NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, January 29, 2013

FLAVIANA MATATA ATWAA TUZO YA MWANAMITINDO BORA WA AFRIKA 2012

Mwanamitindo wa kimataifa wa Tanzania, Flaviana Matata ambaye ameng’ara kimataifa baaada ya kushinda tuzo ya Nigeria’s Next Super Model na kuwa mwanamitindo bora barani Afrika wa mwaka 2012 (Africa’s Most Outstanding Model 2012).
Tuzo aliyojishindia mwanamitindo Flaviana Matata.

NI MFANO WAKUIGWA:UMOJA WA BAJAJI MBEYA WATEMBELEA WATOTO YATIMA SIMIKE NA KUTOA MSAADA

Umoja wa Vijana  waendesha Pikipiki za magurudumu matatu Mkoani Mbeya umeamua kuzindua mpango wa  kutembelea  watoto yatima  na kutoa misaada  kutokana na faida wanayoipata baada ya kusaijili umoja  wao na kuchana  na kutumisha  kwenye maandamano ya kisiasa  na kusababisha vurugu Jijini . Hapa umoja huo ukitoa msaada wa sukari mchele chumvi na madaftari kwa watoto yatima wa simike mbeya
Hapa wanaumoja huo wa bajaji mkoani mbeya wakimkabidhi kijana Frank Musa ada ya awamu ya kwanza kwani kijana huyo amefauru kwenda shule ya sekondari itigi lakini alikosa ada ya kwenda shule hivyo umoja huo umetoa kiasi cha shilingi 40,000/ za kuanzia ili aanze masomo
kulia nia mama janeth Njenga yeye amejitole kumsaidia mtoto Franki kwa ada na matumizi yote ya shule mpaka atakapomalisha elimu hiyo ya sekondari 
Wanaumoja hao wa bajaji wametoa msaada kwa watoto hao yatima wenye dhamani ya shilingi 250,000/
Hapa watoto hao wakiushukuru umoja wa babaji mkoa wa Mbeya kwa kuwakumbuka na kuwajali katika chakula
Mama Anna Kasile yeye ndiyo anaewalea watoto hao akiwashukuru wanaumoja hao kuja kuwaona na kutoa msaada kwa watoto hao


“sisi ni vijana ambao tumeamua kuwa wajasiliamali  ambapo tumejipanga kwa ajili ya kuinuana kiuchumi  lakini kutokana na faida tunayoipata  tumeamua kuwa tutakuwa tunaitumia kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima  katika vituo vilivyopo Mbeya  na tutazindua mpango huu mwishoni mwa mwezi.”walisema wanaumoja hao wa Bajaji mkoani Mbeya.
Picha na Mbeya yetu

Sunday, January 27, 2013

Uwanja wa ndege wa Gao wakombolewa

Wizara ya Ulinzi ya Ufaransa inasema kuwa jeshi linaloongozwa na Wafaransa limeuteka uwanja wa ndege wa mji wa Gao, ngome ya wapiganaji ya Kiislamu kaskazini mwa Mali.
Wanajeshi wa Ufaransa wakikaribia Gao, Mali
Daraja muhimu piya wameiteka.
Mapigano yanaendelea.
Gao ni mmoja kati ya miji mikuu mitatu ya kaskazini mwa Mali iliyotekwa na wapiganaji mwaka jana.
Siku ya Ijumaa wanajeshi wa Mali na Ufaransa waliukomboa mji wa Hombor kilomita 160 kutoka Gao.
Umoja wa Afrika umesema unataka kuzidisha idadi ya wanajeshi wa kuweka amani nchini Mali, na imeomba nchi zanachama kujitolea kwa wanajeshi zaidi katika wiki zijazo.
Piya umeuomba Umoja wa Mataifa usaidie kuwasafirisha wanajeshi hao hadi Mali.

Mateka waachiliwa huru Niger Delta

Mabaharia watano wa India waliotekwa nyara mwezi uliopita nje ya mwambao wa Nigeria wameachiliwa huru, kwa mujibu wa kampuni yao.
Jeshi la Nigeria likipiga doria katika Niger Delta

Mabaharia hao wa meli ya mafuta walitekwa wakati watu waliojihami na silaha tele walipoingia kwa nguvu ndani ya meli yao, SP Brussels, katika eneo la mafuta la Niger Delta kusini mwa Nigeria.
Taarifa ya kampuni ya meli hiyo, Medallion Marine, ilieleza kuwa mabaharia hao ni wazima lakini haikueleza iwapo ililipa kikombozi.

Friday, January 25, 2013

Jaji wa mahakama kuu Kenya atekwa nyara [video]

nzioka1 150x150 Jaji wa mahakama kuu Kenya atekwa nyara [video]
Jaji wa mahakama kuu Grace Nzioki, anayeongoza jopo linalochunguza mauaji ya Tana Delta alitekwa nyara jana usiku na ripoti ya uchunguzi wake iliotarajiwa kutolewa hapo kesho kuibiwa.
Majambazi hao walimteka nyara jaji huyo nyumbani kwake na kisha kumpora vifaa kadhaa ikiwemo kipakatalishi, au ukipenda laptop iliokuwa na ripoti ya uchunguzi wa mauaji ya tana.


