewa ndani ya mapafu na kutoa nje huongezeka kwa asilimia 30 hadi 40 ikilinganishwa na hali ya kawaida. Hakuna sababu inayojulikana inayosababisha kwikwi kwa watoto wachanga, na wazazi wanashauriwa wasitiwe hofu na suala hilo. Hii ni katika hali ambayo kwikwi baada ya upasuaji husababishwa na nusu kaputi au anesthesia.

Wednesday, April 11, 2012

Jamani Jamani, "Mafuriko Tena Dar"

Baada ya mvua kunyesha kwa wingu tena siku ya leo jijini Dar es salaam na maeneo mengine kama Morogoro.Imezuwa wawazo tena kwa watu wanaoishi maeneo ya mabondeni.Mvua hii imenyesha kwa takribani masaa matano mapaka hivi sasa ilipotuma habari hii basi mvua hiyo inaendelea.Mvua hii imeanza majira ya saa 12:00 mchana mapaka hivi sasa.Mbali na hilo jingine na hatari ya kuwa na Sunami kubwa katika nchi zote zilizokatika mwambao wa bahari ya hindi ikiwemo Tanzania na eneo kubwa linalo hofiwa ni Dar es salaam.





Mvua kubwa inanyesha na tayari maji yamejaa.Hapa ni Temeke hospitali na sijui ndugu zetu wa mabondeni hali itakuwaje.Mara mjadala utaanza tena wahame wasihame?
Picha na Mjengwa

Safari ya mwisho ya Kanumba

MAELFU WAJITOKEZA KUMZIKA, WATU 600 WAPOTEZA FAHAMU, POLISI WASEMA HAWAKUTARAJIA UMATI MKUBWA HIVYO

MAELFU ya waombolezaji jana walijitokeza katika mazishi ya msanii nguli wa filamu Tanzania Steven Kanumba (28), yaliyofanyika katika Makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam. Alifariki dunia usiku wa kuamkia Jumamosi ya Aprili 7, mwaka huu.Kabla ya kuzikwa, mwili wa marehemu Kanumba ulipelekwa katika Viwanja vya Leaders ili kuwawezesha waombolezaji kutoa heshima za mwisho. Hata hivyo, ni wachache waliobahatika kupata fursa hizo baada ya kutokea msongamano mkubwa ulioifanya kamati ya maandalizi ya mazishi hayo kusitisha mchakato huo.

Inakadiriwa kuwa waombolezaji wapatao 600 walianguka kutokana na ama msongamano au majonzi ya kifo hicho cha ghafla cha msanii huyo.

Makamu wa Rais, Dk Mohamed Gharib Bilal, Mke wa Rais, Salma Kikwete na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Dk Emmanuel Nchimbi na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe walikuwa wa kwanza kutoa heshima zao za mwisho na kufuatiwa na viongozi wengine wakiwamo wabunge.

Baada ya viongozi hao kutoa heshima zao za mwisho, Dk Bilal na Mama Kikwete waliondoka na kwa mujibu wa ratiba, ilikuwa zamu ya waombolezaji wengine kuaga.

Hata hivyo, kulitokea msongamano mkubwa wa watu kila mmoja akitaka kulifikia jeneza na kulishika. Ilibidi vyombo usalama na walinzi binafsi kufanya kazi ya ziada kurejesha hali ya utulivu katika eneo hilo.

Kutokana na utaratibu mbovu katika kuendesha shughuli hiyo, ratiba ilikatishwa na mwili kuondolewa saa 6:30 kupelekwa makaburini. Kwa mujibu wa ratiba ya mazishi iliyokuwa imetolewa juzi, muda wa kuaga ulipangwa kuanza saa 6:00 hadi saa 9:00 alasiri.

Badala yake, waombolezaji walitakiwa kujipanga kando ya Barabara ya Tunisia ambako gari lililobeba mwili wa msanii huyo lilipita kuelekea makaburini.

Haikuwa kazi rahisi kwa waombolezaji hao ambao baadhi walifika hapo alfajiri kwa ajili ya kutoa heshima zao mwisho kukubaliana na agizo hilo.

“Hatuwaelewi hawa. Sisi hatukuja kuliona jeneza tunataka kumuona ili tujue kama kweli amekufa. Hawa walioandaa utaratibu huu mbovu ni kina nani jamani au wameshindwa kazi?” alisema mmoja wa waombolezaji na kisha kuangua kilio.

Baada ya hali kutulia umati huo wa waombolezaji ulianza kulisindikiza gari la marehemu kwa nyuma huku wengine wakitaka jeneza hilo lishushwe ili walibebe.

Wakati msafara huo ukielekea makaburini, baadhi ya waombolezaji walikuwa wakianguka na wengine kuzirai baada ya kuona jeneza na kuwafanya watoa huduma wa Msalaba Mwekundu kufanya kazi kubwa ya kuwasaidia na kuwapeleka baadhi yao hospitali.

