Kwa habari za burudani na michezo makaliery-t ndio blog yako nitumie na kutoa taarifa kwa email makalimachechi@yahoo.com ipate tangazwa hata biashara pia
Thursday, March 29, 2012
VODACOM FOUNDATION YAKINUFAISHA KIJIJI CHA INYUMBU MKOANI DODOMA KWA VISIMA
Mkuu wa Mfuko wa kusaidia Jamii wa Vodacom Tanzania(Vodacom Foundation) Yessaya Mwakifulefule (kwenye picha ya juu),akimsaidia kumweka ndoo kichwani mama mmoja kati ya wakazi wa kijiji cha Inyumbu Mkoani Dodoma, baada ya kukabidhi msaada wa mradi wa maji wenye thamani ya shilingi milioni 40 katika kijiji hicho.
DUNIANI KUNA MAMBO: MATATANI KWA KULEWESHA MBWA
Bwana
mmoja nchini Marekani amekamatwa na polisi baada ya kumpa pombe mbwa
wake na kumlewesha kiasi cha mbwa huyo kushindwa hata kutembea.
Bwana huyo Todd Harold Schreiner, anashtakiwa kwa kosa la kutesa wanyama. Polisi wa mji wa East Helena walikuta mbwa huyo akiwa amelewa chakari, mara nne zaidi ya kipimo cha wanadamu kinachoruhusu kuendesha gari.
Taarifa zinasema mbwa huyo aitwaye Arly II wakuweza kusimama au kutembea vyema wakati alipokutwa na polisi ndani ya baa moja saa tano na nusu usiku.
Mbwa huyo alichukuliwa na kupelekwa katika zahanati ya wanyama ambapo vipimo vilionesha ana ulevi wa asilimia sifuri nukta tatu nne nane katika damu yake.
Kisheria kipimo cha mwisho cha ulevi wanaadamu wanaruhusiwa kuwa nacho na kuendesha gari ni asilimia sifuri nukta sifuri nane. Muuzaji katka baa aliyokutwa mbwa huyo amesema mwenye mbwa alimpa mbwa wake kilevi aina ya vodka.
Bwana huyo Todd Harold Schreiner, anashtakiwa kwa kosa la kutesa wanyama. Polisi wa mji wa East Helena walikuta mbwa huyo akiwa amelewa chakari, mara nne zaidi ya kipimo cha wanadamu kinachoruhusu kuendesha gari.
Taarifa zinasema mbwa huyo aitwaye Arly II wakuweza kusimama au kutembea vyema wakati alipokutwa na polisi ndani ya baa moja saa tano na nusu usiku.
Mbwa huyo alichukuliwa na kupelekwa katika zahanati ya wanyama ambapo vipimo vilionesha ana ulevi wa asilimia sifuri nukta tatu nne nane katika damu yake.
Kisheria kipimo cha mwisho cha ulevi wanaadamu wanaruhusiwa kuwa nacho na kuendesha gari ni asilimia sifuri nukta sifuri nane. Muuzaji katka baa aliyokutwa mbwa huyo amesema mwenye mbwa alimpa mbwa wake kilevi aina ya vodka.
Monday, March 26, 2012
PAKA MREFU DUNIANI KWA SASA
Guinness World Records
has officially recognized cat named Trouble largest cat in the world.
Representatives of the Guinness Book of Records measured the cat and
veterinarians Savannah breed (a cross between an African wild cats (serval)
and domestic non-pedigreed cats) from the clutches of up to shoulder height
(height of 48 cm) and stated that this cat is a leopard - the world's longest
cat.
Despite this remarkable growth, Trouble weighs a little - only about 9
pounds, because they do not like to eat a lot and has a very active life,
constantly running around like a real wild cat.
The owner of a cat-American champion Debbie Maraspina from Sacramento,
Calif., said she was proud of his pet, which is 3 years, and despite the fact
that it belongs to the breed, the cats that are considered the largest in the
world, her cat Trouble even walked the length of the bodies of their
relatives.
Saturday, March 24, 2012
Kikwete awashukia wabunge, madiwan
RAIS Jakaya Kikwete amewataka viongozi na wanasiasa wakiwamo wabunge na madiwani kuacha kusababisha migogoro kwa maslahi yao binafsi katika kusimamia maji ya Bonde la Mto Rufiji kwa lengo la kulinusuru bonde hilo.Pia Rais Kikwete ameagiza Mto Ruaha usimamiwe vizuri kwa sababu maji yamekauka na kuhatarisha uchumi wa taifa kwa kuwa unatumika kuzalisha umeme na chakula.