Je, tunashughughulikia ufumbuzi wa tatizo la elimu nchini?

Shughuli za  kila siku, kwa namna moja au nyingine, zinakupa taswira ya “maendeleo” (neno sahihi katika kipindi hiki ni “mmomonyoko”) wa sekta ya elimu Tanzania. Nadhani wale ambao wako kwenye michakato ya usaili na shughuli kadha wa kadha za kutafuta na kuajiri vijana ambao wamehitimu hatua fulani ya elimu, wako katika nafasi nzuri kujua kama elimu aliyopata mhusika imempa nyenzo za kukabiliana na changamoto za taaluma au kazi fulani na maisha kwa ujumla.
Bahati mbaya sio wote tuna ndugu, jamaa na marafiki ambao kazi zao zinawapa mwanya wa kuona kinachozalishwa na mfumo wa elimu nchini. Hata hivyo, wakati tunaanza kuelewa kinachoendelea kupitia kwao tunakuwa tumechelewa. Tumechelewa sana. Kwa sababu tunakuwa tayari tumeshapoteza kizazi; tunakuwa tunaangalia matokeo ya makosa yaliyokuwa yakifanywa kwa kipindi kifefu.
Juhudi za asasi kama Twaweza/Uwezo na Tamasha Vijana, kufanya tafiti za kina na kuonesha wapi mapungufu yalipo hasa, ni nzuri na zinahitaji heko badala ya kuzikebehi kwa ‘majibu ya kisiasa’. Zinapaswa kutumiwa katika uundaji na mabadiliko ya mitaala na mfumo mpya wa elimu unaoakisi mwelekeo wa ulimwengu huu wa leo.
Pia, napenda kuchukua fursa hii kuhoji: Kwa nini hatukuwa na vigezo vya kutuambia mwelekeo wa elimu katika ngazi mbalimbali? Yaani, hizi ripoti zingetakiwa ziwe zinatoka angalau kila baada ya miaka kadhaa tangu siku sekta ya elimu na wizara husika zilipotengemaa. Hakuna mtu aliyewahi kufikiria hilo? Kama nilivyosema awali, ni dhahiri kuwa mapungufu tunayoyaona sasa hivi ni matokeo ya mapungufu na makosa ya muda mrefu.
Au bado tunaamini ya kwamba mitihani ya mwisho pekee ndio kipimo thabiti cha elimu?
Kwa upande mwingine, wengi wetu — mtu mmoja mmoja — hatuna hulka ya kufuatilia maendeleo ya wadogo zetu, ndugu zetu na watoto wetu mara kwa mara. Wengi tunasikia malalamiko kutoka kwa wengine, lakini hatushtuki hadi pale watoto wetu wanapopata madaraja ya chini kabisa kwenye mitihani ya mwisho (hasa ya kidato cha nne na sita).
Kama umefanya utafiti au umesoma ripoti za tafiti mbalimbali, utakubaliana nami kuwa hatuwatendei haki vijana ambao wapo mashuleni sasa hivi. Sehemu kubwa hawaandaliwi kukabiliana changamoto za dunia ya sasa.
Wapo wenye mawazo tofauti, kuwa tunapiga hatua; vijana wengi zaidi sasa hivi “wanapata elimu”. Bahati mbaya ulimwengu wa leo hauna mipaka. Nchi yetu sio kisiwa. Vijana wa leo hii wanashindana na vijana kutoka kona mbalimbali za dunia. Kwa mantiki hiyo, kama wengine wanaendelea kwa kasi kubwa kuliko sisi, basi sisi tunarudi nyuma!
Mapungufu tunayoyaona ni mengi, lakini wakati waliopo kwenye sekta ya elimu wakijaribu kuyatambua na kuondokana nayo, ni wajibu wetu — mtu mmoja mmoja — kujaribu kufanya kila tunachoweza kuokoa wengi kadri tunavyoweza, kwa kuwa mabadiliko yanayotakikana yatachukua miaka mingi.
Kwa mtazamo wangu, donda ndugu ni sisi kama jamii kwa ujumla kutoheshimu taaluma ya ualimu. Hatujaweza kuwavutia wengi wanaofanya vizuri mashuleni kuingia kwenye fani ya ualimu. Zaidi ya hayo, walimu wachache tulionao hawapewi motisha ya aina yoyote ile.
Ukiacha upungufu wa zana za kufundishia, n.k., kuna mdahalo mzito wa muda mrefu wa lugha ipi itumiwe (sekondari na vyuoni): Kiswahili au Kiingereza?
Tukumbuke kuwa kwenye taaluma yoyote ile, kitu muhimu ni ujenzi wa “msingi”. Hapa namaanisha, kwa mfano kwenye sayansi, “msingi” ni tabia ya udadisi, jinsi mtu anavyofikiri na anavyokabili tatizo fulani. Katika hatua ya ujenzi wa tabia ya udadisi, awali ya yote mwanafunzi anapaswa kuwa na ufahamu wa mambo yanayomzunguka. Na udadisi au ufahamu huambatana na ujenzi wa taswira fulani kichwani.
Je, elimu inamsaidia mwanafunzi kuwa mdadisi? Lugha inayotumiwa inarahisisha zoezi la kujenga msingi, au tabia ya udadisi?

