NJOMBE

NJOMBE

Sunday, September 16, 2012

Papa Benedict ziarani nchini Lebanon

Maelfu ya watu walijipanga foleni siku ya Jumamosi kando kando mwa barabara za mji mkuu wa Lebanon, Beirut katika siku ya pili ya ziara ya kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Benedict wa kumi na sita

Umati huo ulipeperusha bendera za lebanon na vatican huku msafara wa magari ya Papa ukielekea katika ikulu ya rais wa nchi hiyo.
Papa alifanya mazungumzo na Michel Suleiman wa lebanon ambaye ndiye rais pekee mkristo katika eneo hilo la mashariki ya kati.
Wakati wa ziara hiyo papa alipongeza ushirikiano na utangamano miongoni mwa wakristo na waislamu nchini lebanon huku akishutumu watu walio na misimamo mikali ya kidini.

Ghasia zaidi mgodini Afrika Kusini

Polisi wa Afrika Kusini

Polisi wa Afrika Kusini
Kumekuwa na ghasia zaidi katika mgodi wa Marikana nchini Afrika Kusini ambako polisi wametumia gesi ya kutoa machozi na risasi za mpira kuwatawanya wafanyakazi wa mgodi huo ambao wamekuwa wakiandamana magharibi mwa mji mkuu wa Pretoria.
Polisi hao walivamia makazi ya wafanyakazi hao mapema asubuhi siku ya Jumamosi wakikamata silaha mbalimbali zikiwemo mapanga na mikuki.
Serikali ya Afrika Kusini imeapa kukomesha migomo katika machimbo ya migodi nchini humo.
Migomo hiyo imekuwa ikisambaa na kuendelea tangu polisi walipowaua wachimba migodi 34 katika mgodi wa Marikana hapo Agosti 16 mwaka huu.
Siku ya Ijumaa baraza la mawaziri lilitangaza kuwa halitavumilia kile walichokiita mikutano isiyo halali na kutishia kuwanyanganya silaha waandamanaji hao.

Moto

Wanaume kwa wanawake na watoto walitawanyika baada ya polisi waliokuwa wakisaidiwa na helikopta za jeshi zilizokuwa angani zikirusha risasi za mpira na gesi za kutoa machozi kwa waandamanaji.
Maombolezo wakati wa mazishi ya wachimba madini waliouawa
Picha za televisheni zilionyesha watu waliokua na majeraha yaliyochuruzika damu.
"Gari la polisi lilitupita, tulikuwa ni kundi la wanawake na watu wengine walikimbia. Nilisimama pale nikiangalia na walinipiga risasi mguuni," Melita Ramasedi aliliambia shirika la habari la Sapa.
Wakati polisi wakiwasili katika eneo hilo waandamanaji walitumia matairi yaliyowashwa moto kuzuia polisi hao kuingia katika eneo hilo, ripoti zinasema.
Mapema polisi 500 walifanya uvamizi wa makazi ya wafanyakazi hao mapema asubuhi wakikamata silaha mabalimbali, msemaji wa polisi Thulani Ngubane amesema.
Ameliambia shirika la habari la AFP kuwa polisi waliwakamata watu 12 ingawaje watano kati yao ni kwa makosa ya kukutwa na madawa ya kulevya na sio silaha.
"Popote tutakapoana tabia kama hii ya vurugu na watu wakijichukulia sheria mikononi kwa kufanya maandamano yasiyo halali, hakika tutachukua hatua," alisema.
"Polisi hawatasita kuchukua hatua. Tutachukua hatua kama ambavyo tumekwisha anza na tutaendelea kufanya hivyo."
Maandamano hayo yameshuhudia mamia ya wafanyakazi wakiwa na fimbo na mapanga wakipita kutoka mgodi mmoja hadi mwingine eneo la Marikana na maeneo mengine na kutishia yeyote atakayerejea kazini.

Malipo yakataliwa

Wafanyakazi hao wamekuwa wakidai nyongeza ya mishahara kufikia randi 12,500 kwa mwezi (sawa na pauni 930 au dola za kimarekani 1,500) kutoka kiwango cha sasa cha kati ya randi 4,000 hadi 5,000.
Mapambano kati ya polisi na waandamanaji hivi Karibuni
Mapambano kati ya polisi na waandamanaji
Siku ya Ijumaa wafanyakazi hao walikataa ahadi ya nyongeza ndogo ya mishahara, ya randi 1,000 kwa mwezi, iliyotolewa na mwajiri wao kampuni ya Lonmin,wakisema kuwa ni sawa na kuwatukana.
Tokea vifo vya mwezi Agosti katika mgodi wa Marikana, migomo imekuwa ikisambaa katika maeneo mengine ya migodi nchini Afrika Kusini.
Waziri wa fedha Pravin Gordhan ameonya kuwa migomo hiyo inaweza kuathiri ukuaji uchumi, ajira na imani ya wawekezaji katika nchi hiyo yenye uchumi mkubwa barani Afrika.
Baadhi ya vyama vya wafanyakazi vimetishia kuitisha mgomo mkubwa.

Magharibi: komesheni maandamano

Waandamanaji walipowasha moto katika ubalozi wa Marekani mjini Tunis, Tunisia
Waandamanaji walipowasha moto mkubwa katika ubalozi wa Marekani mjini Tunis, Tunisia
Mataifa ya nchi za magharibi yametaka kukomeshwa kwa maandamano yenye lengo ya kushambulia balozi za nchi hizo kupinga filamu inayomdhalilisha mtume Muhammad iliyotengenezwa nchini Marekani.
Jumuiya ya Ulaya imewataka viongozi wa nchi za Kiarabu na nchi nyingine za kiislamu kuacha maandamano na kudumisha amani.
Marekani inatuma wanajeshi wake kulinda ubalozi wake ulioko Khartoum nchini Sudan ikiiasa pia Sudan kulinda balozi za kigeni nchini humo.
Watu wasiopungua saba waliuawa katika maandamano ya ghasia mjini Khartoum, Tunis na Cairo siku ya Ijumaa, na kuna wasiwasi wa kutokea maandamano zaidi.
Wanajeshi wa Marekani walipelekwa pia nchini Libya siku ya Jumatano baada ya balozi wa Marekani nchini Libya na Wamarekani wengine watatu kuuawa pia nchini Yemen siku ya Ijumaa baada ya ghasia za maandamano mjini Sanaa.
Nchini Afghanistan, wapiganaji wa Taliban wamesema pia wameshambulia moja ya kambi kubwa za vikosi vya kimataifa nchini humo ya Bastion ambapo wanajeshi wawili wa Marekani waliuawa.
Wapiganaji hao wanadai kufanya shambulio hilo kulipiza kisasi kupinga filamu hiyo ya kuukashifu uislamu.
Waandamanaji wakipinga filamu hiyo mjini Sydney Australia siku ya Jumamosi, 15 Septemba 2012
Waandamanaji wakipinga filamu hiyo mjini Sydney Australia siku ya Jumamosi, 15 Septemba 2012


Balozi za Ujerumani na Uingereza nchini Sudan pia zilishambuliwa ingawaje uhusiano juu ya filamu hiyo na nchi hizo haujafahamika.
Siku ya Ijumaa rais wa Marekani Barack Obama na Waziri wa mambo ya nchi za nje Hillary Clinton walihudhuria mapokezi ya kurejeshwa Wamarekani waliouawa mjini Benghazi nchini Libya.
Bwana Obama alisema kuwa Marekani itakabiliana vilivyo dhidi ya mashambulizi yoyote kwa balozi zake nchi za nje.
Maandamano zaidi yameripotiwa kuenea zaidi hadi nchini Australia ambapo polisi walipambana na mamia ya waislamu katika mitaa ya jiji la Sydney.
Polisi hao walitumia gesi ya kutoa machozi na mbwa kujaribu kuwasambaratisha waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe na miti.

Mtengenezaji ahojiwa

Wakati huohuo mmoja wa watu wanaoshukiwa kuhusika na utengenezaji wa filamu hiyo inayolalamikiwa kuukashifu Uislamu, amehojiwa na maafisa wa polisi mjini Los Angels nchini Marekani.
Wanataka kujua iwapo alikiuka masharti ya msamaha wa parole aliokuwa amepewa kufuatia adhabu ya kifungo kwa makosa ya kughushi.
Aliadhibiwa adhabu ya kifungo jela mwaka 2010 kwa kughushi kujipatia fedha benki na baadaye alipewa msamaha wa masharti.
Adhabu hiyo pia ilimpiga marufuku kutumia vifaa vya kompyuta na intaneti.