Licha ya umbali kati ya Viwanja vya Leaders na Makaburi hayo ya Kinondoni kuwa karibu, msafara huo ulichukua takriban saa mbili kufika kutokana na kwenda taratibu ili kutoa fursa kwa waombolezaji ambao baadhi yao walilazimika kupanda juu ya miti, kutoa heshima zao.

Baada ya kufika makaburini, iliwalazimu polisi kuongeza nguvu kudhibiti umati huo na kutoa fursa kwa ibada ya mazishi kuendeshwa kama ilivyopangwa.

Wazirai

Mwenyekiti wa Kamati ya Tiba ya mazishi hayo, Dk Nassoro Ally alisema watu wapatao 600 walizirai katika viwango tofauti kutokana na sababu mbalimbali ikiwamo ya watu kujaa na kubanana na hivyo kukosa hewa.

“Watu wamebanana na kukanyagana. Wemekosa hewa na wengine kati yao wanakabiliwa na matatazo ya kiafya, ugonjwa wa pumu, shinikizo la damu ingawa wapo waliokanyagana na kuanguka kutoka katika miti na kupoteza fahamu,” alisema Dk Ally.

Baadhi ya waombolezaji waliozirai ni pamoja na wasanii Wema Sepetu, Jacqueline Wolper na Irene Uwoya.

Wema alizirai baada ya kufika makaburini na Wolper alifikwa na hali hiyo katika Viwanja vya Leaders.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela alisema watu waliopoteza fahamu hawazidi 30.

Alisema watu waliofika kuaga mwili huo walikuwa ni zaidi ya matarajio yao na kuongeza kwamba kwa mazingira shughuli hiyo, eneo hilo lilikuwa dogo akisema sehemu muafaka ilipaswa kuwa Uwanja wa Taifa.

Kauli za viongozi
Akitoa salamu kwa niaba ya Serikali, Dk Nchimbi alisema huu ni mwaka wa mwisho kwa wasanii kuibiwa kazi zao.
Dk Nchimbi ambaye katika salamu zake pia alitoa ubani wa Sh10milioni kwa niaba ya Serikali, alisema wizara yake ikishirikiana na Wizara ya Fedha, Wizara ya Kazi na Ajira na Shirikisho la Filamu Tanzania (Taff), wameshakutana na kujadiliana namna ya kuzuia wizi katika kazi za wasanii.

“Mwaka huu ndiyo mwisho wa kazi za wasanii kuibiwa na nilipenda sana kuona Kanumba akishuhudia jitihada hizi ambazo tumekuwa tukizifanya naye kama mdau mkubwa wa sekta hii,” alisema Dk Nchimbi na kuongeza:

“Jitihada ambazo amezifanya Kanumba enzi za uhai wake ni dhahiri zimejionyesha leo. Mmejitokeza kwa wingi kuja kumuaga hivyo wasanii mnaobaki mnatakiwa kuiga kile alichokuwa akikifanya.”

Rais wa Taff, Simon Mwakifwamba alisema marehemu Kanumba ameacha pengo kubwa katika tasnia ya filamu kutokana na mchango wake mkubwa aliouonyesha katika kipindi kifupi cha uhai wake.

“Kanumba alikuwa balozi pekee wa filamu nchi za nje. Aliitangaza nchi yetu kupitia tasnia ya filamu hivyo tutamkumba daima kwa kutuonyesha njia,” alisema Mwakifwamba.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amewataka wasanii nchini kufuata nyayo za Kanumba na kumkumbuka msanii huyo milele.

“Watanzania wengi wana majonzi makubwa lakini watambue kwamba ni kazi ya Mungu. Kinachotakiwa sasa hili litumike kama somo kwa wasanii wengine kwani leo tunashuhudia Kanumba akiagwa kama mfalme kutokana na kazi yake nzuri aliyokuwa anaiwasilisha kwa Watanzania,” alisema Nape.

Askofu wa Kanisa la African Inland Church (AIC), Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Charles Salala alisema msiba wa Kanumba ni pigo kwa taifa na kuwaasa Watanzania kutenda mambo mema ili kuwa mfano wa kuigwa kwa jamii.

“Leo tupo katika msiba wa mtu ambaye alikuwa ana mchango mkubwa kwa jamii, ndiyo maana tunashuhudia umati mkubwa wa watu ukiwa umekusanyika hapa, lakini jambo ambalo sisi kama binadamu tunatakiwa kufanya ni kuishi maisha mema na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu ,” alisema na kuongeza:

“Marehemu Kanumba aliwahi kuhudumu katika kanisa hili na alikuwa ni mtu mwenye upendo kwa kila mtu ndiyo maana leo maelfu ya Watanzania tupo hapa kumsindikiza ndugu yetu katika safari yake ya mwisho.”
Habari na Mwananchi,Video na Dj Choka.

Alichoeleza Lulu polisi hiki hapa

MSANII Elizabeth Michael (Lulu), ameiambia polisi
kuwa kifo cha Steven Kanumba kimetokana na ugonvi kati yao, huku taarifa nyingine zikieleza kuwa huenda Lulu akafikishwa mahakamani leo.