Unapomfundisha mwanafunzi wa kidato cha kwanza kuhusu mwendo kasi, atakuelewa vizuri ukitumia mifano ya gololi, ndulele au billiards? Ukitumia mfano ya billiards pekee, mwanafunzi atatumia nguvu nyingi kukariri (kwa kuwa hajui billiards ni nini) badala ya kuanza kujenga taswira na uelewa wa mwendo kasi.
Mabadiliko ya matumizi ya lugha kwenye masomo kutoka darasa la saba hadi kidato cha kwanza huathiri wanafunzi wengi mno. Wapo wachache wanaouruka hiki kihunzi bila matatizo, ila wengi hupata msaada kwa namna moja au nyingine. Wenye bahati tulikuwa na walimu wenye uwezo wa kutuelezea vizuri kwa Kiswahili rahisi kila palipohitajika. Wenye bahati zaidi tulikuwa tuna wazazi ambao waliweza kutusaidia kujenga taswira ya vitu kama electron kwa kutumia Kiswahili.
Bahati mbaya wengi hawana hizo bahati, hivyo sehemu kubwa ya juhudi zao huelekezwa kwenye kukariri maelezo ya Kiingereza bila kuelewa. Hii ni moja ya vyanzo vya misingi mibovu ambayo huja kuanza kuota nyufa wanafunzi wanapofika ngazi za juu.
Kama moja ya njia ya kutatua tatizo la matumizi ya lugha ya Kiingereza kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza ambao bado hawajakimudu vizuri, kuna kitabu kipya kinachoitwa “Enjoy Chemistry, Furahia Kemia” kilichochapwa hivi karibuni. Kitabu hiki kimeandikwa maalumu kwa ajili ya wanafunzi wanaozungumza lugha ya Kiswahili wanaotaka kujifunza Kemia,
na wakati huohuo wapate kumudu lugha ya Kiingereza ili kufanya majaribio na mitihani ya kufuzu elimu ya sekondari.

Kwa upande wa uhaba wa vifaa vya maabara, kitabu hiki kina maelezo ya kufanya majaribio ya Kemia ambayo yatamwezesha mwanafunzi kujifunza mwenyewe. Maelezo ya kitabu yanasema: “Kwa kuwa shule nyingi za sekondari zina uhaba mkubwa wa vifaa vya maabara maalumu kwa ajili ya somo la sayansi lenye majaribio mengi kama ilivyo Kemia, kitabu hiki pia kinaweka mkazo kwenye mbinu ya fanya-mwenyewe. Mbinu hii itawasaida wanafunzi kuelewa Kemia kwa kina na wakati huohuo kulifurahia somo. Njia hii itawapatia wanafunzi walio kwenye shule zisizo na vifaa vya kutosha fursa sawa ya kufanya majaribio ya Kemia kama waliyonayo wanafunzi walio na bahati ya kuwa katika shule yenye vifaa vingi vya maabara.”
Ni muhimu kusisitiza kuwa kitabu hiki hakibadilishi wala kupindisha mitaala ya Kemia nchini.
Wakati wadau wa elimu wakiendelea kufanya midahalo na mijadala ya mabadiliko katika sekta ya elimu na mitaala, juhudi kama hizi zinatia moyo kwa kuwa naamini zitasaidia kuokoa vijana kadhaa.
Tafadhali, pitia kitabu hiki kisha tupe maoni yako hapo chini. Pia, wataarifu na wengine na wakaribishe kupiga kura juu ya lugha gani itumiwe kufundisha wanafunzi wa ngazi ya sekondari.
Imetolewa na Mzumbe

Je unajuwa nini kinaendelea katika Tume ya Katiba:Jijuze sasa




Karibu Tume ya Mabadiliko ya Katiba 
Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83. Tume ina Wajumbe 32 ikiongozwa na Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti. Tume ina Sekretarieti inayoongozwa na Katibu na Naibu Katibu.
 Kwa mujibu wa kifungu cha 9 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, jukumu kuu la Tume ni kuratibu na kukusanya maoni ya wananchi kuhusu mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Aidha, jukumu la Sekretarieti ni kuiwezesha Tume kufanya kazi zake.

  Kuhusu Tume

Tume ya Mabadiliko ya Katiba imeundwa kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83. Jukumu kuu la Tume ni kuratibu na kukusanya maoni ya wananchi kuhusu kupatikana Katiba Mpya.
Tume pia inatekeleza majukumu mengine yafuatayo:-
a)           Kuandaa na kuendesha programu za kuelimisha umma;
b)           Kuitisha na kusimamia mikutano na mabaraza ya katiba;
c)           Kutathmini na kuchambua maoni ya wananchi;
d)           Kupitia na kuchambua michango, mawazo, maoni, taarifa na mapendekezo yaliyokusanywa na
              kufanyiwa tathmini siku za nyuma;
e)           Kupitia na kutafiti usahihi na ulinganifu wa masharti ya kikatiba yanayohusu mamlaka ya wananchi,
              mifumo ya kisiasa, demokrasia, utawala wa sheria na utawala bora;
f)            Kumuomba mtu yeyote kufanya majadiliano na Tume au kuwasilisha nyaraka kuhusu mabadilioko ya Katiba;
g)           Kuchapisha Rasimu ya Katiba katika Gazeti la Serikali na magazeti mengine ili kutoa fursa kwa wananchi kusoma
              na kutoa maoni zaidi kwa Tume kupitia mabaraza ya Katiba;
h)           Kutayarisha na kuwasilisha ripoti kwa kila hadidu ya rejea; na
i)            Kuwasilisha Rasimu ya Katiba katika Bunge Maalum la Katiba