Rais wa Gambia asitisha hukumu ya kifo

Rais wa Gambia Yahya Jammeh

Rais wa Gambia Yahya Jammeh
Rais wa Gambia Yahya Jammeh, amesitisha utekelezaji wa adhabu ya kifo kwa wafungwa waliohukumiwa dhabu hiyo.
Ofisi ya rais huyo imesema hatua hiyo inafuatia wito wa kimataifa uliotaka adhabu hiyo ikomeshwe lakini ameonya kuwa usitishaji huo ni wa muda.
''Hatua itakayofuata itatategemeana na iwapo kiwango cha uhalifu kitapungua ambako usitishaji huo utakuwa wa moja kwa moja, na iwapo uhalifu utaongezeka basi hukumu hizo zitatekelezwa,'' taarifa ya rais huyo imesema, kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters.
Kiongozi huyo wa Gambia alikosolewa na jumuiya ya kimataifa mwezi uliopita alipotangaza kutekeleza adhabu ya kifo kwa wafungwa.
Wafungwa tisa waliuawa kwa kupigwa risasi kufuatia uamuzi wa rais huyo huku wengine 37 wakibakia katika orodha ya wafungwa waliohukumiwa adhabu ya kifo.
Rais huyo alisema kuwa wafungwa wote arobaini na saba waliohukumiwa adhabu ya kifo wangekuwa wamekwishauawa kufikia katikati ya mwezi Septemba mwaka huu.
Utekelezaji huo wa hukumu ya kifo ulikuwa ni wa kwanza nchini Gambia iliyo maarufu kwa watalii, katika kipindi cha miaka 27, huku wanaharakati wa haki za binadamu wakisema kuwa wengi wa wafungwa hao ni wale wa kisiasa.
Umoja wa Afrika na mashirika ya kutetea haki za binadamu walipinga adhabu hiyo.
Benin ambayo ni mwenyekiti wa sasa wa Umoja wa Afrika ilimtuma waziri wake wa mambo ya nje kwenda nchini Gambia kumuonya Bwana Jammeh kuacha kutekeleza adhabu ya kifo kwa wafungwa hao.
Siku ya Ijumaa kundi la Upinzani la Gambia liliiambia BBC kuwa lina mpango wa kuanzisha serikali likiwa uhamishoni katika nchi jirani ya Senegal katika kipindi cha siku chache zijazo.
Lengo la kundi hilo la National Transitional Council of The Gambia (CNTG) ni kuona linamaliza utawala wa ki-dikteta wa rais Yahya Jammeh.
Hukumu ya kifo ilifutwa wakati wa utawala wa rais wa zamani wa nchi hiyo Dawda Jawara lakini ikarejeshwa tena muda mfupi baada ya rais Jammeh kunyakua madaraka mwaka 1994.

Friday, September 14, 2012

Muingereza akamatwa Uganda kwa Ushoga


Msanii moja toka Uingereza amekamatwa nchini Uganda kwa madia ya kuandaa na kuonyesha mchezo wa kuigiza kuhusu ushuga.
David Cecil katika mahakama ya Makindye
Polisi wanasema kuwa Muingereza huyo alionyesha mchezo huo wa kuigiza licha ya kwamba Uganda ilipiga marufuku kwa muda onyesho hilo.
Mtayarishi David Cecil wa Uingereza alifikishwa katika mahakama moja mjini Kampala na kushitakiwa kwa madia ya kukaidi na kupuuza amri ya serikali.
Mahakama hiyo iliambiwa kuwa Bwana Cecil alionyesha mchezo huo kwa jina "The river and the mountain" katika ukumbi wa Tilapia Cultural Center taraehe 17 Agosti na pia katika ukumbi mwengine wa Mish Mash Cultural Center tarehe 26 Agosti mjini Kampala.
Mahakama hiyo ya Kampala ilikataa kuamuachilia Muingereza huyo kwa dhamana na badala yake kuagiza awekwe katika gereza la Luzira hadi siku ya jumatatu ,Septemba 17 ambapo kesi yake inatarajiwa kuendelea.

Washukiwa wa mashambulizi wakamatwa Libya


Kundi linaloshukiwa kuafnya mashambulizi mjini Benghazi
Maafisa nchini Libya wamewakamata washukiwa kadhaa wa machafuko yaliyosababisha kifo cha balozi wa Marekani nchini humo pamoja maafisa wengine wanne wa ubalozi huo mjini Benghazi.
Waziri mkuu mpya wa Libya Mustafa Abu Shaqur aliambia BBC kuwa uchunguzi unaoendelea kuhusiana na kisa hicho unaonekana kufanikiwa.
Shambulizi lilifanyika siku ya Jumanne wakati wa maandamano yaliyopinga filamu iliyotengezwa nchini Marekani kumkejeli Mtume Mohammed.
Maandamano sawa na hayo yamesambaa katika nchi za kiarabu na mataifa ya Kaskazini mwa Afrika.
Maandamano zaidi yanatarajiwa kufanyika baada ya maombi ya Ijumaa
Makabiliano kati ya polisi wa kupambana na ghasia pamoja na waandamanaji yameendelea usiku kucha katika mji mkuu wa Misri, Cairo ambako makundi ya wapiganaji wa kiisilamu pamoja na watu wengine waliitisha maandamano ya amani ya watu milioni moja baadaye leo Ijumaa.
Hapo jana kulizuka ghasia zaidi nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kati ya polisi na waandamanaji wanaokashifu filamu ambayo wanasema kuwa inakejeli imani ya Kiislamu.
Runinga ya Misri ilionyesha gari likiteketezwa moto na watu wengine wakikimbia vitoza machozi.
Waandamanaji walitaka kufukuzwa kwa balozi wa Marekani nchini humo huku polisi wakiwafyatulia mabomu ya kutoa machozi waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
Nchini Yemen waandamanaji walivamia ubalozi wa Marekani wakichoma moto magari kabla ya vikosi vya ulinzi kuwadhibiti kwa kuwafukuza kutoka eneo hilo.
Maandamano zaidi pia yamefanyika katika nchi za Tunisia, Morocco, Sudan, Mauritania na Iran.
Wakati huohuo maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .
Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .
Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.
Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .
Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.
Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.
Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika

Washukiwa wa mashambulizi wakamatwa Libya

 

Kundi linaloshukiwa kuafnya mashambulizi mjini Benghazi
Maafisa nchini Libya wamewakamata washukiwa kadhaa wa machafuko yaliyosababisha kifo cha balozi wa Marekani nchini humo pamoja maafisa wengine wanne wa ubalozi huo mjini Benghazi.
Waziri mkuu mpya wa Libya Mustafa Abu Shaqur aliambia BBC kuwa uchunguzi unaoendelea kuhusiana na kisa hicho unaonekana kufanikiwa.
Shambulizi lilifanyika siku ya Jumanne wakati wa maandamano yaliyopinga filamu iliyotengezwa nchini Marekani kumkejeli Mtume Mohammed.
Maandamano sawa na hayo yamesambaa katika nchi za kiarabu na mataifa ya Kaskazini mwa Afrika.
Maandamano zaidi yanatarajiwa kufanyika baada ya maombi ya Ijumaa
Makabiliano kati ya polisi wa kupambana na ghasia pamoja na waandamanaji yameendelea usiku kucha katika mji mkuu wa Misri, Cairo ambako makundi ya wapiganaji wa kiisilamu pamoja na watu wengine waliitisha maandamano ya amani ya watu milioni moja baadaye leo Ijumaa.
Hapo jana kulizuka ghasia zaidi nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kati ya polisi na waandamanaji wanaokashifu filamu ambayo wanasema kuwa inakejeli imani ya Kiislamu.
Runinga ya Misri ilionyesha gari likiteketezwa moto na watu wengine wakikimbia vitoza machozi.
Waandamanaji walitaka kufukuzwa kwa balozi wa Marekani nchini humo huku polisi wakiwafyatulia mabomu ya kutoa machozi waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
Nchini Yemen waandamanaji walivamia ubalozi wa Marekani wakichoma moto magari kabla ya vikosi vya ulinzi kuwadhibiti kwa kuwafukuza kutoka eneo hilo.
Maandamano zaidi pia yamefanyika katika nchi za Tunisia, Morocco, Sudan, Mauritania na Iran.
Wakati huohuo maafisa wa Marekani wanasema serikali ya nchi hiyo inachunguza ikiwa mashambulio ya jumanne kwenye ubalozi wa Marekani katika mji wa Libya wa Benghazi yalikuwa ni ya kupangwa au la .
Balozi wa Marekani nchini Libya , Christopher Stevens, aliuawa .
Maafisa wa Marekani wameelezea mashambulio hayo kama yenye utata na yenye kupangwa kitaalamu na kuna tetesi kwamba makundi ya jihad huenda yalihusika .
Awali ilifikiriwa kuwa mashambulio hayo yalikuwa na uhusiano na maandamano ya kupinga filamu iliyokuwa inamkejeli Mtume Mohammed.
Takriban waandamanaji mia mbili wamekusanyika karibu na ubalozi wa Marekani mjini Cairo Misri kwa usiku wa pili kuelezea hasira yao juu ya filamu hiyo .
Aliyekuwa balozi wa Marekani nchini Libya Christopher Stevens
Awali waandamanaji walirusha mawe kwenye ubalozi huo na vikosi vya usalama vikafyatua mabomu ya kutoa machozi kuwa tawanya.
Watu wenye silaha waliokuwa na maguruneti walichomo moto jengo la ubalozi na walioshuhudia wanasema watu hao walizingira eneo hilo.
Rais Obama amelaani vikali shambulio hilo na ameahidi kushirikiana na serikali ya Libya kuwafikisha mbele ya sheria wahusika

