NJOMBE

NJOMBE

Saturday, March 30, 2013

PICHA 4 ZA RAIS KIKWETE KWENYE ENEO GOROFA LILIPOPOROMOKA LEO DAR ES SALAAM


.
.
.
.
.
.
.
Mkuu wa mkoa Said Meck Sadick akiwa na Rais Kikwete na Kamanda wa polisi kanda maalum Dar es salaam Suleiman Kova, picha zote kutoka kwa mwandishi wa habari Mtoki ambae pia ni mmiliki wa mrokim.blogspot.com

PICHA 6 ZA JENGO LA GOROFA LILILOANGUKA LEO DAR ES SALAAM



.
.
.
.
.
.
.
Picha zimepigwa na Ramadhani.
Kwa maelezo ya shuhuda, inasemekana limeanguka saa moja asubuhi ambapo kwa muda huo kulikua na watoto wa kihindi wanacheza mpira, kulikua na vibarua ambao wanataka kumwaga zege kuendelea na ujenzi na ndio walikua wanabadilisha nguo kuanza kazi.
Ni posta mtaa wa Indira Gandhi pembeni ya msikiti mkubwa wa Itnasheri, lilikua ni gorofa la floor 12 ambapo mpaka sasa hakuna hesabu kamili ya vifo lakini shuhuda anasema kwa muda mfupi baada ya kuanguka alishuhusia maiti nne.
Sehemu ya chini zinaonekana bado nzima hazijadondoka ila kifusi cha kutoka juu ndio kimefunika lakini kuna watu ndani yake wako hai na inaripotiwa wanapata hewa vizuri na wamekua wakiwapigia ndugu zao na kuwaita waje kwenye eneo la tukio.
Endelea kuwa karibu na millardayo.com taarifa zaidi zinazidi kufatiliwa.
.
.
hii picha imepigwa na Salma Msangi wa Channel ten ambae unaweza kutazama kazi zake pia kupitia salmamsangi.com
hii picha imepigwa na Salma Msangi wa Channel ten ambae unaweza kutazama kazi zake pia kupitia salmamsangi.co
m habari na matukio na Millardayo

Tuesday, March 19, 2013

STAMINA AFUNGUKA JUU YA UANDISHI WA MASHAIRI A.K.A MISTARI NA DAU LINAKWENDAJE




Baada ya kusumbuliwa sana na wasanii wachanga na wasanii wakubwa tu katika game la mziki wetu, kumtaka awaandikie nyimbo, Stamina ameamua kufunguka na kusema sasa ni wakati wa kuanza kutoza hela katika uandishi, baada ya kuandika hits kadhaa alizogoma kuzitaja..
"kuna swala moja nataka niliweke wazi, maana toka mwakajana mwishoni nasumbuliwa sana na watu wa kawaidaa, wasanii wa kawaida na wasanii wengine wakubwa tu amabao sitaki kuwataja, wamekuwa wakinitaka niwaandikie nyimbo, wengine wanauliza kabisa bwana utatuchaji sh ngapi, wengine wanataka kisela, na kuna baadhi ya hit songs nimeziandika...
"mwisho wa siku leo nataka nitangaze wazi kwamba, mtu yeyote atakaetaka nimwandikie wimbo, aidia ikiwa yake, naandika wimbo mmoja wenye verse 3 kwa 2,50,000 aidia ikiwa yake, na aidia ikiwa yangu yaani anataka kila kitu niandike mimi, yeye anataka tu wimbo naandika kwa 300,000, hizi ni bei zangu nimeona bora niziweke wazi, maana nasumbuliwa sana na watu...kama ni mwanangu naweza mfanyia bure tu lakini kwa sasa bora niweke wazi tu."