Saturday, January 19, 2013

"STORY FUPI YENYE MAFUNZO KWENU WADADA




Hii ni Barua toka kwa Dada
Nilipoingia katika mahusiano naye
nilimuamini, nikampa kila kitu
nilichoweza. Nakumbuka enzi zile
nyumbani tulikuwa tuna ng’ombe, niliiba maziwa kila siku na kumpelekea kwao.
Akanenepa!!
Penzi letu likawa huru alipoanza maisha
yake mwenyewe. Sikuwa najua lolote
kuhusu mapenzi.

Alinifundisha.
Nikaegemeza maisha yangu yote kwake.Akanifany a nikawa mtumwa wa
ngono kila nikienda chumbani kwake.
Kama haikutosha sasa akaanza
kunifundisha kunywa pombe. Niliamini
kuwa ndiye mume wangu mtarajiwa,
kwa nini nikatae?

Nilimkubalia kila kitu. Alinilazimisha ngono hata nilipokuwa
katika siku zangu. Kweli nilikuwa
msomi na niliyajua madhara ya kufanya
hivyo lakini sikutaka kumuudhi huyo
niliyeamini kuwa ni mume wangu.
Nilipenda tututmie kinga lakini aliipinga sana. Nikapata mimba ya kwanza!!
Hakuwa na pesa lakini alinilazimisha
niitoe. Nikaiba pesa nyumbani
nikafanyaalivyo taka. Kwa mara ya
kwanza nika toa mimba.
Haikuniuma sana!! Niliamini kuwa ni yeye atakuja kunioa na atanifichia aibu hii.

Nilitegemea sasa tutaanza kutumia
kinga. Lakini hapana haikuwa hivyo.
Aliendelea kunilaghai. Tayari aliujua
udhaifu wangu. Alinishika hapa na pale.
Nikishtuka tayari amefanya anavyojua. Pombe kidogo na nyingine kidogo.
Nikazoea lakini nikawa na wahi kulewa.
Akautumia udhaifu huu kunifanyia jambo
baya lililonifanya niandike haya kwako.

Akaniingilia kinyume na maumbile.
Alinilawiti!! Nilishindwa kumshtaki popote.
Nikavumilia kwa kuwa alikuwa mume
wangu mtarajiwa. Mume asiyejulikana
hata kwa wazazi.
Mchezo ule ukaendelea. Akajitetea eti
hataki nipate mimba tena, hivyo hiyo ni mbinu mbadala.

Najuta kumuamini!!
Lakini huyo alikuwa mume wangu.
Miaka ikapita, ule urembo wangu
niliozoea kuuona katika kioo ukatoweka,
simu za mara kwa mara kutoka kwake
zikatoweka, akawa mkali sana kwangu. Hakutaka niende kwake. Wakati huo
nilikuwa nasoma chuo.
Pesa ya mkopo ikitoka ananitafuta na
tunakuwa marafiki tena. Anasema
ananipenda na atanioa. Ananilewesha na
kunitumia kinyume na maumbile. Pesa ikiisha na mapenzi yanaisha
nabaki mwenyewe katika msoto. Sasa
akaanza kubadilisha wasichana waziwazi.
Ningesema nini mimi?

Ninajua alishindwa kusema neno moja
tu. Tuachane!! Nilijua tayari ameniacha!!!
Afya yangu ikadolola sana,
nikalazimika kwenda kupima hospitali.
Sikuwa na virusi. Nikapewa ushauri
nikautumia.
Siku zikasonga nikampata mwanaume mwingine. Huyu alikuwa ananijali sana.
Nikaanza kumsahau yule aliyenitenda.
Nilipomaliza chuo akajitambulisha
nyumbani na alitaka kunioa.

Akanioa kweli. Maisha yakaanza. Mwaka
wa kwanza, mwaka wa pili na hadi wa tatu. Sikuwa nabeba mimba.
Mume wangu alikuwa mvumilivu sana,
hakuwahi kunilaumu. Lakini niliumizwa
na mawifi. Nikaamua kwenda hospitali.
Nikaambiwa kizazi changu kiliharibiwa
kwa kutoa mimba mara kwa mara. Pia mapenzi ya kinyume na maumbile
yamenivuruga kabisa.

