NJOMBE

NJOMBE

Saturday, March 31, 2012

TAASISI YA HASSAN MAAJAR TRUST YAANZISHA DUKA LA HISANI MIKOCHENI

 Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro akizungumza katika uzinduzi wa duka la hisani la taasisi ya Hassan Maajar Trust uliofanyika kwenye jengo la Arcade Mikocheni jijini Dar es salaam, ambapo duka hilo linauza vifaa mbalimbali zikiwemo ngua za kiume, nguo za kike, viatu N.K.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Hassan Maajar Trust Zena Maajar Tenga akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika asubuhi hii Mikocheni jijini Dar es salaam.
 Wageni mbalimbali wakipata kifungua kinywa katika hafla hiyo.
 Wageni waalikwa katika uzinduzi huo wakibadilishana mawazo.
 Watoto kutoka shule ya msingi ya Ushindi Mikocheni wakiimba wimbo wa taifa katika hafla hiyo.
 Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro, katikati ni Mgoyela.
Mjumbe wa Taasisi ya Hassan Maajar Trust Zuhura Sinare Murro akionyesha ngua zilizopo katika duka hilo.
 Wageni waalikwa wakiangalia nguo katika duka hilo.
Mdau Fredrick  Njoka  akiangalia suti katika duka hilo.
Habari na matukio na Full Shangwe

RAIS JAKAYA KIKWETE KATIKA TUZO ZA (AJET) USIKU HUU DIAMOND JUBILEE

 Rais Jakaya Kikwete akiongea na Fili Karashani Mwandishi mkongwe naambaye ameshinda  tuzo ya Maisha ya Mafanikio katika Tasnia ya Habari mwaka 2011, katika tuzo za (EJAT) zilizoandaliwa na Baraza la Habari Nchini Tanzania (MCT) na washirika wake, hafla hiyo inafanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee usiku huu, katika picha kushoto ni Mwandishi wa siku nyingi Khamis Ben Kiko.
 Rais Jakaya Kikwete akimkabidhi Nevil Meena cheti cha ushindi wa jumla kwa katika tuzo hizo mara baada ya kutangazwa rasmi.
 Kikundi cha Ngoma za asili cha Simba Thietre kikitumbuiza katika tuzo hizo.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mapunda akikabidhi tuzo kwa mwandhishi wa habari wa Mlimani Radio Tuma Dandi mshindi wa habari za watu wenye ulemavu- Redio
 Mhariri wa gazeti la Tanzania Daima Absalom Kibanda akikabidhi tuzo kwa Abdallah Majura Mkurugenzi wa Radio Sports FM ya Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya bia ya Serengeti Graham Anderws akimkabidhi cheti na zawadi yake Nevil Meena kutoka gazeti la Mwananchi.
 Mkurugenzi wa kampuni ya Executive Solution Agrey Maleale akimkabidhi zawadi yake Khamis Hamad kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo.
 Katibu Mtendaji wa MCT Bw. Kajubi Mukajanga akizungumza katika hafla hiyo.
Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mkurugenzi wa Makampuni ya IPP Bw. Reginald Mengi walipkutana katika hafla hiyo.

NATHAN MPANGALA MCHORAJI BORA WA KATUNI, ASHINDA TUZO YA (EJAT)

.Nathan Mpangala Kwa wiki kadhaa sasa yuko mafunzoni nchini Mexico, akihudhuria kozi fupi ya waandishi wa habari, inayohusu Civil Resistance and Non violence Conflict. Hapa akiwa na baadhi ya washiriki wenzake toka sehemu mbalimbali duniani, wakiandaa michoro kwa ajili ya video itakayotumika kwenye kampeni ya familia zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki kutokana na mauaji ya kila siku yanayohusishwa na biashara ya dawa za kulevya.
Nathan Mpangala pia usiku huu ameshinda tuzo ya wachoraji bora wa katuni katika tuzo za (AJET) zilizoandaliwa na Baraza la Habari (MCT) zinazofanyika usiku huu kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.
Hapa wakiendelea na kazi yao ya kuandaa katuzi hizo zinazohusu mauaji yanayotokana na  madawa ya kulevya nchini Mexico.