Friday, March 15, 2013

Audio) Nay wa mitego ft Diamond Platnumz - Muziki Gani


Nay na Diamond ndani ya studio wakiwa wanaandaa ngoma hiyo ya muziki gani




SONG: MUZIKI GANI
ARTIST: NEY WAMITEGO FEAT DIAMOND
PRODUCER: MR TOUCH

CHORUS
Hivi nyi ma mc mnachoimba kitu gani, mara bangi mara matusi sa ndo muziki gani (diamond).
Hii no hip-hop h.o.p muasisi wa burudani, tushachoshwa kutwa mapenzi, kabane Pua nyumbani (ney)  X2 

DIAMOND
Hata bibi yangu mi aliniambia , mwanamke anahitaji kubembelezwa
Kupetipeti matunzo pia, ukienda rafu utampoteza,
Muziki ni mfano wa binti muzuri,
Na ndio maana namtunza kwa   vazi na uturi

NEY WA MITEG
Aaah piga kimya, we ndo haufai kabisa hauna maana
Wabana pua kila siku mnarogana, bibi yako alikuambia muziki ni kama binti
Mbona unawachezea unawatema kama big g
Mara wema, mara Jo keti, mara Naj, mara Penny, je mnafanya mziki mpate mabinti

DIAMOND
Uuuhhuuuu, hata wazee wazamani, walishasemaga kazi na dawa
Chamuhimu jukwaani, ni kuhakikisha wanapagawa,
Kwa michezo ya kuringa ringa  ndo huwa wanadata
Badilika usiwe mjinga, utawakamata

CHORUS
Hivi nyi ma mc mnachoimba kitu gani, mara bangi mara matusi sa ndo muziki gani (diamond).
Hii no hip-hop h.o.p muasisi wa burudani, tushachoshwa kutwa mapenzi, kabane Pua nyumbani (ney)  X2 
  
NEY WA MITEGO
Muziki wenu ushirikina ndio umetawala, q chilla analalama anasema umemroga
 Mganga wako aliekutoa umemkimbia hujalipa,  bila skendo za magazeti basi huskiki

DIAMOND
Mi ni mti wenye matunda, milele siogopi kupigwa mawe
Ubaya wenu wengi kayumba, elimu mliitupa sandakalawe

NEY WA MITEGO
Bado hujanishawishi, bongo fleva inanipa kichefu chefu
Kwanza nyie malimbukeni wa umaarufu
Mnalenta maringo mpaka kwa mashabiki , Wabana pua nyie watoto sio riziki,
Mnavaa nguo za dada zenu, zinawabana mapaja nyie makaka duu
Aah nyie watoto mchele mchele , kwenye show viuno mbele mbele X2
Nimewanyamazisha, brazameni vipi  we bado unabisha

DIAMOND
Mi nnamengi nnayajua, ila we ni mtemi utaanzisha utata
Michezo yenu kutoboa pua, bora ninyamaze usinipige mbata 

Thursday, March 14, 2013

PAPA MPYA APATIKANA - FRANCIS WA KWANZA

Kadinali Jorge Mario Bergoglio wa Argentina amechaguliwa kuwa Papa mpya wa Kanisa Katoliki.
Kadinali Bergoglio anakuwa mtu wa kwanza kutoka Amerika kusini kuchaguliwa kuwa Papa.
Mara tu baada ya kuchaguliwa alichagua jina la Papa Francis I.
Awali moshi mweupe ulishuhudiwa ukifuka kutoka bomba la kutolea moshi katika kanisa la Sistine Chapel na kufuatiwa na kengele kupigwa. Hii ilikuwa ni ishara kwa walimwengu kuwa makadinali ambao walianza mchakato wa kumchagua Papa mpya hatimae walikuwa wamefaulu katika kazi yao.
Kadinali Bergoglio anachukuwa mahali pa Papa Benedict XVI, ambaye alijiuzulu mwezi uliopita akisema hana nguvu na uwezo wa kuendelea kuliongoza Kanisa Katoliki.
Makadinali 115 wamekuwa faraghani tangu siku ya Jumanne alasiri na wakaanza mchakato wao kwa kupiga kura mara nne kwa siku.
Ilikuwa inahitajika kuwa angalau Makadinali 77 yaani theluthi-mbili wangeliweza kumpigia kura mmoja wao ili aweze kutangazwa kuwa Papa mpya.