Nililia sana huku nikimkumbuka yule
aliyeuleta uchungu huu kwangu.
Dunia haikuwa mahali pangu sahihi.
Nimekuandikia barua hii mdogo wangu.Uisome mwenyewe!! Lakini
uwasimulie wengi baada ya kifo changu.
Uwasimulie bila kuchoka wasichana wa
kileo wanaodanganyika na kufanya
mambo magumu kuwaridhisha wapenzi
wao. Waambie watakufa kwa mateso kama mimi.
Wasipokusikiliz a usijisikie vibaya maana
hata mimi nilikuwa siwasikilizi watu
waliponambia lolote kuhusu yule
mume mdanganyifu .
Sitajiua lakini nitakufa kabla ya wakati!!!

Nimekuandikia wewe kwa kuwa u
mwandishi. Japo kwa sasa u mtoto
mdogo najua utaipata nafasi siku moja
ya kuwafikishia wasichana hawa.
Usilie kwa sababu nitakufa. Lia
kwasababu mwanaume mwenzako AMENITENDA HIVI!!! TAFADHARI TAFAKARI''

Friday, January 18, 2013

Uvumbuzi wa Sukari Angani

Je ulikuwa unafahamu kuwa sukari ina vimelea muhimu vya uhai? Ingawa hii haimaanishi kuwa kula vitu vitamu kwa wingi ni kuongeza uhai. Sukari imetengenezwa kwa fomula rahisi iliyotokana na kemikali ziitwazo carbon, hydrogen na oxygen. Kemikali hizi ndizo zilizojenga karibu kila mwili wa kiumbe hai anayepatika hapa duniani pamoja na kemikali nyingine ya nitrogen.
Hivyo basi timu ya wanaastronomia kwa kutumia telescope yenye nguvu wameweza kuona sukari kwenye gesi zinazopatikana kuzunguka nyota ndogo yenye ukubwa sawa na Jua letu. Sukari ilishawahi kuonekana angani, lakini hii ni mara ya kwanza kuonekana kwa ukaribu katika nyota inayofanana na Jua. (Umbali uliopo kati ya sukari hii na jua ni sawa na umbali uliopo kati ya Jua na sayari ya Uranusi). Na kwa vile sukari ina vimelea vya maisha, kuonekana kwake karibu na nyota inayofanana na jua ni habari nzuri sana. Kitu ambacho kinaonyesha kuwa maisha kama yetu yanawezekana kupatikana katika sayari nyingine ulimwenguni!
Wanaanga hawa wamegundua pia, sukari hii huingia ndani kuelekea katika nyota. “ Sukari hii siyo tu kwamba ipo katika sehemu sahihi ya kuweza kuingia kwenye sayari, lakini pia inasogea kuelekea katika uelekeo sahihi” anasema mwanaastronomia Cécile Favre.
Jihusishe: Je ni kitu gani ungeweza kukigundua kama ungekuwa unashughulika na moja kati ya telescope kubwa zaidi Duniani? Papo hapo ili kusheherekea miaka 50 ya Kituo cha Anga cha Ulaya Kusini unaombwa kupiga kura juu ya kitu umbacho ungependa kichunguzwe na telescope yake kubwa iitwayo VLT!

KATIKA KUHAKIKISHA DAR ES SALAAM PANAKUWA PASAFI GREEN WSTE PRO IMEANDAA KAMPENI YA KUSHIRIKISHA WANANCHI


Katika kuhakikisha jiji la DAR ES SALAAM linakuwa safi Kampuni ya GREEN WASTE PRO imeandaa kampeni ambayo itawashirikisha wananchi na vikundi mbali mbali kushiriki katika zoezi la usafi litakalofanyika mwishoni mwa wiki
MENEJA MSAIDIZI wa kampuni hiyo ABDALLAH MBENA amesema wananchi wanahitaji elimu yak kutosha juu ya namna gani wanaweza kuweka mazingira yao safi na kwamba kwa kupitia kampeni hiyo wananchi wataweza kujinufaisha kiuchumi kupitia taka rejea na kuweka mazingira yao safi na salama.
Kwa upande wake MENEJA UENDESHAJI wa kampuni hiyo ELIZABETH SCHEEPERS amesema takataka zinafaida nyingi ikiwemo kutumia madafu kutengenezea mkaa ambao utawasaidia watanzania kuepukana na suala la ukataji miti ovyo

Thursday, January 17, 2013

HIVI NI LINI WATOTO WA KIBONGO MTAACHA KUWANUNULIA BOXER WAPENZI WENU??



Haya jamani wadada wa kitanzania, wadada wa Dar es Salaam, wakaka wanaulizaa lini mtaacha kuwapa zawadi za boxer na vest na kuanza kutoa zawadi za maana kama wadada wenzenu wa nje..??


Wakionesha kuchoshwa kabisa na zawadi hizo wakaka hao walienda mbali zaidi na kutolea mifano ya zawadi ambazo wasichana wa nje wamekuwa wakitoa kwa wapenzi wao ambapo walianza na Mariah Carey ambaye alimnunulia pete mpenzi wake ambaye sasa ni mume wake Nick Cannon yenye thamani ya dola milioni mbili..



Awakuishia kwa Mariah Carey, waliendelea mbeleee, wakamzungumzia na Kim Kardashian aliyemnunulia baby dady wake Kanye West gari ya kifahari ya LAMBORGHINI yenye thamani ya dolla laki 7.5 kwenye birthday ya baby wake..