Thursday, September 13, 2012

Malema awashauri wanajeshi kudai haki zao

Mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini Julius Malema, amewashauri wanajeshi wenye manung'uniko kujipanga vyema na kupigania kazi zao.
Malema aliyatoa matamshi hayo kwa wanajeshi wanaokabiliwa na makosa ya kinidhamu yaliyotokana na maandamano waliyoyafanya mwaka 2009 wakidai mishahara mizuri na mazingira bora ya kazi.
Kambi za jeshi leo ziliwekwa katika hali ya tahadhari kabla ya hotuba yake kwa wanajeshi hao, ikiwa ndio mara ya kwanza hatua kama hii kuchukuliwa tangu kumalizika kwa enzi ya ubaguzi wa rangi.
Bwana Malema ni mwanasiasa anayeibua mgawanyiko hapa. Hivi maajuzi alifukuzwa kutoka chama cha ANC na kwa sasa anafanyiwa uchunguzi kuhusiana na kashfa ya ufisadi.
Lakini hajaondoka ANC kimya kimya. Badala yake ametumia mauaji ya hivi maajuzi katika mgodi wa Marikana kuanzisha kampeni kali dhidi ya mabepari nchini Afrika Kusini na kutaka yafanyike mapinduzi ya kiuchumi.
Wengi wanamshutumu kwa kuhusika na ubinafsi mbaya wa kisiasa, lakini malema anapokea uungwaji mkubwa kutoka kwa jamii za watu maskini na kimya cha serikali ni ishara tosha kuwa imeshindwa kukabiliana naye.
Manung'uniko ya wanajeshi ni fursa nyingine kwa Malema kuonyesha ubabe wake na hali ni tete nchini Afrika Kusini.
Hofu iliyopo ni kwamba migomo huenda ikaenea zaidi na kwamba serikali kwa sasa inazingirwa na migogoro ya ndani huku baadhi ya mirengo serikalini ikipanga njama ya kumtimua madarakani rais Jacob Zuma.

Rais wa Somalia anusurika shambulizi

Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud , amenusurika jaribio la kumuua mjini Mogadishu.
Milipuko miwili imetokea nje la lango la makao ya rais huyo katika hoteli ya Al-Jazeera wakati rais huyo alipokuwa anajiandaa kufanya mkutano na waandishi wa habari.
Taarifa zinasema kuwa waziri wa mambo ya nje wa Kenya Sam Ongeri pia alikuwa katika hoteli hiyo wakati wa shambulizi. Hata hivyo wawili hao wamenusurika. Inaarifiwa watu wanne wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa.

Balozi wa Marekani auawa Libya


Balozi J Christopher Stevens
Balozi wa Marekani nchini Libya ameuawa baada ya kushambuliwa na watu waliokuwa wamejihami na kuvamia ubalozi wa Marekani Mashariki mwa mji wa Benghazi. Balozi J Christopher Stevens, ni miongoni mwa maafisa wengine wa ubalozi waliouawa kufuatia maandamano kuhusu filamu iliyotolewa nchini humo ikimkejeli Mtume Muhammad.
Idara ya mambo ya ndani nchini Marekani, imethibitisha tu kifo cha afisaa mmoja wa ubalozi huo ingawa bado haijataja jina lake.
Maandamano ya kupinga filamu hiyo pia yalifanyika mjini Cairo dhidi ya ubalozi wa Marekani.
Wakati huohuo, waziri wa mambo ya nje wa Marekani Bi. Hilary Clinton, amelaani mashambulizi hayo.
Serikali ya Libya imetaja shambulio hilo kama kitendo cha uoga.
Ubalozi huo uliteketezwa na watu waliojihami kwa bunduki kulalamikia filamu moja iliyotengenezewa nchini Marekani ambayo wanasema inamdhihaki Mtume Mohammed.
Wanamgambo hao wanaoripotiwa kuwa na ufungamano na kundi la waislamu wenye msimamo mkali walitumia maguruneti ya kurushwa kwa roketi kuvamia ubalozi huo kabla ya kuiteketeza. Maafisa wa Libya wameiambia BBC kwamba hali imetulia kwa sasa.
Machafuko hayo ya Libya yalijiri saa kadhaa baada ya maelfu ya waandamanaji kukusanyika nje ya ubalozi wa Marekani mjini Cairo kuelezea hasira zao kuhusu filamu hiyo kumhusu Mtume Mohammed.
Kwa wakati mmoja waandamanaji hao waliingia ndani ya ubalozi huo na kuichana bendera ya Marekani na kurejesha yao.

Wednesday, September 12, 2012

Simba Mabingwa wa Ngao ya Hisani wamlamba Azam

Nahodha wa Simba Juma Kaseja ikipokea na kuinuwa juu Ngao ya Hisani toka kwa Mgeni rasmi Mh Makongoro Mahanga
Habari na picha katika michezo


Ulinzi waimarishwa Tana River, Kenya

Moja ya vijiji vilivyoathirika
Usalama umeimarishwa katika eneo la Tana River baada ya siku mbili za mashambulizi ya kulipiza kisasi kati ya jamii za Pokomo na Orma.
Watu arobaini na wawili walifariki katika mashambulizi ya hapo jana ambapo zaidi ya watu miatatu walishambulia vijiji vinne.
Hapo jana wabunge kutoka eneo hilo waliwasilisha hoja bungeni ya kutaka wanajeshi zaidi kupelekwa katika eneo hilo ili kuimarisha usalama na kusitisha makabiliano ya kikabila.
Waziri mkuu Raila Odinga alisema kuwa mauaji hayo huenda yakatafsiriwa kwa misingi ya mkataba wa Roma.
''Mashambulizi haya yamepangwa na yamekuwa yakiendelea kwa muda. Hili sio tukio la ghafla bali limepangwa kwa umaakini mkubwa na kisha kutekelezwa.'' alisema waziri mkuu. ''Ni makosa yanayoweza kupelekwa katika mahakama ya kimaitaifa ya uhalifu wa kivita'', alisema Raila.
Wabunge wa eneo hilo waliowasilisha hoja hiyo wanataka mkutano na rais Mwai Kibaki kuhusu mgogoro unaoendelea huko.
Hali ya kibinadamu katika eneo hilo inasemekana kuzorota kila kukicha ingawa shirika la Red Cross na mashirika mengine ya kijamii yanatoa misaada kwa waathiriwa.
Mnamo siku ya Jumatatu, watu 38 waliuawa katika mapigano mapya yaliyozuka katika eneo hilo siku tatu tu baada ya watu 12 wa kabila la Pokomo kuuawa katika mashambulizi yaliyofanya na jamii hasimu ya Orma.
Polisi 11 ni miongoni mwa waliouawa katika makabiliano hayo.
Kulingana na Red Cross, nyumba ziliteketezwa moto baada ya kijiji kimoja kuvamiwa.
Tukio hilo linajiri baada ya mashambulizi mengine kutokea kwenye eneo hilo la Tana River na kusababisha vifo vya karibu watu kumi na saba.
Polisi kwa usihirikiano na shirika la msalaba mwekundu waliweza kuokoa manusura. Inaarifiwa watu wameanza kuhama eneo hilo la Tana River kukimbilia usalama wao.
Mwezi jana zaidi ya watu 50 waliuawa katika mapigano mengine kati ya jamii za Pokomo na Orma.
Hizi ni ghasia mbaya zaidi kushuhudiwa hivi karibuni tangu zile za mwaka 2007 kufuatia uchaguzi uliozua utata mkubwa.
Jamii ya wapokomo ambao ni wakulima wanaoishi katika eneo la mto Tana huzozana mara kwa mara na jamii ya wafugaji ya Orma chanzo kikiwa malisho na maji.Lakini wadadisi wanasema sio mzozo kuhusu malisho ndio unasababisha mashambulizi haya bali huenda yamechochewa kisiasa.
Serikali ya Kenya imelaumiwa sana kwa kujikokota katika kuchukua hatua za kusitisha mashambulizi haya ya kulipiza kisasi ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda mrefu huko Tana River.
Wito umetolewa wa kuwapokonya silaha makundi ya watu waliojihami ili kukomesha mashambulizi hayo.