Na kabla ya mchakato huo kuanza kulikuwa hakuna dalili za kuonyesha nani angelichaguliwa.

Tuesday, March 5, 2013

541938N0snQhfG[1]Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma (UDom,) Bernadeta Minja, amefariki dunia papo hapo na watu wengine 11 wamejeruhiwa katika ajali ya basi la kampuni ya Muhamed Trans likitokea Dar es salaam kwenda Dodoma baada ya kupata ajali katika eneo la Kiegea Gairo barabara ya Morogoro Dodoma . Chanzo cha ajali ni uzembe wa dereva wa basi wakati akijaribu kupita lori lililoharibika.

541448glERpca2[1]

Ronaldo kwa mara ya kwanza Tangu 2009 ndani ya Trafoo ya Zamani

   Mchezaji wa zamani wa Manchester United Christiano Ronaldo kwa mara ya kwanza anarudi kucheza nyumbani tangu aondoke mahali hapo 2009.Mchezaji huyo anafurahi kufika kwa mara nyingine Old Traford kwani amenukuliwa akisema anajisikia amani sana anapofika mahali kama hapo na kumkumbusha mengi katika historia yake ya mpira.Na vile mashabiki wanavyomkaribisha anajisikia vyema ndio anakasema Manchester ni nyumbani kwangu.
  Ronaldo anarudi kwa mara ya kwanza na timu yake Real Madrid inayochuana leo majira ya 10:45 PM saa tano kasorobo usiku katika mechi ya marudiano ya Mechi za mabingwa baada ya mechi ya kwanza timu hizo kutokuzidiana nguvu na kutoka sare ya 1-1 ndani ya Bernabeu 
 
Ukiwa kama mshabiki na mpenzi wa mpira na hasa kwa wale washabiki wa Manchester United Unakumbuka nini unapoona vidio hii na ukihusisha na Cr7 alivyosema.
                                                             Coming Home


Sunday, March 3, 2013

HIVI TUNAENDA WAPI:MWALIMU AUAWA KWA RISASI NA POLISI HUKO MAKETE KWA KOSA LA KUTOVAA HELMET


Mwili  wa  mwalimu aliyeuwawa  kwa  kupigwa  risasi na  polisi Makete  kisa kutovaa Helment (kofia ya  pikipiki)
 
Mwalimu mmoja wa shule ya sekondari kitulo wilayani makete aliyefahamika kwa jina la casto sote kawamba ameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa jeshi la polisi Makete
 
Akizungumza na mtandao huu wa www.francisgodwin.blogspot.com mkuu wa polisi wilaya ya Makete SP Peter Kaiza kuhusu tukio hilo lililotokea eneo la benki ya NMB tawi la Makete jana majira ya saa moja na robo alisema kuwa mwalimu huyo alikuwa anakwenda kupata huduma za kibenki kupitia mashine ya kutolea pesa ya ATM akiwa na pikipiki ndipo alipo amuliwa na askari mmoja aitwae Jose Msukuma na kukutwa na umauti huo .
 
Inadaiwa kuwa kisa cha mauwaji yake ni madai kutovaa kofia hiyo na baada ya kuitwa na askari hao alikaidi amri na kutaka kumgonga askari huyo aliye kuwa lindo.
 