Wakamalizia kwa mama Blu Ivy Beyonce!! Alimpa mume wake Jay Z private jet yenye thamani ya dola millioni 40 kwenye Father's Day.



Lakini wao wanaambulia boxer na vest kwahiyo wanawaomba mbadilike muendane na mfumo wa digitali, hayo mambo ya vest na boxer ni analogia yashapitwa na wakati..



Hako ni kajiutani tu msichukulie kama vipi japo kunakaujumbe

WAMECHOKA!!

PROFESSOR JAY AMKUBALI VANESSA MDEE..


Hii ni tweet ya Processor Jay kwa Vanessa Mdee, ilionyesha kiasi gani msanii huyu mkubwa na nguli Tanzania kumkubali vilivyo Vanessa Mdee ambaye anaonekana kuwa moto wa kuotea mbali kwa sasa..


Tuesday, January 15, 2013

Je? Unafahamu kuwa Wanawake wanauwezo mkubwa zaidi wa kunusa.

Wenyewe hawajui lakini, mwanamke anaweza kunusa hasira, naam ikiwe mumewe ana hasira hata akikaa kimya , mkewe atakuwa wakwanza kujua kwamba mmmh! leo kumeharibika.
Mwanamke pia anaweza kunusa uogoa wa mumewe.
Dr Gün Semin wa Utrecht University, Ujerumani anasema hii ni kutokana na jasho la mwanamume!
Utafiti unaonyesha kuwa jasho analotoka mwanamume linatuma ujumbe katika kiwili wili cha mwanamke na kumuambukiza hali unayosikia bila ya wewe kumuambia kitu.. Jasho lako linatuma ujumbe kwa mkeo au kwa mchumba wako.
Ukiwa wewe mwanamume umeshutshwa na kitu au umebabaika au umeogopa au ana hasira. Jasho lako litasema. Na System ya mama itapokea ujumbe!
Dr Gün Semin wa Ujerumani anasema mwanamume akikasiria anatoa jasho lenye kemikali aina fulani. Akiwa na uoga anatokwa na jasho aina tofauti.
Ndio maana mkeo au mchumba wako atakuuliza kuna nini lakini? Hata ukikataa mwili wake unamuashiria kwamba lazima kuna kitu. Sio ati wao ni wajanja sana lakini jasho lako limetoa chembechembe fulani kulinagani na hali yao na hivyo kutuma ujumbe wa siri kwa system ya mama.
Ni majaliwa ya wanawake hayo.
....
Kipepeo aweza kunusa mpenzi wake akiwa mbali
Vipepeo wanawake pia wanamajaliwa ya kuweza kunusa vitu.
Wanasayasi wanasema kipepeo ana uwezo wa kunusu kipepeo mchumba wake au anayemfaa hata akiwa maili 7 au nani hivi.
Kipepeo atanusa nakujua kiboko yangu anakuja japo yuko kilomita nyingi.
Nani mwenye uwezo mkubwa zaidi wa kunusa? Kwa wanyama ni Dubu, yaani bear, sio teddy bear.
Baharini ni papa. Papa anaweza kunusa hata damu amboyo bado ingali ndani ya samaki mwengine. Ni papa huyo.
..............
Wanasayansi wanasema kuwa wanawake ni viumbe wa ajabu!
Katika mahusiano ya kawaida, urafiki tu wa kimapenzi, boy friend na girl friend wanawake bila ya wao kujua huvutiwa na watu wakaidi, watukutu watu wenye miguvu kuvu, misuli misulu, watu wenye vimo virefu kwa kiingereza hao wabajulikana kama Alfa men.
wabasayansi wanasema watu wenye vurugu vurugu , watundu wanauwezo mkubwa wa kutongoza.
Pengine hii nikutokana na sababu ya kutoogopa kukataliwa.
........
Lakini katika ndoa wanawake bila ya wao hata kujijua huvutiwa na watu wadhaifu , watu waungwana, wastaarabu, wenye hekima watu wenye vimo vya wastani.
Wanawake wanapenda Alpha men kama wapenzi tu
Hata enzi za adamu na hawa mambo yalikuwa vivyo hivyo.
......
Watafiti wa maswala ya kijamii na mahusiano wanasema kuwa kwa akina dada wengi katika ndoa huvutiwa na watu wasio na misuli, wenye vimo vya wastani au hata wafupi - hawa kimombo wanajulikana kama Beta men- B-E-T-A, Beta, baada ya Alfa , kuna Beta katika alphabeti za kirumi.