Rais Kikwete alitoa rai hiyo baada ya kufanya ziara katika maeneo mbali mbali ikiwamo Pawaga unakopita Mto Ruaha na kuona jinsi maji yalivyopungua kwenye mto huo.
Akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Maji mkoani Iringa, Rais Kikwete alisema hakuna njia ya mkato kunusuru bonde hilo isipokuwa viongozi wa serikali kusimamia kiukamilifu.
“Wakati Serikali inapoamua kusimamia mazingira ikiwamo kuwaondoa watu kwenye vyanzo vya maji, wabunge na madiwani acheni kusababisha migogoro kwa maslahi yenu binafsi, acheni tamaa ya kuomba kura kwa kutumia bonde hili badala yake angalieni maslahi ya Taifa.
“Kama itatokea vita kuu ya tatu ya Dunia, basi itakuwa vita ya kupigania maji, hali imekuwa mbaya sana na hakuna njia ya kujinusuru zaidi ya kufanya mabadiliko tena haraka,” alisema Kikwete.
Alisema ikiwa maji yataendelea kupungua kwa kasi, uchumi wa taifa utayumba kwa kuwa Taifa linategemea bonde hilo kujiendesha kiuchumi na kuzalisha umeme katika mabwawa ya Mtera na Kidatu sambamba na chakula kinachozalishwa kwenye mabonde Usangu, Kilombero na Rufiji.
“Itafika wakati chakula kitakuwa tabu, umeme shida na asilimia 80 mpaka 90 ya umeme na chakula nchini, kinapatikana katika Bonde la Ruaha, lazima tuchukue hatua za kulinusuru haraka bonde hilo,” alisema.
Kutokana na hali hiyo aliziagiza wizara zinazohusika kutafakari hatua za haraka ili kunusuru maji katika mabonde hayo.
Rais Kikwete alisema maji yamepungua nchini kwa sababu baadhi ya watu wamekuwa wakiharibu mazingira kama vile kukata miti, kuchoma moto hovyo na kuishi karibu na vyanzo vya maji.
Alisema uharibifu huo umesababisha kuwapo kwa vipindi virefu vya tatizo la ukame na mafuriko.
Alisema kwa nchi zilizoendelea, suala la viwanda limekuwa likihatarisha amani ya nchi kutokana na kuwapo kwa mabadiliko makubwa ya tabia nchi.
“Wakubwa wanaochafua mazingira wamekuwa wabishi kuchukua hatua kunusuru mazingira, hali hii itaendelea kuwa mbaya zaidi kwa sababu tayari kina cha bahari kimepanda, joto limeongezeka na kipindi cha ukame kimeongezeka,” alisema Kikwete.
Alisema ipo haja kwa viongozi kusimamia kwa ukaribu suala la mazingira na upatikanaji wa maji ili kuweza kufikia malengo ya millennia ikiwemo suala la wananchi wote kufikiwa na huduma ya maji safi na salama.
Rais Kikwete alizindua miradi mikubwa ya maji miwili Mkoani Iringa wa kwanza ukiwa wa maji safi na taka wa manispaa ambao umegharimu zaidi y ash Bil 73 na kuweza kufikisha asilimia 96 ya wananchi wote wanaopata huduma ya maji safi.
Mradi mwingine ni wa Pawaga ambao umefadhiliwa na kanisa la Aglikan na kughalimu zaidi ya sh Bil mbili, ambao umewafikia zaidi ya wananchi 20,500 wa maeneo hayo.
Aliwataka wananchi kutunza miradi hiyo ambayo imefadhiliwa na Jumuiya ya Watu wa Ulaya na Ujerumani ili kuepuka tatizo la upatikanaji wa maji ambalo lilidumu kwa muda mrefu.
Awali Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Dr Christine Ishengoma alisema mkoa huo umeanza kuhifadhi vyanzo vyake vya maji.
Habari na Mwananchi
Thursday, March 22, 2012
Raia wa Zambia wazua vurugu mpakani Tunduma
Vurugu
zimeibuka katika mji mdogo wa Tunduma mpaka wa Tanzania na Zambia
kufuatia wananchi wa Zambia kudaiwa kuwazuia wafanyabiashara kutoka
Tanzania kuvuka mpaka kwenda kufanyia biashara zao nchini humo.
Kutokana
na hatua hiyo, Watanzania nao walijibu mapigo kwa kuwatimua raia wa
Zambia waliokuwa wakifanya biashara zao upande wa Tanzania na hivyo
kusababisha kuibuka kwa vurugu katika mpaka huo.