Habari zilizopatikana jana kutoka Kituo cha Polisi Oysterbay zilieleza kuwa, Lulu alisema kuwa kulitokea ugomvi kati yake na Kanumba baada yeye kuzungumza na simu
kutoka kwa mtu maarufu anayetajwa kuwa mpenzi wake.

"Lulu alisema kuwa ugomvi ulitokana na simu aliyopigiwa na mpenzi wake mwingine, ambaye ni mtu maarufu nchini, ndipo
Kanumba akamfokea na ndiyo ugomvi ukaanzia hapo," chanzo hicho kimesema.

Chanzo hicho kiliongeza kuwa baada ya Kanumba kuanguka, Lulu alitoka nje na kuondoka kwa gari lake hadi maeneo ya Coco Beach, lakini baadaye daktari wa Kanumba alimpigia simu akimtaka arudi ili wampeleke hospitali.

"Alipororudi Sinza ndipo akakamatwa, lakini walikuja Kituo cha Polisi Oysterbay kuchukua PF3," kilisema chanzo hicho.

Chanzo kiliongeza kuwa tangu Lulu alipofikishwa kituoni hapo amekuwa mtulivu asiye na wasiwasi wowote hata katika mahojiano na polisi.

Katika hatua nyingine, Polisi wa kituo hicho jana walipata wakati mgumu baada ya kuibuka kundi la vijana waliotokea makaburi ya Kinondoni kumzika Kanumba, walioandamana wakidai wanamtaka Lulu.

"Tunataka jembe letu", waliimba vijana hao waliofikia 100 wakitokea Barabara ya Ali Hassan Mwinyi huku wakishika majani na kufanya askari waliokuwapo kituoni hapo kuwahi kuchukua silaha na mabomu ya machozi kujiandaa kutuliza ghasia kama zingezuka.

Hata hivyo vijana hao walitawanyika baada ya kuona askari wakiwa tayari kupambana nao na kukimbia maeneo mbalimbali.
Katika hatua nyingine Patricia Kimelemeta anaripoti kuwa,
Msanii Elizabeth Michael maarufu kwa jina la Lulu huenda akafikishwa mahakamani leo kujibu tuhuma za kuhusika na kifo cha Steven Kanumba.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela aliliambia gazeti hili jana kuwa Lulu atafikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni mara baada ya polisi kupata ripoti ya vipimo kutoka Mkemea mkuu wa Serikali.

“Tunasubiri ripoti ya Mkemia Mkuu kubaini chanzo cha kifo hicho kwa sababu wamechukua baadhi ya sampuli za marehemu kwenda kupima na kwamba tutakabidhiwa leo(jana). Kimsingi tukipata tu taarifa hiyo tutamfikisha mahakamani,” alisema Kenyela.

Aliongeza ripoti hiyo itaweza kuwasaidia kuandika mashtaka ili yaweze kufikishwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kumfikisha mahakamani.

Kamanda Kenyela alisema kuwa, ripoti ya madaktari imewasilishwa juzi na kwamba imeonyesha kuwa Kanumba amefariki kwa ugonjwa wa mtikisiko wa ubongo.

Msanii Stephen Kanumba alifariki usiku wa Ijumaa Kuu
Chanzo Mwananchi.

Tuesday, April 10, 2012

LIVE KUTOKA KINONDONI MAKABURINI KWENYE MAZISHI YA STEVEN KANUMBA

Matukio na Picha Na Dj Choka

Hii ni barabara ya Kinondoni kuingia kwenye makaburi ya Kinondoni ilikuwa ni balaaaa yani dah, kule mbele ndio mwili wa marehemu Steven Kanumba ndio unakuja

 Kwa wingi wa watu ilibidi watu wapande juu ya miti lakini baadae waliamuriwa washuke chini na kamanda Kova

 Ray akiwa aamini kama swaiba wake ndio anakwenda kwenye nyumba yake ya milele

 Charlz Baba akiwa na wenzake kutoka Mashujaa Band, Charz ameniambia walikuwa wanatokea Morogoro so waliweza kuwahi makaburini

Kauli ya Mwisho ya Kanumba Kwa Wasanii wenzake

Hii ya pili ni kauli ya mama yake mzazi baada ya kupata habari za Msiba wa mwanae kipenzi Steven Kanumba

LIVE KUTOKA LEADERS KUMUAGA KANUMBA

 Hawa watoto wanaopita ndio watoto waliokuwa wakicheza movie na marehemu Kanumba enzi ya uhai wake

 Mama yake Kanumba aliyenyoosha mkono juu kuwapungia watu waliokuja uwanjani

 Huyu dada hapa mbele alikuwa akilia kwa uchungu sana hadi nilikuwa namuonea huruma

 Hemed na Yusuph Mlela wakiingia

Makamu wa rais Dk. Mohamed Ghalib Bilali 

 Mke wa rais Mama Salma Kikwete

Mbunge wa Mbeya mjini Joseph Mbilinyi akitoa heshima zake za mwisho kwenye mwili wa marehem.
Picha na Matukio na Dj Choka