Kwanini ieve hivyo.
Sayanmsi ya mahusiana inasema kuwa watu wasiokuwa nguvu, vimo vya kutisha au misulu eti, eti wanajali sana familkia zao na wake zao.
Maelezo ni kwamba
kwa kuwa hawaezi kushindana katika ulimwerngu wa mahaba kwa kutumia nguvu na kifua basi mwenyezi mungu amewapa sifa za kuwa wakarimu, wenye kutoa, kujali wapenzi wao , na kama njia ya kutinza ndo zao Mungu amewapa watu sampuli hiyo uwezo wa kuwa waaminifu. Wasipo kuwa hivyo kuna hofu ya kutorokwa!
Ni sayansi ya mahusiano!
.........
Jee unajua kuwa kufanya kazi usiku ni hatari kwa akina mama? Na inaweza kusababisha kifo?
Utafiti uliofanywa na madaktari nchini Uingereza umegundua kuwa wanawake wanaopendelea kufanya kazi usiku wanahatari ya kupatikana na sartani ya matiti- breast cancer.
Katika kichwa cha Kazi za usiku zinasababisha vifo 500 kila mwaka nchini Uingereza utafiti hunasema shift za usiku ni hatari kwa akina amma.
Dr Lesley Rushton, wa Imperial College Mjini London anasema Mawanamke akifanya kazi ya usiku kwa wastani ya siku tatu kwa wiki kwa miaka sita - anakaribisha kansa ya matiti.
Kufanya kazi usiku au kukosa usingizi kwa akina mama kunatatiza utengenezaji wa homoni ya ya MELATONI, hii ni chembechembe inayosaidia usingizi na hii inasadikiwa kuwa na uwezo wa zuia kansa.
................
Wanasayansi wana mambo!
Dawa ya kuzuia nyumba ndogo
Sasa kumegunduliwa dawa aina ya homoni inayoweza kuwazuia wanaume kwenda nje, au kuwa na uhusiano wa pembeni,
Dawa hii iliyovumbuliwa Ujerumani inaitwa FIDELITY HORMON. Dawa ya uaminifu! Au kampuni hiyo ya ujereumani imeipa dawa hiyo jina la CUDDLE DRUG! Dawa ya kukumbatiana.
Dr René Hurle­mann, of Bonn University nchini Ujerumani anasema mwanamume akipewa dawa hii ya kumeza huyeyuka na kuingia katika damu, hivyo mwanamke mrembo akipita karibu, basi mume analazimika kukaa umbali wa inchi sita . Mume bila kujua damu yake itakuwa haipatani na mwanamke mwengine mbali na mkewe.
Mwanamke huyo akiwa mrembo zaidi , ndio dawa inafanya kazi vizuri zaidi. Ni FIDELITY HORMON. Tembe za uaminifu.
.....
iPad inaweza kusababisha maradhi ya moyo
The iPad ni komputa ndogo ya mkoni hii inatengezwa na kampuni ya Apple Ipad yakanzwa ilinza kuuzwa tarehe 3 April mwaka 2010 NA iPada ya kisasa zaidi imetolewa tarehe 2 novemba mwaka huu wa 2012.
Ipada inaweza kupiga picha ya video, picha ya kawaida , kucheza muziki , kuzuru mtandao na mambo mewngi tu.
Lakini ujajua kwamba ukiwa na tabia ya kutumia Ipad usiku usiku huenda ukapatikana na matatizo ya moyo au msongo au kudorora kwa afya, yaani depression?
Utafiti pia unasema kuwa ukiwa na tabia ya kuangali televisheni hadi usiku mpevu kila mara basi unakaribisha maradhi ya moyo au depression.-kudorora kwa afya.
Profesa Samer Hattar anasema wa Marekani anasema utafiti umegundua kuwa televisheni na komputa ya iPad inatoa mwanga usistahili wakati mwili unahitajika kulala.
Hivyo kutumia iPad na televisheni usiku sana inaweza kusababisha maradhi ya moyo au mtu kukosa raha maishani au kutompenda starehe au mkuwa mtu pweke, kutumia iPad au televsiheni kila mara usiku sana kunasababisha upweke.