Mkuu
wa Wilaya ya Mbozi, Gabriel Kimolo, akizungumza na NIPASHE jana mjini
Vwawa alisema baada ya kujulishwa kutokea kwa vurugu hizo, Kamati ya
Ulinzi na Usalama ya Wilaya imekwenda mjini Tunduma ambako walijadiliana
kwa pamoja na hatimaye vurugu hizo kudhibitiwa.
“Ni
kweli nimejulishwa kuwapo kwa tukio hilo. Lakini kimsingi hazikuwa
vurugu kubwa. Kamati ya Ulinzi na Usalama imeweza kulishughulikia suala
hilo na sasa hali imetulia katika mji huo,” alisema Kimolo.
Hata
hivyo, alisema vyombo vya ulinzi na usalama vimechukua hatua ya
kuimarisha ulinzi katika kila kona ya mji huo ili kusitokee machafuko
zaidi yatakayoleta athari kwa wananchi wa Tunduma na wageni kutoka nchi
mbalimbali.
Kaimu
Afisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Mji wa Tunduma, Aidan Mwashiga,
alisema vurugu hizo ziliibuka baada ya wananchi wa mji wa Nakonde Zambia
kuendesha operesheni ya kuwatimua Watanzania wanaofanya biashara
zisizokuwa za halali katika mji huo.
Alisema
kufuatia hali hiyo, Watanzania nao walichukua hatua ya kuanza kuwatimua
wafanyabiashara wa Zambia wanaofanya biashara zao katika mji wa Tunduma
na kusababisha kutokea kwa vurugu.
Hata
hivyo, alisema vurugu hizo zimedhibitiwa na vyombo vya ulinzi na
usalama na kwamba askari wamewekwa tayari katika mji wa Tunduma ili kama
kutaibuka vurugu ziweze kudhibitiwa.
Mji wa Tunduma umekuwa mara kadhaa ukikumbwa na vurugu zinazosababishwa na wafanyabiashara wa pande mbili.
Mwaka
2005, mfanyabiashara wa Tanzania aliuawa na askari polisi wa nchini
Zambia na hivyo kusababisha mpaka wa Tanzania kufungwa kwa siku tatu
hadi serikali ilipomaliza tatizo hilo kwa kukaa na serikali ya Zambia.
Waziri
wa Mambo ya Ndani, Shamsi Vuai Nahodha, alipofanya ziara wilayani
Mbozi, aliagiza Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kuimarisha ulinzi katika
mji wa Tunduma kufuatia kutokea kwa matukio ya vurugu mara kwa mara
katika mji huo.
CHANZO:
NIPASHE
Tembelea hifadhi za Taifa wakati wa Pasaka

Bodi
ya Utalii Tanzania (TTB) kwa kushirikiana na makampuni ya usafirishaji
watalii ya PongoSafaris, Burco safaris na Cordial Tours kwa pamoja
wamekutayarishia wewe mwananchi ofa kabambe ya Pasaka ya kutembelea
Hifadhi za Taifa za Ruaha, Mikumi na mji wa kihistoria wa Bagamoyo kama
ifuatavyo.
SAFARI YA RUAHA/MIKUMI
Kuondoka Dar: (Asubuhi) 3/4/2010
Kuondoka Ruaha: (Asubuhi) 5/4/2010
Gharama: 250,000/= (Mtu mzima)
Kuondoka Dar: (Asubuhi) 3/4/2010
Kuondoka Ruaha: (Asubuhi) 5/4/2010
Gharama: 250,000/= (Mtu mzima)
SAFARI YA MIKUMI
Kuondoka Dar: (Asubuhi) 5/4/2010
Kurudi (Jioni): 5/4/2010
Gharama: 40,000/= (Mtu mzima)
Kuondoka Dar: (Asubuhi) 5/4/2010
Kurudi (Jioni): 5/4/2010
Gharama: 40,000/= (Mtu mzima)
SAFARI YA KULALA MIKUMI
Kuondoka Dar (Asubuhi): 4/4/2010
Kurudi (Asubuhi): 5/4/2010
Gharama : 90,000/= (Mtu mzima)
Kuondoka Dar (Asubuhi): 4/4/2010
Kurudi (Asubuhi): 5/4/2010
Gharama : 90,000/= (Mtu mzima)
SAFARI YA BAGAMOYO
Kuondoka Dar (Asubuhi): 4/4/2010
Kurudi Dar (Jioni): 4/4/2010
Gharama: 25,000/=( mtu mzima)
Kuondoka Dar (Asubuhi): 4/4/2010
Kurudi Dar (Jioni): 4/4/2010
Gharama: 25,000/=( mtu mzima)
- Gharama za watoto kwa safari zote zitakuwa kama ifuatavyo: Miaka 0-3 (Bure); Miaka 4-10 (50% ya gharama ya mtu mzima)
- Gharama zote zinajumuisha: Usafiri, Ada za viingilio, Malazi, Uongozaji, Chakula na vinywaji baridi. Makampuni hayatahusika na ghara nyinginezo kama vile vileo, sigara n.k.