Marekani yaadhimisha mashambulizi ya 9/11


Nchini Marekani,maadhimisho ya miaka kumi na moja tangu kutokea kwa mashambulio ya 9/11 mjini New York na katika makao makuu ya idara ya ulinzi ya Pentagon mwaka wa elfu mbili na moja yanafanyika.
Kwa mara ya kwanza hakutakuwepo na hotuba yoyote wakati wa sherehe hizo kutoka kwa wanasiasa.
Familia za zaidi ya watu elfu mbili mia saba waliouawa zitaruhisiwa kufika katika eneo la tukio la mashambulizi hayo maarufu kama Ground Zero mjini New York,.
Awali idara ya afya nchini Marekani ilitangaza kuwa manusura wa mashambulio hayo na wale waliowasaidia watapewa uchunguzi na matibabu ya takriban aina hamsini za saratani bila malipo, kwa sababu walivuta hewa iliyokuwa na sumu baada ya mashambulio hayo.

Malema aitisha mgomo wa kitaifa wa wachimba migodi

Mwanaharakati wa kisiasa nchini Afrika Kusini Julius Malema ametoa wito wa maandamano makubwa ya kitaifa nchini humo kwa wafanyakazi wa migodini.
"wamekuwa wakiiba madini haya ya dhahabu kutoka kwenu." bwana Malema aliambia wachimba migodi waliokuwa wanamshangilia katika mgodi mmoja wa dhahabu mashariki mwa Johannesburg.
"sasa ni wakati wenu." aliongeza Malema.
Migomo migodi ya wachimba migodi imekumba Afrika Kusini na kuathri shughuli za kuchimba madini ya Platinum na dhahabu katika nchi hiyo yenye rasilimali nyingi.
Lakini baadhi wanamtuhumu Malema kwa kuwa na njama na kujinufaisha kisiasa huku wengi wakiwa bado wanaomboleza vifo vya wachimba migodi 34 wa Marikana mwezi jana nchini humo.
Watu 44 walifariki katika mgodi huo katikati ya mwezi Agosti. 34 wakipigwa risasi na kuuawa na polisi kwa siku moja.
Tume ilibuniwa na serikali kuchunguza matukio katika mgodi huo.
Wadadisi wanasema kuwa kuangazia baadhi ya mambo yanayohusu chama cha ANC kama uhusiano wake na biashara kubwa kubwa pamoja na kupuuza wananchi wafanyakazi ambao wamekuwa daima wakiunga mkono chama hicho bila shaka ni mwiba kwa chama tawala.
"lazima mgomo wa kitaifa ufanyike," Malema aliwaambia wafanyakazi wanaogoma katika machimbo ya dahahabu ya KDC.
''Yametosha! Tumesubiri miaka mingi kunufaika na madini haya. Lazima sasa mfaidike na nyiyi kutokana na dhahabu hii.'' alisema Malema.
Wakati akitoa hotuba yake, Malema alishangiliwa sana watu wakipiga firimbi na mbinja pamoja na kupuliza vuvuzela.
Malema alifurushwa kutoka chama tawala ANC na angali anachunguzwa kwa madai ya ufisadi . Lakini anaendelea kuzua hisia miongoni mwa umma hasa kufuatia mauaji ya wachimba migodi mwezi jana.

Ubalozi wa Marekani wateketezwa Libya

Afisa mmoja wa ubalozi wa Marekani ameuawa na wengine wamejeruhiwa wakati kundi la watu waliojihami na silaha walipovamia jengo hilo mjini Benghazi.
cairo protests
Maandamano pia yamefanyika mjini Cairo, Misri
Inaaminika kuwa watu hao walikuwa wanaandamana kulaani filamu mmoja iliotengenezwa nchini Marekani ambayo wanasema inamkejeli Mtume Mohammed.
Jengo hilo liliteketezwa kabisa na wandamanaji hao waliokuwa na hasira.
Maandamano hayo yalichochea makabiliano kati ya vikosi vya serikali na kundi la wanamgambo maarufu kama Ansar al Sharia brigade, mjini Benghazi.
Msemaji wa serikali ya Marekani, amelaani kitendo hicho na ameongeza kuwa wanashirikiana na idara ya usalama nchini Libya kuimarisha usalama kwenye balozi zake.
Taarifa zinasema kuwa wakaazi wa mji mkuu Tripoli, wamekuwa wakishawishiwa kupitia ujumbe kwenye tovuti za kijamii wafanye maandamano lakini hakuna aliyejitokeza.
Sehemu ya filamu hiyo inasambazwa kupitia mtandao wa Youtube kwa lugha ya kiarabu.
Maandamano sawa na hayo pia yamefanyika mjini Cairo nchini Misri. Kundi lingine la watu limeingia kwenye ubalozi wa Marekani na kuteketeza bendera ya nchi hiyo.
Taarifa kutoka Cairo zinasema, maelfu ya Waislamu na Wakristo wameungana kulaani filamu hiyo. Hata hivyo hakuna aliyejeruhiwa kwenye maandamano hayo yaliofanyika Misri.

Waandishi waandamana kimya kimya Tanzania


Ramani ya Tanzania
Waandishi wa habari nchini Tanzania hii leo walifanya maandamano ya kimya kimya kulaani kuuawa kwa mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi.
Kwa upande wa jiji la Dar es Salaam ambalo ndilo lenye idadi kubwa ya waandishi nchini, maandamano hayo yalianza katika kituo cha runinga cha Chanel Ten na kumalizikia katika uwanja wa jangwani.
Akiwahutubia waandishi wa habari waliohudhuria maandamano hayo, Nevil Meena ambaye ni katibu mkuu wa jukwaa la wahariri nchini Tanzania amesema lengo la kufanya maandamano ni kutumia njia wanazotumia watanzania wengine kueleza kero lao.
Hapo jana chama cha Upinzani nchini Tanzania Chadema, kilimtaka rais Jakaya Kikwete kuunda tume ya kimahakama itakayochunguza kifo cha mwandishi huyo kwa madai kwamba hawana imani na kamati iliyoundwa na waziri wa mambo ya ndani kwa maelezo kuwa haina mamlaka ya kisheria.
Huku mazingira yaliyopelekea kifo cha mwandishi wa habari Daudi Mwangosi yakiwa bado yamegubikwa na utata, chama cha Demokrasia na maendeleo kimewataka waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi na mkuu wa jeshi la polisi Said Mwema kuachia ngazi mara moja kama njia ya kuwajibika.
 Mwenyekiti wa chama cha Chadema Freeman Mbowe, amesema kuwa Chadema haina imani na kamati iliyoundwa na waziri Nchimbi kwa madai kwamba imekosa mamlaka ya kisheria.
Hivyo amemtaka rais Jakaya Kikwete aunde tume ya kimahakama itakayochunguza kifo cha mwandishi huyo na kwamba, iwapo hayo hayatatekelezwa, chama hicho kitafanya maandamano makubwa.
Katibu mkuu wa jukwaa la wahariri nchini Tanzania, Nevil Meena alisema kuwa tukio la kuuawa kwa mwandishi huyo wa habari marehemu Daudi Mwangosi tarehe mbili mwezi huu katika kijiji cha Nyololo huko mkoani Iringa, kumeibua hisia kali miongoni mwa waandishi wa habari pamoja na wanaharakati huku wengi wao wakihoji usalama wa waandishi wanapokuwa kazini hasa katika mazingira magumu.