Nigeria kutwaa kombe la Afrika 2013?

SPORTS/MICHEZO

 
Kikosi cha Nigeria
Wacheza kamali wanataka kucheza karata zao vizuri kuhusu kinyang'anyiro cha ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2013. Wacheza kamali hao wataelekeza karata yao katika timu ya Nigeria wakiipa nafasi ya kuwa katika timu tatu bora za juu.
Timu ya Nigeria, The Super Eagles, imeshiriki mara 16 katika mashindano ya kombe hilo na kushinda mara mbili, ikishika nafasi ya pili mara nne na mara saba katika nafasi ya tatu, ikiwa ni rekodi ya kujivunia katika kipindi cha miaka 50.
Ni katika mwaka 1963 na 1982 (ikiishia raundi ya kwanza) na 2008 (robo fainali) Eagles wakishindwa kutwaa medali na wanaonekana wamejipanga angalau kuingia nane bora katika fainali za mwaka 2013 nchini Afrika Kusini baada ya kupangwa katika kundi C pamoja na timu za Burkina Faso, Ethiopia na Zambia.
Kocha wa timu ya Nigeria, Stephen Keshi
Timu zinazoshika nafasi ya kwanza na ya pili katika makundi, husonga mbele na kuingia robo fainali. Nigeria na mabingwa watetezi Zambia wanapewa nafasi ya kusonga mbele. Kwa mshangao timu ya Nigeria, The Super Eagles, walishindwa kufuzu katika fainali za mwaka 2012zilizoandaliwa kwa pamoja kati ya Gabon na Equatorial Guinea na ilimgharimu kocha wake Samon Siasia wakati aliposhindwa kuongezewa mkataba.
Kocha wa sasa Stephen 'Big Boss' Keshi, kocha asiye na mzaha ambaye alikuwa katika kikosi cha wachezaji wa Nigeria walioishinda Zambia kwa kuilaza magoli 2-1 katika fainali zilizofanyika Tunisia, miaka 19 iliyopita. Alikuwa mchezaji kiungo imara ambaye aliongoza kwa mfano na alitumia wiki chache zilizopita kufanya mazoezi katika kambi nchini Ureno akijaribu kujenga moyo wa ushindi kwa timu yake ya Super Eagles.
Obi Mikel akidhibiti mpira
"Nataka wachezaji wenye njaa ya kusaka ushindi, wenye kujitolea na ambao wanajivunia kuchezea timu ya taifa ya Nigeria," amesisitiza kocha huyo ambaye alipambana na Togo na Mali bila kufuzu hatua ya kwanza katika mashindano yaliyotangulia ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
"Ni vizuri kuona wachezaji wakifanya jitihada kuwania namba katika kikosi changu cha kwanza. Ushindani huo unanipa changamoto nzuri. Hakuna mwenye namba ya kudumu katika timu-- ni lazima wapiganie na pia wapiganie kuhifadhi namba wanayopataKocha wa Mlinzi wa kati na nahodha wa Super Eagles, Joseph Yobo, analeta changamoto sawa katika rekodi ya mchezaji bora wa zamani wa mwaka wa Afrika Nwankwo Kanu kwa kucheza katika fainali sita za Kombe la Afrika.
"Kushinda kombe si kazi rahis lakini naahidi kutafanya kwa uwezo wetu wote kufikia lengo hilo. Nawaomba Wanaigeria kutuombea na kuwa na imani na timu hii,"anasema mchezaji huyo kiungo wa zamani wa Everton ambaye kwa sasa anacheza soka nchini Uturuki.
"Tunasafiri kwenda Afrika Kusini tayari kupeperusha bendera ya taifa letu na hatutachoka hadi tutakapotimiza lengo letu. Bahati nzuri tuna kikosi kizuri cha wakufunzi ambacho kinatufahamu vizuri na nina uhakika wachezaji wako tayari kwa hilo.

Wapiganaji wauteka mji mwingine Mali


Wapiganaji wa kiisilamu walioteka Kaskazini mwa Mali
Wapiganaji wa kiisilamu wameuteka mji uliokuwa unadhibitiwa na wanajeshi wa serikali licha ya harakati za kijeshi dhidi ya wapiganaji hao kwa usaidizi wa Ufaransa.
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian alisema kuwa mji wa Diabaly, ambao uko umbali wa kilomita 400 kutoka mji mkuu ulitekwa katika makabiliano yaliyofanyika kati ya wapiganaji hao na wanjeshi Jumatatu.
Bwana Le Drian alisisitiza kuwa harakati za jeshi la Ufaransa zimeweza kupiga hatua.
Aliongeza kuwa wapiganaji hao waliweza kutoroka na kukimbilia Mashariki mwa nchi lakini akakiri kuwa wanjeshi wa Ufaransa wanakumbwa na wakti mgumu kukabiliana na waasi ambao ambao wamejihami vilivyo.
Awali waziri wa mambo ya nje wa Ufaransa, Laurent Fabius alisema kuwa harakati za jeshi la Ufaransa katika kusaidia wanajeshi wa Mali dhidi ya wapiganaji wa kiisilamu hazitachukua muda mrefu sana.
Juhudi zao zitadumu tu wiki chache.
Mnamo Jumapili, Jeshi la wanahewa la Ufaransa liliimarisha mashambulio yake dhidi ya wapiganaji hao hasa kwenye miji ya Gao na Kidal.
Wizara ya Ulinzi ya ufaransa inasema mashambulizi hayo yatakamilika katika muda wa wiki kadhaa.
Maeneo ambayo tayari yametwaliwa na jeshi la Mali kwa usaidizi wa Ufaransa
Mamia ya wanajeshi kutoka mataifa ya Afrika Magharibi wanatarajiwa kujiunga na wanajeshi wa Ufaransa. Tayari Uingereza imetoa ndege mbili za kijeshi kusaidia katika usafirishaji wa wanajeshi na vifaa nchini mali.
Jeshi la Ufaransa lmekuwa likipambana na wapiganaji hao tangu Ijumaa , wakisaidia wanajeshi wa serikali kutwa maeneo yaliyotekwa na wapiganaji hao na hata kufanikiwa kutwa mji wa Konna.
Ufaransa imeitisha mkutano na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, baadaye hii leo.
Akiwahutubia waandishi wa habari,bwana Fabius alikataa kikosi kushirikishwa kwa muda mrefu kama ilivyo nchini Afghanistan chini ya NATO.
''Baadaye tutaweza kuondoka lakini hatuna nia ya kukaa hapa kwa muda mrefu.''
Bwana Fabius alisema kuwa ikiwa Ufaransa isingeingilia mgogoro huu, kulikuwa na tisho la wazi kuwa wapiganaji hao wangeweza kuingia zaidi ndani ya Mali na hata kufika mji mkuu Bamako, huku athari kubwa zikijitokeza.