- Kiwango cha chini cha idadi ya watu wanaohitajika kwa kila safari ni 15
PONGO SAFARIS & TOURS LIMITED
NIC Life house, 3rd floor, Sokoine Drive/Ohio Street, DSM
Tel: +255-22-2135728 Mob: +255 714354444
Email: info@pongosafaris.com
NIC Life house, 3rd floor, Sokoine Drive/Ohio Street, DSM
Tel: +255-22-2135728 Mob: +255 714354444
Email: info@pongosafaris.com
BURCO SAFARIS
Ground floor, NSSF Water front house,
Sokoine Drive, DSM
Tel: +255-22-2128010/2125408
Email: safaris@burco.co.tz
CORDIAL TOURS
Tel: +255-22-2136259 Mob: +255 754 270784
Email: info@cordialtours.com
Ground floor, NSSF Water front house,
Sokoine Drive, DSM
Tel: +255-22-2128010/2125408
Email: safaris@burco.co.tz
CORDIAL TOURS
Tel: +255-22-2136259 Mob: +255 754 270784
Email: info@cordialtours.com
Wednesday, March 21, 2012
Taswira Toka Kisiwa cha Mbudya
Tuesday, March 20, 2012
EBWANA DA MWANADASHOST LINA AKIWA MBEFELE MAREKANI
Mapic ya kufa mtu
Dar kukosa maji siku mbili
Baadhi
ya vitongoji vya jiji la Dar es Salaam vinatarajia kukosa huduma ya
maji kwa siku mbili kutokana na kupasuka kwa bomba kubwa linalosambaza
huduma hiyo katika eneo la gereji Wilaya ya Bagamoyo.
Chanzo:Nipashe
Afisa
Uhusiano wa Mamalaka ya Maji safi na Maji taka (Dawasco), Teddy Mlengu,
alisema baadhi ya maeneo ya Jiji la Dar es Salaam yanatarajiwa kutopata
huduma ya maji kutokana na kupasuka kwa bomba kubwa linalosambaza
huduma hiyo katikati ya jiji
Maeneo yatakayoathirika na huduma hiyo, kuwa ni Mbezi Beach, Kawe, Tegeta, Sinza, Mwenge, Ilala, Mwananyamala na Bunju.
Alisema
mafundi wanashughulikia tatizo hilo kwa juhudi kubwa na wanatarajia
kulifunga kesho na kuwataka wakazi wa maeneo hayo kutumia maji kwa
uangalifu kwa kujiwekea akiba ya kutosha.
Mlengu alisema Jumamosi walilazimika kuzima mtambo unaosambaza huduma ya maji katika maeneo hayo kutokana na hitilafu ya umeme. Chanzo:Nipashe
Wanajeshi waua raia watano kwa risasi
Watu
watano wameuawa kwa kupigwa risasi na wengine wanne kujeruhiwa baada ya
kuzuka tafrani baina ya wananchi na wanajeshi waliokuwa wakishirikiana
na mgambo kuendesha operesheni maalum ya kuwaondoa waliovamia eneo la
hifadhi katika kijiji cha Maguba, kata ya Igawa, tarafa ya Malinyi
wilayani Ulanga.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Adolphina Chialo, alithibitisha kutokea kwa
mauaji hayo saa Jumamosi iliyopita saa 8:00 mchana.
Waliouawa
ni Sanyiwa Ndaya (34), Lutaya Ndala (48), Nchambi Bujiku (28), Kulwa
Luhende (48) na Shija Msheshiwa (35), ambaye alifariki wakati akipatiwa
matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Ulanga. Wote wakazi wa Kijiji cha
Mguba, kata ya Igawa.
Waliojeruhiwa
na kulazwa Hospitali ya Wilaya ya Ulanga ni Nkama Jisonge (35), Zina
Msheshiwa (30), Msheshiwa Taiya (60) na MT 70328 Koplo Paulo Lawrent
ambao hali zao zimeelezwa kuendelea vizuri.
Akifafanua
kuhusiana na tukio hilo, Kamanda Chialo alisema kuwa siku ya tukio
askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Job Edward (54) Ofisa Mteule wa
daraja la pili, ambaye ni mshauri wa mgambo wilaya ya Mahenge akiongoza
timu ya watu 15 akiwemo askari mwingine wa jeshi hilo, MT 70328 Koplo
Paulo Lawrent na mgambo, walikwenda katika eneo hilo kwa ajili ya
operesheni maalum ya kuwaondoa watu waliovamia hifadhi hiyo.