Rwanda yahusishwa upya na uasi DRC



Wanachi wakipinga vita Mashariki mwa DRC
Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch, linasema kuwa lina ushahidi mpya kuonyesha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu uliofanywa na waasi wa M23 kwa usaidizi wa wanajeshi wa Rwanda.
Shirika hilo linasema limefanya mahojiano na watu 190, walioshuhudua matukio hayo Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Utafiti wa shirika hilo unasema kuwa waasi wa M23 waliwasajili vijana wadogo na wanaume jeshini.
33 kati ya wale waliosajiliwa, wamesemekana kuuawa walipojaribu kutoroka. Baadhi walifungwa kamba na kupigwa risasi , hatua hiyo ikisemekana kuwa mfano wa adhabu itakayotolewa kwa watakaojaribu kutoroka.
Jamii ya kimataifa ilisitisha msaada kwa Rwanda baada ya madai ya jeshi la Rwanda kusaidia waasi hao ingawa baadaye msaada ulianza kutolea tena pale Uingereza iliposema kuwa imeweza kuzungumza na Rwanda kuhusu swala hilo.
Shirika hili linasema liliwahoji familia za waathiriwa wanyarwanda, maafisa wa utawala pamoja na wapiganaji wa zamani wa kundi la M23 kati ya mwezi Mei na Septemba.
Kwa mujibu wa afisaa mkuu wa utafiti,Anneke Van Woudenberg, waasi wa M23 wanafanya visa vya kuogofya vya ukiukwaji wa haki za binadamu, Mashariki mwa Congo.
Moja ya visa walivyodokezewa watafiti wa HRW, ni kile cha mwanamke mwenye umri wa miaka 32 aliyesema kuwa waasi wallivunja mlango wake na kumpiga mtoto wake mwenye umri wa miaka 15 hadi kufariki na kisha kumteka nyara mumewe. Kabla ya kuondoka waasi hao walimbaka kila mmoja kwa zamu, na kisha kumwagia mafuta taa kwenye miguu yake na kuiteketeza. Aliokolewa na jirani zake baada ya waasi hao kuondoka.
HRW imetoa wito kwa jamii ya kimataifa kuwachukulia hatua waasi wa M23 huku akipendekeza maafisa wa Rwanda waliohusika na vita hivyo kufunguliwa mashtaka kwa kusaidia waasi hao kukiuka haki za binadamu pamoja na kutoa mafunzo, silaha na zana nzito za vita kwa waasi hao.
Hata hivyo serikali ya Rwanda imekuwa ikikana madai kuwa jeshi lake linahusika na uasi Mashariki mwa DRC.

Tuesday, September 11, 2012

Shinikizo za Chadema Tanzania

Ramani ya Tanzania
Chama cha upinzani nchini Tanzania cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimewataka waziri wa mambo ya ndani pamoja na mkuu wa jeshi la polisi kujiuzulu kufuatia mauaji ya mwandishi wa habari Daudi Mwangosi yaliyotokea wiki moja iliyopita huko mkoani Iringa.
Vilevile uongozi wa chama hicho umemtaka rais Jakaya Kikwete kuunda tume ya kimahakama itakayochunguza kifo hicho kwa madai kwamba hawana imani na kamati iliyoundwa na waziri wa mambo ya ndani kwa maelezo kuwa haina mamlaka ya kisheria.
                                            Marehemu Daudi Mwangosi enzi za uhai wake

Huku mazingira yaliyopelekea kifo cha mwandishi wa habari Daudi Mwangosi yakiwa bado yamegubikwa na utata, chama cha Demokrasia na maendeleo kimewataka waziri wa mambo ya ndani Emmanuel Nchimbi na mkuu wa jeshi la polisi Said Mwema kuachia ngazi mara moja kama njia ya kuwajibika.
Mwenyekiti wa chama cha Chadema Freeman Mbowe, amesema kuwa Chadema haina imani na kamati iliyoundwa na waziri Nchimbi kwa madai kwamba imekosa mamlaka ya kisheria.
Hivyo amemtaka rais Jakaya Kikwete aunde tume ya kimahakama itakayochunguza kifo cha mwandishi huyo na kwamba, iwapo hayo hayatatekelezwa, chama hicho kitafanya maandamano makubwa.
Kwa upande mwengine, waandishi wa habari nchini wamedhamiria kufanya maandamano ya kimya kimya nchi nzima hapo kesho kulaani kuuawa kwa mwandishi mwenzao. Maandamano hayo yanatarajiwa kufanyika katika mikoa yote kuanzia saa mbili asubuhi. Kwa upande wa Mkoa wa Dar es Salaam, yamepangwa kuanza katika kituo cha runinga cha Chanel Ten na kumalizikia katika viwanja wa mnazi mmoja.
Katibu mkuu wa jukwaa la wahariri nchini Tanzania, Nevil Meena amesema kuwa tukio la kuuawa kwa mwandishi huyo wa habari marehemu Daudi Mwangosi tarehe mbili mwezi huu katika kijiji cha Nyololo huko mkoani Iringa, kumeibua hisia kali miongoni mwa waandishi wa habari pamoja na wanaharakati huku wengi wao wakihoji usalama wa waandishi wanapokuwa kazini hasa katika mazingira magumu.
Mtaniwia radhi kwa picha hii ya kutisha.Hivi ndivyo Mwangosi alivyouwawa Iringa

Somalia yapata Rais mpya

 
Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud
Bunge la Somalia limemchagua Hassan Sheikh Mohamud kuwa Rais mpya wa nchi hiyo.
Kulikuwa na wagombea 22 kwenye uchaguzi huo, akiwemo Rais anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed na waziri mkuu Abdiweli Mohamed Ali.
Hassan Sheikh Mohamud alishinda kufuatia duru ya tatu ya upigaji kura, ambapo alikuwa anachuana na Rais anayeondoka Shariff Sheikh Ahmed.
Katika raundi ya kwanza Sheikh Ahmed alikuwa amepata ushindi mwembamba wa kura 64 dhidi ya 60 alizopata Sheikh Mohamud.
Kwa jumla wabunge 271 walipiga kura.
Katika duru ya mwisho wabunge wengi waliowaunga mkono wagombea waliochujwa walimuunga mkono Sheikh Mohamud , akapata kura 190 dhidi ya 70 alizopata Rais anayeondoka.
Hii ni mara ya kwanza kwa uchaguzi wa Rais kufanyika katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu, tangu kuondolewa kwa serikali ya kijeshi mwaka 1991

Ethiopia kuwaachilia wandishi wa kigeni


Martin Schibbye na Johan Persson
Ethiopia imewasamehe waandishi habari wawili raia wa Sweden waliofungwa jela nchini humo mwaka jana kwa madai ya kuunga mkono vitendo vya kigaidi.
Wawili hao wanatarajiwa kuachiliwa baadaye wiki hii
Martin Schibbye na Johan Persson walikuwa wanahudumia kifungo cha miaka 11 baada ya kukamatwa mwaka jana mwezi wa saba na waasi mashariki mwa Ethiopia.
Duru za serikali zilisema kuwa waandishi hao walisamehewa na hayati Meles Zenawi kabla ya kifo chake mwezi jana.
Wamekuwa wakidai kuwa walikuwa tu nchini Ethiopia kikazi.
Schibbye na Persson, waliomba kuachiliwa baada ya hukumu yao mwaka jana kwa madai ya kuunga mkono kundi la wapiganaji la Ogaden (National Liberation Front (ONLF), ambalo Ethiopia inawaona kama kundi la kigaidi.
Afisaa mmoja wa serikali ambaye hakutaka kujulikana, alisema kuwa waandishi hao wataachiliwa wiki hii pamoja na wafungwa wengine 1,900.
Mwaka mpya wa Ethiopia ambapo wafungwa huachiliwa, utasherehekewa siku ya Jumanne.
Meles,ambaye alikuwa mamlakani kwa miaka 21 alifariki mwezi jana baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Serikali imesema kuwa naibu wake Hailemariam Desalegn, ataapishwa kuhudumu hadi uchaguzi mpya utakapofanyika mwaka 2015.