Nae mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Makete Idd Nganya ambaye ndie mwajiri wa marehemu amesema kuwa mwili wa marehemu bado umehifadhiwa katika hospitali ya wilaya ya makete wakati utaratibu wakusafirisha mwili huo kwenda kwao mbeya kwa ajili ya mazishi ukiendelea


Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo ambaye jina lake limehifadhiwa amesema kuwa askari hao walikuwa wakiomba fedha kwa mwalimu huyo na baada ya kukataliwa ndipo walipo anza kumshushia kichapo na alipo wazidi walilazimka kutumi asilaha na kumpiga begani kwa risasi


Walimu wenzake na marehemu ambao walifika hospitali kujua kuhusina na kifo cha mwalimu mwenzake wameeleza kusikitishwa na tukio hilo na kulifananisha na tukio la kikatili machoni pao
Mganga mkuu mfawidhi ambaye ni msemaji wa hospitali ya wilaya ya makete Dr Michael Gulaka amesema kuwa wao walipokea mwili wa marehemu na sio majeruhi

Tuesday, February 26, 2013

Serikali ya Tanzania kuwaibia wananchi wake.

Mkutano uliofanyika AICC Arusha
Ndugu zanguni mtaniwia radhi kwa kusema haya najuwa ni kipindi kirefu sana nimekaa kimya ni kutokana na hali tu na mambo kuwa mengi, Ila nikaona sio vyema napopata nafasi yakushirikiana nanyi katika mambo kadhaa hasa ya maisha ni vyema.Hivi Hii Serikali yetu haina ya kufanya inawaza namna ya kuwaibia wananchi wake kila siku bila kuwaboreshea maisha wananchi wake.Hebu tujiulizeni kodi wanazokatwa wafanyakazi zinawasaidia nini hao wafanyakazi na bado pia bado Nchi inaenda kukopa nchi za nje, Bado haitoshi inakopa kwenye mifuko ya jamii kama NSSF na mingineyo na bado hairudishi.Hivi tunakwenda wapi,Ikaona haitoshi sasa inataka kuzui wafanyakazi hao wanaokatwa kodi na pia kuchangia mifuko ya jamii wasipate hela zao hadi miaka 55 wakati kwa mtanzania wa kawaida anaishi miaka 47 hadi 49 sasa hiyo miaka 55 mfanyakazi huyo atachukuwa mafao yake akiwa kaburini kama sio uwizi ni nini tena sio uwizi ni ujambazi mkubwa. Hii imenitoka akili baada Mbunge wa Kigoma Mh Zitto nae kutaka mfuko huo uchukuliwe akipingana na sera ya Mbunge mwenzie toka Chama cha Demokrasia na maendeleo Mh John Mnyika kutaka watu wawewanapata fedha zao kila waachapo kazi au kusimamishwa.Kutoka na hiyo imenijenga kwamba wanasiasa wote ni sawa hakuna anatoka chama gani wala ni nani.Kuna jambo limenitoa imani kabisa na viongozi wetu, hebu tuchukue hii kama changa moto wote najuwa tunalijuwa kundi la wasanii wa bongo flavor linalojulikana kama leka tutigite kutoka Kigoma likiwa chini ya Mh huyo, Kama mheshimiwa huyu haja pata kitu kidogo kuwakandamiza wananchi ni nini.Kapata nafasi hiyo na kaliambia kundi lake hilo lifanye wimbo kwa ajiri ya mifuko ya jamii hapa wewe unakuwa na imani na viongozi hao,Sijatoa hewani ni mambo yanayoendelea ndani ya serikali yetu na sio kama wanataka kufunga kwa makubaliano bali inaonekana ni kwa lazima.

Mwenyewe husika na vidio au nyimbo hiyo maoni yako kuwakomboa wafanyakazi na wananchi na nchi kwa ujumla

Tuesday, February 5, 2013

MWENGE ILIVYOTEKETEA KWA MOTO JANA

Baadhi ya wafanyabiashara eneo la Mwenge stendi ya daladala wakijaribu kuokoa mali zao baada ya maduka yao kuungua moto.
MADUKA kadhaa ya vipodozi, nguo yameungua moto na kusababisha hasara kubwa kwa wamiliki wake.
Moto huo umetokea mishale ya saa 5.20 leo asubuhi baada ya kutokea hitilafu ya umeme kwenye moja ya kibanda cha biashara.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, moto huo ulianza taratibu kisha kupamba moto.
Wafanyabiashara wa maduka ya vipodozi ndiyo waliopata hasara kubwa kwa mali zao kuharibika kufuatia kutaka kuziokoa.