HAFLA YA KUTOA TUZO ZA (EJAT) KWA WANAHABARI YAFANYIKA USIKU WA 30 MARCH DIAMOND JUBILEE

  kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee ambapo kunafanyika hafla kubwa ya utoaji wa tuzo ya Umahili wa uandishi wa habari kwa mwaka wa 2012 zinazoandaliwa na Baraza la Habari MCT na washirika wake ambapo mgeni rasmi ni Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Kikwete.
Wamejitokeza wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo wasomi na waandishi wa habari wakongwe kama picha ya kwanza inavyoonekana kutoka kulia ni Profesa Aisha Yahya Othman mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mlimani, Jenrrali Ulimwengu, Jaji Mstaafu Thomas Mihayo aliyesimama na Profesa Shivji kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam wakiwa katika hafla hiyo usiku huu.
 Hawa ni miongoni mwa majaji kulia ni Itillio Tagalile, Afisa Uhusiano wa Tanesco Badra Masoud na Wenceslaus Mushi wakijadili jambo.
 Kushoto ni Awaichi Mawala kutoka Zantel na Mkurugenzi Msaidizi wa CCBRT Haika Mawala
 Wageni waalikwa kutoka mashirika mbalimbali nao wamehudhuria katika hafla hiyo.
 Majaji wakiwa katika meza yao.
 Mwenyekiti wa bodi ya TANAPA Modestus Lilungulu  kushoto na mjiumbe wa bodi Dk.Marcelina Chijoriga kulia wakiwa katika hafla hiyo.
 Waziri wa habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Katibu mtendaji wa Baraza la Habari MCT Kajubi Mukajanga.
 Mhariri kutoka magazeti ya Uhuru na Mzalendo Jaquiline Liana akizungumza na Mkurugenzi wa Gazeti la Jambo Leo Juma Pinto kulia.
 Clement Mshana Mkurugenzi wa Shirika la Utangazaji TBC akizungumza na Profesa Helmasi Mwansoko Mkurugenzi wa Utamaduni Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
 Wadau kutoka Shelutete kutoka TANAPA na Geofrey Tengeneza kutoka TTB nao wapo katika hafla hiyo.

 Wanaharakati kutoka taasisi mbalimbali nao wamejongea katika hafla hiyo.
 Kutoka kulia ni Mbunge wa Kondoa Kusini akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Michezo kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Leonard Thadeo.
 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa kampuni ya bia ya Serengeti Teddy Mapunda akiwa katika picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji na Mkurugenzi wa Fedha wa Kampuni ya bia ya Serengeti Graham Anderws
 Bendi ya Msondo ikitumnuiza katika hafla hiyo.
Mzee wa Kammbi popote Antonio Lugas akiwa na mdau Abel Onesmo kutoka Clouds FM

FLORA MBASHA KUTUMBUIZA TAREHE 1 APRIL NCHINI MAREKANI

Mwimbaji maarufu Afrika Mashariki katika medani ya Muziki wa Injili Flora Mbasha yuko ziarani kwa mwezi sasa nchini marekani kwaajili ya huduma ya tar1 april hapa ni mchanganyiko wa wanamuziki mbalimbali maarufu wa nyimbo za injili katika mazoezi ya nyimbo zitakazoimbwa.

Hapa Flora alikuwa akielezea jinsi ya kuitikia nyimbo zake zote atakazoimba, baada ya ziara nchini Marekani mwimbaji huyo anategemea kuelekea nchini Canada kwa wiki moja kisha Uingereza kwa wiki 1 tena na kurudi nyumbani Tanzania.

Vionjo vikipikwa..

Kushoto ni mpiga piano maarufu sana na ndiye mwalimu wa sauti na anasimamia music ni music dirrector pia ndiye mwandaaji wa marathon hapa Boston kwa wale wanaojua kukimbia Tanzania fursa ipo pembeni aliyesimama ni mpiga Bass maarufu sana ni mkali mno anapiga Bass utasema ni mashine inapiga kumbe ni vidole tu.

Hapa kitu kinapikwa..

Aaaah mwana wa kwetu..

Chagua pozi kali Pozi namba 1.

Au Pozi namba 2.

Nani kaona mboga?

Meneja ambaye vilevile ni mume wa Mwanamuziki wa injili Flora Mbasha, Emanuel Mbasha akiwa na wenyeji wake.

