NJOMBE

NJOMBE

Tuesday, July 30, 2013

BINTI ALIYETOROKEA UINGEREZA KUKWEPA KUOLEWA NA MFALME MSWATI III...

KUSHOTO: Tintswalo Ngobeni. KATIKATI: Sherehe za kimila ambapo Mfalme huchagua mke kati ya wasichana hao. KULIA: Mflame Mswati III.

Msichana mdogo ameomba hifadhi ya ukimbizi nchini Uingereza baada ya kukataa kwa dharau harakati za ndoa za wake wengi za Mfalme Mswati III wa Swaziland na kugoma kujiunga kwenye nyumba harimu ya wake 13.

Tintswalo Ngobeni, mwenye umri wa miaka 22, alitimkia Uingereza kutoka taifa hilo la kusini mwa Afrika akiwa na umri wa chini ya miaka 18 baada ya kuvuta hisia za mfalme huyo milionea, mtawala maarufu mkandamizaji kwa maisha yake ya anasa.
Ikiwa ni sehemu ya mila za Swazi, Mfalme Mswati III, mwenye umri wa miaka 45, ameruhusiwa kuchagua mke mpya kila mwaka.

Tintswalo, ambaye sasa anaishi mjini Birmingham, alikuwa na umri wa miaka 15 tu wakati Mfalme huyo alipofanya harakati zake baada kumuona kwenye jumba la kifalme la mke wake wa nne, LaNgangaza. Binti huyo alisema 'alitishika' pale alipogundua dhamira zake za ndoa.

Aliongeza: "Alianza kunipigia simu kwenye shule ya bweni. Aliniuliza kama ningetaka kuwa sehemu ya familia ya kifalme. Ilinibidi kukaa kimya kuhusu mashaka yangu lakini nilifahamu sikutaka kuolewa naye na kujitolea maisha yangu kwa mfalme huyo.
"Wake zake wamewekwa kwenye majumba yao, wakizingirwa na walinzi, na hakika hawawezi kwenda kokote isipokuwa tu mfalme akisema hivyo. Kitu pekee wanachofanya ni kwenda Marekani mara moja kwa mwaka, wakati mfalme huyo anapowapatia posho kwa ajili ya manunuzi."

Tintswalo alikuwa amelazimishwa kuachana na maisha ya starehe kwenye shule moja ya bweni huku shangazi yake, ambaye alikuwa mlezi wake mkuu, akisuka mipango ya kutorokea Uingereza kuungana na mama yake, ambaye alihamia mjini Birmingham miaka mitano kabla, akimtoroka mume wake mnyanyasaji.

"Sikuwa na jinsi," alisema. "Hakuna aliyewahi kumwangusha mfalme huyo au kuthubutu kumdharau, hivyo nikatoweka tu."

Tangu kuwasili nchini Uingereza, Tintswalo amekuwa sauti ya upinzani dhidi ya utawala kandamizi za Swazi, ambapo vyama vya upinzani vya siasa vimefungiwa na wanaharakati wamekuwa wakikamatwa mara kwa mara au kushambuliwa.

Hatahivyo, shughuli kuu za Tintswalo, ikiwamo maandamano ya kila wiki nje ya ubalozi wa Swazi mjini London akiwa na kikundi cha Swazi Vigil, zimesikika kwa mamlaka hizo nchini kwake na sasa anaamini yuko kwenye hatari kubwa zaidi kuliko ilivyowahi kutokea.

Alisema: "Hivi karibuni nilipata taarifa kwamba watu wametumwa kutoka Swaziland kuja kunikamata, jambo ambalo hakika linanitisha mno. Kama nikirejea, nitakamatwa au mbaya zaidi huku pale kuna watu ambao wanateseka, kupigwa au kuuawa kwa kujihusisha na siasa."

Tintswalo sasa anaishi katika mashaka ya kuweza kurejea nchini Swaziland, baada ya ombi lake la kwanza la hifadhi ya kisiasa nchini Uingereza mwaka 2007 kukataliwa mwaka 2011.

Mwezi uliopita, alikamatwa na kupelekwa kwenye kituo cha kushikilia wahamiaji baada ya miezi 18 ya kuripoti kila wiki katika mamlaka hizo.
Hatahivyo, baada ya shinikizo kutoka TUC na ofisi ya Mbunge wa Birmingham kupitia chama cha Labour, Roger Godsiff, Tintswalo aliachiwa na sasa amekata rufaa wizara ya Mambo ya Ndani.

Godsiff alisema juzi: "Tumefurahishwa mno wanasheria walifanikiwa sana katika kuwezesha kutazamwa upya kwa kesi ya Ngobeni."

Baba huyo wa watoto 27, Mfalme Mswati III alikuwa mgeni kwenye harusi ya William na Kate na pia kwenye sherehe za Miaka 50 ya Malkia wakati wa majira ya joto mwaka jana.

Mke wa sita wa mfalme huyo alitoroka kutoka kwenye jumba hilo harimu mwaka jana, akielezea miaka kadhaa ya 'machungu na udhalilishaji wa kimwili' uliofanywa na mume wake.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani alikataa kuzungumzia chochote.

2 comments:

  1. GREETINGS everyone out there, i will never forget the help Dr Iruwa rendered to me in my marital life. i have been married for 5 years now and my husband and i love each other very dearly . after 3 years of our marriage my husband suddenly change he was having an affair with a lady outside,i notice it then i was praying for divine intervention the thing became more serious i told my pastor about it we prayed but nothing happen. my husband just came home one day he pick up his things and left me and the kids to his mistress outside at this time i was confuse not knowing what to do again because i have lost my husband and my marriage too. i was searching for help on the internet, i saw many people sharing testimony on how Dr Iruwa help them out with their marital problems so i contacted the email of Dr Iruwa i told him my problem and i was told to be calm that i have come to the right place were i can get back my husband within the next 24hours. He told me what went wrong with my husband and how it happen.that he will restored my marriage. to my greatest surprise my husband came to my office begging me on his knees that i should find a place in my heart to forgive him,that he will never cheat on me again. i quickly ask him up that i have forgiven him. Your case is not too hard why don't you give Dr Iruwa a try he work surprises because i know he will help you to fix your relationship with your ex partner. i thank god for using Dr Iruwa to save my marriage. People call Doctor Iruwa a nice man but i call him a God sent!Do you need help i will advice you to contact Dr with this information: website:www.superiorquickspellsolution.com Email: E-mail:iruwa567@gmail.com CALL:+27633647906

    ReplyDelete