Kwa
mujibu wa Kamanda Chialo, watu hao baada ya kufika walivamiwa na
wananchi waliokuwa na silaha za kijadi na walipojaribu kujitetea, Koplo
Lawrent aliyekuwa na bunduki aina ya SMG alifyatua risasi hewani ili
kuwatawanya wananchi hao ambao waliendelea kupambana nao.
“Na
yeye huenda katika kunusuru silaha ile isiporwe na wananchi, alirusha
risasi hewani zilizopoteza maisha ya wananchi wanne pale pale katika
eneo la tukio, huku mwananchi mmoja akifariki dunia wakati akipatiwa
matibabu katika Hospitali ya Wilaya ya Mahenge,” alisema Kamanda Chialo.
Kufuatia
tukio hilo, Chialo alisema watu wanane wamekamatwa na wanahojiwa na
polisi ili hatua zaidi za kisheria dhidi yao zikuchukuliwe na kuongeza
kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi zaidi kuhusiana na tukio hilo.
Awali,
ilidaiwa kuwa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Morogoro ilikwenda
katika eneo hilo na kuwazuia wananchi kuendelea na shughuli za kilimo
na uharibifu wa mazingira katika eneo hilo la hifadhi, lakini walikataa
kwa madai kuwa hawafahamu mipaka kati ya eneo lao na eneo la hifadhi.
Inadaiwa
kuwa mipaka hiyo iliwekwa na Serikali na wananchi hao kutakiwa kutii
mamlaka ya Serikali kwa kuacha kufanya uharibifu ndani ya hifadhi bila
mafanikio, hadi ilipofanyika operesheni hiyo katika eneo hilo ambalo ni
hifadhi ya wanyamapori linalomilikiwa na wizara ya Maliasili na Utalii.
Habari kamili na Nipashe
Hii ndio Tanzania tembea ujionee
Hii ilikuwa Oktoba 2011 - Mto Rufiji
Mto Rufiji ulivyo Sasa hivi...
Uwanja mdogo wa ndege wa Mtemere - Selous GR
Ni
Uwanja mdogo wa ndege wa Mtemere uliopo pembezoni mwa geti la Mtemere,
geti la kuingilia kwenye pori la akiba la Selous huko Mloka Rufiji. Ni
uwanja ambao unatumika zaidi na ndege ndogo ambazo huleta wageni ukanda
wa Mtemere. Selous kuna viwanja kama hivi kadha wa kadha vingiwe vikiwa
chini ya usimamizi wa hotel ambazo ndio watumiaji wakuu. Picha hizi
zilipigwa wakati wa kumalizia game walk ambapo tulikuwa tunarudi kwenye
geti la mtemere ili tuendelee na mambo mengine. unayoiona kwenye picha
ya juu ni njia ya kurukia na kutua ndege - runway - ya uwanja huu.
Mashirika
kadhaa ya ndege ndogo yana safari za kila mara (scheduled) kwenda
Selous kupitia kiwanja hiki. Coastal Air ni mojawapo.
Eneo la maegesho ya ndege wakati wa kushusha na kupakia abira.
Magari ya hoteli na makampuni mengine yakiwa pembe ya uwanja yakisubiri ndege ya coastal ili wapokee wageni wao. Coastal hupeleka ndege mara mbili kwa siku ktk kiwanja cha Mtemere. Ya kwanza hutua saa nne asubuhi na ya pili (mwisho) hufika majira ya saa kumi jioni.
Taswira toka Selous GR
Mama na mwana
Wababe wa majini wakiwa ndani ya moja ya maziwa ndani ya pori la akiba la Selous.
Inaelezwa ya kwamba Viboko ndio wanaongoza kwa kujeruhi na kuua watu barani Afrika (kusini mwa Sahara) kushinda mnyama mwingine yeyote yule wa porini.
Inaelezwa ya kwamba Viboko ndio wanaongoza kwa kujeruhi na kuua watu barani Afrika (kusini mwa Sahara) kushinda mnyama mwingine yeyote yule wa porini.
Mtaani tunasema ukiona manyoya ujue kaliwa..
Porini wanasema ukiwaona hawa jamaa wapo chini ujue kaliwa pia
Porini wanasema ukiwaona hawa jamaa wapo chini ujue kaliwa pia
Shughuli ya sharubu ni usiku, mchana ni siesta kwa kwenda mbele
Kipanga
Subscribe to:
Posts (Atom)




