Monday, September 10, 2012

Maadhimio ya Kamati kuu ya Chadema



1.Uwajibikaji wa kisiasa wa viongozi wa serikali na idara zake.,Waziri Emmanuel Nchimbi,IGP Mwema,Paul Chagonja,RPC Morogoro na Kamanda wa FFU,na RPC IRINGA na Kamanda wa FFU wajiuzulu na au wafukuzwe kazi

2.RPC Morogoro na Iringa,makamanda wa FFU Morogoro na Iringa,na maaskari waliouwa wakamatwe mara moja na kufunguliwa mashitaka

3.Rais aunde tume huru ya uchunguzi wa vifo tata katika matukio ya kisiasa.1.ARUSHA vifo 3.IGUNGA,vifo vingi havijulikani bado,3.ARUMERU MASHARIKI,vifo 5, 4.SINGIDA kifo 1, MOROGORO na IRINGA
chadema haitatambua wala kushirikiana na kamati batili ya NCHIMBI.

4.Msajili wa vyama vya siasa John Tendwa ni mtu hatari kwa taifa kwa kauli tata anazozitoa.anashirikiana na au anajipendekeza kwa CCM na Serikali yake.CHADEMA tangu sasa haitafanya kazi na Tendwa wala kufanya mawasiliano naye ya kiofisi.Labda kama atagundua makosa yake na kuomba msamaha,chadema itatafakari namna ya kufanya naye kazi tena.

5.TBC TAIFA Television na Redio ni hatari kwa taifa,kwa kubobea kupotosha umma juu ya matukio mengi.Hivyo CHADEMA Inatangaza mgogoro na TBC na inaelekeza na kuomba wanachama ,wapenzi,na wananchi wote wapendao ukweli na haki,kuisusia TBC

6.Jeshi la Polisi lijue kuwa Maandamano ndiyo siasa yenyewe na mikutano ya hadhara ni lazima kwa mawasiliano ya umma na siasa.kuzuia vitu hivyo ni kunyima wananchi haki yao ya kikatiba ya uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni,pia kupata habari na taarifa

7.Operesheni MOVEMENT FOR CHANGE M4C,Inaendelea kadiri ya ratiba ilivyopangwa katika utaratibu uleule uliokuwepo awali.Inarejea Iringa Siku si nyingi.Na kamati kuu Imetoa msisitizo MAALUM kwa jimbo mojawapo singida,ambapo wamesema watatumia helcopita,magari,pikipiki na baiskeli na miguu,na badala ya kupita vijijini kama majimbo mengine,Chadema wanasema kwa sababu maalum katika jimbo hilo watapita kitongojikwa kitongoji,ili kufunza adabu baadhi ya viongozi (msisitizo ni wa msoma MAAZIMIO.jimbo hili laweza kuwa la Mwigullu Mchemba,kadiri ya wanahabari waliokuwepo)

8.Kutokana na mgogoro wa muda mrefu mkoani mwanza uliosababisha meye wa chadema kuvuliwa umeya kinyume na utaratibu na kwa njama za CCM na Serikali,na bahati mbaya sana kwa kushirikisha madiwani wa CHADEMA,KAMATI KUU imewavua UANACHAMA madiwani wake wawli 1 ADAMU CHAGULANI wa kata ya IGOMA na HENRY MATATA wa KITANGIRI, PIA uongozi wote wa CHADEMA mkoa wa mwanza Umevunjwa.
Imesomwa na Mwenyekiti CHADEMA Taifa

Hali mbaya ya wafungwa magerezani Chad

Ramani ya Chad
Wafungwa nchini Chad wanawekwa katika mazingira mabaya kiasi kuwa wanaotumikia kifungo wako katika hatari ya kufa jela.
Kulingana na shirika la Amnesty International, wafungwa wanawekwa katika magereza yaliyosongamana watu na kukosa hewa safi. Na yote hayo waliyashuhudia wakati walipotembelea magereza sita.
Ripoti ya shirika hilo imeelezea kisa kimoja ambapo wafungwa tisa walikufa gerezani baada ya kukosa hewa huku wengine saba wakiuawa kwa kupigwa risasi na walinzi.
Shirika hilo linasema kuwa wafungwa wanawake wanaishi katika hatari ya ubakaji na wengi wakiishi na watoto wao wenye hata miezi saba ndani ya magereza.
''Sio vyema wafungwa kuishi katika mazingira mabaya kama yale, mabaya sana kiasi cha mfungwa kuwa katika hatari ya kufia gerezani.'' alisema mtafiti mkuu wa shirika hilo Christian Mukosa.
"wafungwa wengi walikuwa na utapia mlo wakionekana wadhaifu sana. Baadhi walifungwa minyororo siku nzima wengi wakiugua maradhi ya ngozi, maradhi ya ngono, Malaria au Kifua kikuu" aliongeza Christian.
Shirika hilo limetoa wito kwa serikali kuchunguza madai hayo ya ukiukwaji wa haki za binadamu. Serikali ya Chad bado haijajibu ripoti hiyo ya Amnesty.

Jeshi la Mali lauwa wasafiri

Jeshi la Mali linasema kuwa limewapiga risasi na kuwauwa watu 16 katika jimbo la Segou, katikati mwa nchi, baada ya gari la watu hao kutosimama kwenye kituo cha ukaguzi.
Rais Dioncounda Traore wa Mali (kulia) na Waziri Mkuu Midibo Diarra
Wakuu wanasema gari hilo liliendelea hata baada ya kuonywa kwa risasi.
Inaarifiwa kuwa baadhi ya wale waliouwawa ni wahubiri wa Kiislamu kutoka Mauritania, ambao walikuwa wakielekea kwenye mkutano wa kidini nchini Mali.
Waandishi wa habari wanasema huenda kuwa jeshi liliwafikiria wasafiri hao kuwa wapiganaji wa Kiislamu ambao wanadhibiti eneo la kaskazini mwa Mali.

Somalia kupata rais Mpya

Wabunge wa Somalia
Wabunge 257 wa bunge jipya Somalia leo wanatarajiwa kumchagua rais wa nchi hiyo katika hatua ya hivi karibuni kuleta amani nchini humo.
Wabunge hao wapya wanakusanyika katika kituo cha mafunzo kwa polisi mjini Mogadishu kuanza kupiga kura.
Kamati ya uchaguzi imeidhinisha idadi ya wagombea 25 wa kiti hicho , akiwemo rais wa serikali ya mpito Sheikh Sharif sheikh Hassan na waziri mkuu Abdiweli Mohamed Ali.
Serikali ya mpito ambayo imedumu kwa muda wa miaka minane itakabidhi mamlaka kwa serikali mpya baada ya uchaguzi wa rais.
Rais wengi wa Somalia walilazimika kuikimbia nchi yao kufuatia hali mbaya ya usalama nchini Mwao.
Baadhi yao wanaoishi katika kambi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya wamekuwa na hisia mbali mbali kuhusu na mchakato wa kuleta amani na usalama pamoja na uthabiti unaoendelea nchini Somalia.
Mwandishi wa BBC mjini humo Daud Aweis anasema kuwa shughuli itachelewa kuhu wabunge wakipitia ukaguzi mkali kuhakikisha usalama wakati wa uchaguzi huo.
Ni Mara ya kwanza kwa miaka mingi kwa rais kuchaguliwa nchini Somalia ikiwa ni ishara ya usalama kuimarika.
Hata hivyo kundi la wapiganaji la al-Shabab, bado linadhibiti maeneo mengi ya kusini na katikati mwa Somalia.