Flash ya pamoja

DIAMOND APIGA SHOW KALI, WEMA SEPETU AKITIA AIBU UKUMBINI


 Msanii wa Muziki wa kizazi kipya Ommy Dimpozzz akifanyiwa mahojiano mara baada ya kuwasili kwenye tamasha la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya, Diamond Platinum akiwarusha mashabiki waliohudhuria katika tamasha lake la Diamond Are Forever lililofanyika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 Diamond akionyesha umahili wake wa kuimba.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
...Kumbe jini kisilani kaingia katika utamu wa penzi langu, alikuwa akiimba
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 ...hapa alikuwa akimwaga mauno mbele ya mashabiki waliohudhuria.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
Janeth Sostenes akifanya mahojiano na Godwin Gondwe.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
...Aha! madansa wa Diamond wakiwajibika nae
 Mashabiki wa kutosha wakifuatilia show.
 ...Diambond akiwajibika vilivyo
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 ...Madansa wakiwajibika
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
  ...Safi sana 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
...Utata ulianzia hapa pale Dimond alishuka stejini na kwenda kwenye meza waliokuwa wamekaa akina Steve Nyerere na Mboni Masimba na ndipo alipopewa t-shirt ambayo kwa mujibu wa udadisi na uchunguzi wa udadavuzi wa mambo wa Kajuna Blog, ilisemekana kuwa t-shirt hiyo ilikuwa inapicha ya mwanadada ambaye alikuwa akitoa na Diamond kwa sasa. Na ilikuwa ni maalum kwa ajili ya kumrusha roho Wema Sepetu.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 ...Mwanadada Mboni Masimba akimkabidhi Diamond t-shirt huku Steve Nyerere akimtunza, vile vile alichukua t-shirt aliyopewa na kuipeleka kwa mwanadada Jokate Mwegelo.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 ...Hapa akikabidhiwa t-shirt na kupewa maelekezo mahali pa kuipeleka.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
...Baada ya hapo kumaliza lile movie la kwanza aliendelea na kupita katika meza mbali mbali huku akiwasalimia wageni waalikwa.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
...Akiimba na bendi ya Odama ambayo alimpa ushirikia mkubwa.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 ...Mauno yamekolea
 
 
 
 
...Akiendelea kutoa shukrani kwa wageni waliofika kumsapoti.



 Msanii wa Muziki wa Kizazi kipya Q-chief  akimpa sapoti mdogo wake Diamond
 ...Ehe! utata mkubwa ambao ulizuka ni hapa ambapo mwanadada huyu alimtuza dola za Kimarekani, Diamond
 ...Diamond aliendelea kuimba huku mwanadada huyo akimtunza huku akitoa tabasamu na kicheko
 Mwadada huyo hapa alikuwa amemaliza na kuondoka kwa mikogo..
Baada ya Diamond kurudi stejini ndipo mwanadada Wema Sepetu alienda kumtuza na pesa zake kukataliwa. Wema alikaa akimbembeleza kwa muda wa dakika 10 japo zoezi lake halikufanikiwa.
 ...Diamond aliendelea kuwajibika huku Wema akijaribu kumbembeleza
 ...Bembeleza, bembeleza na wewe jamaa ndiyo aliendelea kuwajibika
 ...Ndipo alipochukia na kuzitupia hizo hela stejini huku akiondoka huku akiwa amenuna
 ...Shamim Mwasha akilaumu kitendo alichokifanya Diamond cha kukataa hela alizoenda kutuzwa na Wema... 'Haiwezekani hii ni aibu sana'
Pesa alizokataa kuzichukua zikiwa zimetupwa 
 ...Hapa alipiga kitu cha 'Nimpende Nani'
 ...Jokate na marafiki zake wakishangilia
 ...Baada ya tuio hilo kutokea Mange Kimambi alimuita mshereheshaji wa tamasha hilo, Taji Liundi na kumuomba amuite Diamond aje amuombe msamaha na ndipo Diamond akakataa.
 ...Diamond alishuka na kuelekea kwa mwanadada Jokate Mwegelo na kuanza kukata mauno.
 ...mwanadada Mboni Masimba akiwa amevaa t-shirt alizokuwa amevaa.
 ...Aha! nimependeza sana
Taji Liundi akimbembeleza Diamond ili aende nae kwa Wema ndipo Diamond akakataa. 


 
 ...Mwanadada Mariam (Miss Popular) akimfuta jasho Diamond wakati Taji Liundi akimbembeleza ili aende kwa Wema.
 ...Diamond akiserebuka na warembo
 Marafiki wa Wema Sepetu wakijaribu kumbembeleza wakati akimwaga chozi... huku watu wengine wakishangilia na kuimba aibu yetu au aibu yao???
 ...hapa mwanadada akijaribu kubembeleza bila matumaini.
 Msanii wa kizazi kipya, Ommy Dimpozzz akimpa sapoti Diamond...huku akitoa ushuhuda wa maisha yake na    ya Diamond walipotoka.
 ...baada ya ujumbe wa Ommy Dimpozz, Diamond alimwaga chozi na hapa alikuwa akijifuta.
 Amini nae hakuwa nyuma kumpa sapoti
 ...Barnaba, Amini na Diamond wakiwajibia
Baada ya Barnaba kuimba wimbo wa 'Napembelezwa' ndipo mwanadada Wema alienda kumtuza na kutoa machungu yake. Kwa mujibu wa uchunguzi na maoni ya watu mbali mbali walikiona kitendo cha Wema Sepetu kwenda mbele kumtuza Diamond ni sawa na kujidhalilisha na kuhusishwa na mambo ya kishirikina.
Pia Justmine Loyce Bobbie alisema: Kwanini Wema anamfatafata mtoto wa watu kila kona? amuache na maisha yake jamani.. mbona Diamond hamfatilii lol, YATAMSHINDA