Hata hivyo, Kikosi cha Zima moto kilichofika eneo la tukio kwa wakati na kimepongezwa kwa kufanya kazi nzuri na kuweza kuudhibiti moto huo.
Adha, jeshi la polisi limepongezwa kwa kazi nzuri lililoifanya ya kudhibiti vibaka ambao walijiandaa kufanya uhalifu wa kuiba mali katika kurupushani hizo za uokoaji.
Askari wa Kikosi cha Zima moto akizima moto huo uliokuwa ukiunguza maduka ya vipodozi.
Wananchi wakishuhudia tukio hilo.
Baadhi ya maduka ya vipodozi yakiungua moto.
Wanausalama wakidumisha amani eneo hilo.

BREAKING NEWS: MSANII WA BONGO FLEVA BUI BUI APATA AJALI

Tweet toka kwa Mh.Zitto Zuberi Kabwe

So I miss this whole session of parliament! My question to be asked by on new licenses to north Mara mine and Mkuju uranium
Mheshimiwa Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma kaskazini anasikitika kukosa bunge la leo pale ukizingatia swali zuri toka kwa Mheshimiwa Tundu Lissu akiulizia juu ya vibali vipya ikiwemo mgodi North Mara na Mkuju Uranium

Na tweet toka kwa watu wakiendelea kutafuta ufafanuzi zaidi
  1. lukuvi na ndugai wanaboa sana
  2. Why are you missing the entire session??
  3. Kwanini unamiss? unahitajika sana bungeni kwani changamoto zako zinaifanya SERIKALI isijisahau
  4. Why you miss that session, So what are the feedback from Mh. Lissu

Monday, February 4, 2013

KARUECHE TRAN KWENYE ROLLING OUT NA RIHANNA KWENYE ROLLINGSTONE COVERS

Baada ya Karrueche Tran kwa mara ya kwanza kutokea kwenye magazine cover Rolling Out na kuingia mtaani, Rihanna ametokea kwenye cover ya Rolling Stone Magazine akiongelea mahusiano yake na Chriss Brown. Rihanna ameliambia gazeti hilo anasema “ Niliamua ilikuwa muhimu zaidi kwangu kuwa na furaha, Nisingeacha maoni ya mtu yeyote yaje kiivyo, hata kama ni kosa , kosa ni langu, baada ya kuchafuliwa sana kwa miaka mingi, kunifanya niwe nahasira na kuniweka gizani, bora niishi maisha yangu ya ukweli na kujibu mashambulizi. Naweza sana” Alisema Rihanna Na kuendelea kusema “ Ukiongeza kipande kutoka nje, sio tatizo sana duniani. Unatuona tukitembea kuelekea sehemu Fulani, kuendesha gari kuelekea sehemu Fulani, studio, club na unadhani unajua. Lakini ni tofauti sasa hivi, hatuna yale malumbano ya aina ile tena. Tunaongea kuhusu upuuzi, Tunaheshimiana. Tunajua kabisa nini tunacho sasa, na hatutaki kupoteza. Siwezi kusema hakuna kitu tena kitaenda kinyume lakini na uhakika itamshtua, Alisema Rihanna kupitia Rolling Stone Magazine.

PICHA MBALIMBALI ZA KUUNGUA JENGO LA PPF TOWER

Jengo la PPF Tower jana liliwaka moto na chanzo cha moto huo haijajulikana.Kwa maelezo zaidi na habari zaidi tutaendelea kuwapa.