Sunday, September 9, 2012

Wariri wa mambo ya Nje Mh.Bernard Membe ndani ya Mbamba Bey Mbinga

 Hivyo ndivyo anavyosema mwenyewe kupitia Tweeter Bado naendelea kuchati nae Nitakupa taarifa kulingana na sehemu alizopitia kutafuta ushahidi juu ya Ziwa Nyasa

Embedded image permalink
Mkutano wake  wa kwanza na Wazee wa Mbamba Bay unaofanyika pwani ya Ziwa Nyasa. Niko pamoja na Mbunge wa Mbinga na DC
Nimemaliza kuzungumza na Wazee wa Liuli, sasa naelekea Lituhi 

Waziri wa Kenya auziwa gari lililoibiwa

Waziri mmoja wa Kenya amekanusha kuwa amehusika na wizi wa gari moja la rais ambalo amekutwa nalo.
Rais Daniel Arap Moi
Waziri wa Serikali za Mitaa, Fred Gumo, alisema gari lake alikuwa amempa mfanya biashara alioko Mombasa na badala yake akakabidhiwa hilo gari, ambalo lilikuwa limeibiwa kutoka kwa rais wa zamani, Daniel Arap Moi, miaka mine iliyopita.
Bwana Gumo alisema hakujua kuwa gari hilo lilikuwa la kuibiwa.
Alisema hakulitumia sana kwa sababu hakupata nyaraka zote za gari hilo.

Wengi wauawa katika mapambano Sudan

Waasi wa Darfur wasema walivitimua vikosi vya serikali
Jeshi la Sudan na waasi wanasema wamekuwa katika mapambao tofauti mara mbili yaliyowaacha watu kadhaa kuuawa.
Jeshi linasema limewaua wapiganaji 32 walioshambulia kijiji magharibi mwa eneo la Darfur wakati waasi nao wakidai kuwa wamevitimua vikosi vya serikali kutoka eneo hilo.
Katika tukio tofauti Khartoum inasema kuwa waasi 45 wameuawa katika kijiji cha eneo la kusini la Kordofan, karibu na mpaka wa kusini wa Sudan.
Waasi wa Vuguvugu la Haki na Usawa (The Justice and Equality Movement-JEM) wamesema wamekiteka kijiji hicho huku wakiua askari mmoja.
Mwaka jana vikundi vya waasi katika majimbo mawili na pia katika jimbo la Blue Nile walianzisha muungano wenye lengo la kuiondoa serikali ya rais Omar al-Bashir.
Khartum inaishutumu Sudan Kusini kuwaunga mkono waasi hao.
Serikali mjini Juba inakanusha shutuma hizo ikiilaumu serikali ya Sudan kuyaunga mkono makundi ya waasi Sudan Kusini.
Mapigano ya hivi sasa yanakuja wakati Marekani ikiwa imetoa onyo kuhusu mgogoro unaoendelea wa mpaka kati ya Sudan na Sudan Kusini.
Onyo hilo lilitolewa na balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa, Susan Rice kufuatia mkutano wa Baraza la Usalama kujadii mgogoro huo.
Sudan Kusini imekubali pendekezo la suluhu ya mpaka lililotolewa na Umoja wa Afrika, lakini Sudan inakataa pendekezo hilo.
Tarehe ya mwisho ya Agosti 2 ya kufikia muafaka iliyokuwa imewekwa na Umoja wa Mataifa imeshindwa kuzaa matunda.
Hata hivyo pande zote mbili zinashinikizwa kuwa zimefikia makubaliano kabla ya tarehe mpya iliyowekwa ya Septemba 22.
Sudan na Sudan Kusini zimekuwa katika mgogoro kuhusu mpaka kati ya nchi hizo mbili na mapato ya uchimbaji mafuta.
Sudan Kusini ilipata uhuru kutoka Sudan mwaka jana, ikimaliza miaka mingi ya mapigano kati ya eneo la kaskazini linalokaliwa na Waislamu wengi na lile la kusini lenye Wakristo wengi na dini nyingine.

Nigeria yaua wapiganaji wa Boko Haram

Ulinzi eneo la Maiduguri kaskazini mwa Nigeria
Jeshi la Nigeria linasema limewaua watu saba wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa kundi la wapiganaji wa Kiisalmu wenye msimamo mkali la Boko Haram katika mapambano kaskazini mwa nchi hiyo.
Msemaji wa jeshi hilo amesema watu wengine zaidi kumi na watatu wamekamatwa baada ya kushambulia kituo cha ukaguzi cha jeshi, katika mji wa Maiduguri.
Ghasia hizo zimetokea siku moja baada ya polisi wa Nigeria, kusema kuwa wataanza kulinda kutwa-kucha, milingoti ya simu za mkononi kufuatia milingoti kadhaa kama hiyo kushambuliwa mwezi uliopita, kaskazini mwa nchi.
Boko Haram ilisema ilifanya mashambulio hayo, kwa sababu milingoti hiyo inatumiwa kufuatilia mawasilino baina ya wafuasi wake.
Akitoa maelezo ya tukio hilo la Maiduguri, Luteni Kanali Sagir Musa amesema, ''Kundi la watu wenye silaha wanaoshukiwa kuwa wafuasi wa Boko Haram walishambulia kituo cha ukaguzi cha kijeshi sehemu ambayo wanajeshi walikuwa wameweka kizuizi na kufanya ukaguzi.
Ramani ya Nigeria ikionyesha eneo la Maiduguri
''Wanajeshi walijibu shambulio hilo kwa risasi. Watu saba wenye silaha waliuawa katika majibizano hayo ya ufyatulianaji risasi, na wengine kumi na watatu walikamatwa huku wengine wakikimbia. Hakuna majeruhi waliopatikana kwa upande wa wanajeshi.''
Boko Haram wanataka kuwekwa kwa utawala wa sheria ya Kiislamu nchini Nigeria.
Kundi hilo lilianzisha kampeni ya kijeshi mwaka 2009 kupigania kuanzishwa kwa utawala wa Kiislamu, likishambulia majengo ya serikali na makanisa na pia kuwaua wahubiri wa Kiislamu wenye msimamo wa kati.
Nchi hiyo imegawanyika kati ya eno la kaskazini lenye Waislamu wengi na lile la kusini linalokaliwa na Wakristo wengi na dini nyingine.

Saturday, September 8, 2012

Kanisa la Anglikana lataka kuwa na rais

Askofu Mkuu wa kanisa la Anglikana, Rowan Williams, amefichua kuwa kanisa hilo linaandaa mpango wa kumteua rais wa kanisa, ambaye atabeba sehemu ya jukumu la kuongoza kanisa duniani.
Askofu Rowan Williams

Alisema mtu atayechukua nafasi hiyo ataweza kusafiri kwa urahisi, na hivo kumuacha Askofu Mkuu kushughulika zaidi na kuongoza kanisa.
Doctor Williams, ambaye anastaafu mwezi wa Disemba baada ya uongozi wa miaka 10, alikiri kuwa hakuweza kufanya mengi kuzuwia mgawanyiko kanisani juu ya swala la uhusiano wa jinsia moja.

Hofu ya vita kuhusu mpaka wa Sudan na S. Kusini


Mkutano wa Umoja wa mataifa kuhusu mzozo wa Sudan mbili
Balozi wa Marekani katika umoja wa mataifa Susan Rice, amesema mzozo kuhusu mpaka kati ya Sudan na Sudan Kusini huenda ukasababisha vita kuzuka tena kati ya nchi hizo mbili.
Bi Rice ametoa matamshi yake katika mkutano wa baraza la usalama la umoja wa mataifa kuhusu mzozo wa mpaka kati ya nchi hizo nchini Marekani.
Sudan Kusini imekubali mpango wa amani uliopendekezwa na Muungano wa nchi za Afrika ingawa Sudan imeukataa.
Nchi hizo mbili nusura zipigane mapema mwaka huu sababu kuu ikiwa mzozo wa mpaka na ugawanaji wa mapato ya mafuta .
Sudan Kusini ilipata uhuru wake kutoka kwa Sudan mwaka jana na kumaliza miaka mingi ya mapigano kati yake na Sudan.
Akiongea mjini New York, Bi Rice alisema kuwa hatua ya serikali ya Khartoum kukataa kusaini mpango wa amani inaweka nchi hizo katika hatari ya kurejelea vita.
Alisisitiza kuwa hatua ya kujikokota ya Khartoum inazua wasiwasi kuhusu kujitolea kwake kutatua mzozo huo.
Licha ya Sudan Kusini kukubali mpango wa amani, Bi Rice amekariri kuwa Marekani ina wasiwasi kwamba nchi hizo hazichukulii kwa uzito swala hilo kama ambalo linapaswa kushughulikiwa kwa dharura.
Muda wa mwisho uliowekwa na Umoja wa mataifa wa kuafikia makubaliano mwezi Agosti tarehe mbili, haukuweza kufikiwa na nchi hizo mbili.
Hata hivyo, pande hizo mbili zinashinikizwa kutia saini mpango huo wa amani ifikapo tarehe 22 mwezi Septemba.
Mwezi jana serikali za Khartoum na Juba zilifanya mkutano wa wiki tatu mjini Addis Ababa, Ethiopia.
Kwenye mazungumzo hayo, mwafaka ulifikiwa wa kugawana mapato ya mauzo ya mafuta ingawa bado mazungumzo zaidi yanahitajika kuhusu usalama.
Mazungumzo hayo yataendelea mwishoni mwa mwezi Agosti.
Majeshi ya Sudan yamepigana mara kadhaa na yale ya Sudan kusini tangu Sudan kusini kujipatia uhuru mwaka jana.
Huenda baraza la usalama la umoja wa mataifa likaziwekea vikwazo nchi hizo iwapo zitashindwa kukubaliana kusitisha mzozo huo katika eneo la mpakani.

Wahamiaji haramu matatani Italia

Wahamiaji haramu waokolewa
Walinzi wa mwambao kutoka shirika la majeshi ya muungano ya NATO wanawatafuta manusura wa boti iliyozama ufuoni mwa kisiwa cha Lampedusa ambapo mtu mmoja alifariki na wengine wengi bado hawajulikani waliko.
Manusura wengine 56 wakiwemo wanawake wajawazito wameokolewa kutoka kwenye boti hiyo iliyozama mapema leo asubuhi.
Kisiwa cha Lampedusa ambacho kiko umbali wa kilomita 120 kutoka Tunisia, ni eneo ambalo hutumiwa na wahamiaji wengi haramu wa kiafrika kuingia barani Ulaya kwa sababu ya ukaribu wake kwa bara hilo.
Maafisa wanasema kuwa idadi ya watu waliokuwa kwenye boti hiyo heunda ikawa zaidi ya miamoja ikilinganishwa na idadi iliyokuwa imeripotiwa awali.
Baadhi ya manusura waliokolea kutoka baharini na wengine walikuwa kwenye sehemu ya kisiwa hicho ambako hakuishi watu.
Msemaji wa walinzi wa NATO, alinukuliwa akisema watu 56 wamepatikana wote raia wa Tunisia.
Mnamo siku ya Alhamisi, watu 56 walizama wengi wao wakiwa watoto baada ya boti yao kuzama Magharibi mwa pwani ya Uturuki.
Wengine 45 waliokuwa kwenye boti hiyo walinusurika.
Wahamiaji hao haramu walikuwa wairaqi, raia wa Syria na wapalestina wakikimbilia barani Ulaya.
Kulingana na shirika la kimataifa la Amnesty International, mnamo mwaka 2011, takriban watu 1,500 walizama katika bahari ya Mediterranea wakiwa njiani kuelekea barani Ulaya.
Wengi walikuwa wanatoroka vurugu nchini Tunisia na Libya,wakati wa harakati za mageuzi katika nchi za kiarabu.

Mashambulizi ya kulipiza kisasi Kenya

Ramani ya Kenya
Takriban watu kumi na moja wa kabila la Pokomo wameuawa katika mashambulizi mapya ya kulipiza kisasi katika eneo la Tana River,Kusini Mashariki mwa Kenya.
Mtu mmoja aliyeshuhudia tukio hilo alisema alisikia watu wakipiga mayowe wakati kijiji kimoja kilipokuwa kinashambuliwa na kisha wenyeji kuteketezwa.
Eneo hilo ambako zinaishi jamii za kuhamahama ni kitovu cha mizozo ya ardhi na maji kati ya jamii za Orma na Pokomo.
Watu wengine kumi walijeruhiwa kwenye uvamizi huo uliotokea usiku wa kuamkia leo.
Uvamizi huu umetokea baada ya mashambulizi mengine kutokea mwezi jana ambapo watu 52 kutoka jamii ya Orma wengi wakiwa watoto na wanawake kuuawa kwa kunyongwa na kuteketezwa kiasi cha kutotambulika.
Ni katika tukio ambalo lilitajwa kuwa ghasia mbaya za kikabila kutokea katika miaka ya hivi karibuni nchini Kenya. Polisi na viongozi wa kijamii walisaidia kutuliza hali na kurejesha usalama kati ya jamii hizo mbili lakini hali ya wasiwasi iimeendelea kutanda.
Licha ya kwamba polisi waliahidi kuimarisha hali ya usalama katika eneo hilo, viongozi wa eneo hilo wanasema vikosi vya usalama vimeshindwa kuzuia ghasia.
Mbunge wa eneo hilo, Danson Mungatana amewashtumu maafisa wa usalama kwa kushindwa kuchukua hatua za kuwalinda wananchi licha ya kufahamu mapema kwamba mashambulio yatatokea.
Jamii hizo mbili za Pokomo na Orma, zimekuwa zikizozana kuhusu matumizi ya ardhi na maji ambazo ni rasilimali adimu.
Wapokomo ni wakulima ambao hukuza chakula kando ya mto Tana wakati jamii ya Orma wakiwa wafugaji wa kuhamahama.

Friday, September 7, 2012

TANZANIA NCHI YANGU INAYOPOTEZA UHALISIA WAKE

Namshukuru Mungu kuzaliwa Tanzania, Nchi iliyobariliwa kila aina ya utajiri duniani, mwenyezi Mungu yupo pamoja nasi kwa kila kitu ndiomana nchi kama za mashariki ya mbali ulaya na amerika zimetajirika kupitia maliasili za watanzania tuliolala usingizi bila kujua wapi tunaelekea na hii baiskeli yetu ya miti, kwanza napenda kutoa pole kwa ndugu zetu wote waliopoteza maisha kwenye matukio tofauti kama mabomu ya Mbagala na Gongo la mboto,kuzama kwa meli ya MV BUKOBA,MV SPICE, MV SKAGIT, tumepoteza nguvu kazi kubwa ya taifa, lakini yote tisa sijui ni tatizo nini ukiuliza tumeunda tume tuwaachie tume wafanye kazi yao, yakitokea tena oooh nimakosa yakimaumbile sisi ni ngumu kuyazuia, wenzetu
wanazidi kuteketea, nchi inaingia gizani wawakilishi wetu wanakula rushwa wanaanza kurushia vijembe bungeni mambo yanapita hakuna hatua zilizochukuliwa, dah inaumiza sana, hivi napenda kuuliza tunaangalia maisha ya mjini tu au na watu wa kijijini tumewasahau, kwa sababu inasikitisha kuniambia uchumi umekuwa wakati watu zaidi ya milioni kumi hawajui watakula nini pale wanapofika muda husika kwa sababu hata shilingi mia moja hawana mfukoni. Mnamo mwaka 2010 nilibahatika kufanya utafiti katika mkoa wa Rukwa wilaya ya sumbawanga vijijini jimbo la kwela kuhusu kushuka kwa elimu katika mkoa wa Rukwa, ni masikitiko makubwa sana pale ukiipata hiyo taarifa nafikiri serikali ifike pahala iseme kuna maeneo tumeshindwa kufikia              malengo na watoe taarifa kwa nini wameshindwa hili hata wananchi watafute namna nyingine ya msaada hili wajikomboe na tatizo hili la uchumi.
Madini ya Tanzanite
Tatizo lingine vijana wakitanzania tuliowengi tunapenda mijadala ambayo haijengi nchi ni kubomoa nchi kwa sababu ya itikadi ya chama, na pili tumeshajiwekea katabia kakutofanya kazi sijui tunategemea nini, jamani hii nchi hawa jamaa wanaipeleka sehemu ambapo palipo tufanya tuwaone wakoloni wabaya, na watu wa kurekebisha hayo maswala ni sisi si wao, sasa tufike pahala jamani watanzania wenzangu tuangalie maisha haya na nchi yetu inapokwenda. ni mtazamo wangu
 
 Vijana wakiwa kijiweni na baada ya hapo ni kwenye pombe tu na mambo mengine sasa je tutaweza kujikwamuwa hapa tulipo na kwenda mbele licha tu ya kukosa ajira hata wenyewe kujishughulisha hatuwezi jamani.Hebu jamani tujufunze kutoka china,Watu wa China wanafanya kazi sana ndiomana hata nchi yao inakuwa kiuchumi si watu wakukaa tu kama hapa kwetu